Mocumentary
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 771
- 1,960
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Dkt. Charles Mahera amesema licha ya mafanikio makubwa ambayo taasisi hiyo inajivunia anapitia kipindi kigumu kwani amepokea barua ya vitisho kutoka nje ya nchi kuhusu masuala ya uchaguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Mahera amesema amepokea barua hiyo kutoka kwa raia wa Marekani anayefahami kama kwa jina la Robert Amsterdam akiitisha NEC."Kwa hiyo kama Taifa mjue ni majaribu tuliyonayo ambayo haya majaribu lazima muendelee kuyaombea," amesema Mahera.
Aidha, amekemea vitendo vya baadhi ya watu ksema kuwa fulani atakwenda The Hague (Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu) na amewataka kutumia muda huo kueneza sera na si vitisho. Kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba28 mwaka huu, NEC imesema kuwa tayari yamekamilika kwa asilimia 80.
Taasisi hiyo imewaonya wananchi kuto kuuza vitambulisho vya kupigia kura, badala yake wavitunze iliwatimize haki yao ya msingi.
Chanzo: Swahilitimes
View attachment 1584785
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Mahera amesema amepokea barua hiyo kutoka kwa raia wa Marekani anayefahami kama kwa jina la Robert Amsterdam akiitisha NEC."Kwa hiyo kama Taifa mjue ni majaribu tuliyonayo ambayo haya majaribu lazima muendelee kuyaombea," amesema Mahera.
Aidha, amekemea vitendo vya baadhi ya watu ksema kuwa fulani atakwenda The Hague (Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu) na amewataka kutumia muda huo kueneza sera na si vitisho. Kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba28 mwaka huu, NEC imesema kuwa tayari yamekamilika kwa asilimia 80.
Taasisi hiyo imewaonya wananchi kuto kuuza vitambulisho vya kupigia kura, badala yake wavitunze iliwatimize haki yao ya msingi.
Chanzo: Swahilitimes
View attachment 1584785