Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 2,439
- 6,691
Wakuu,
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Dkt. Ayub Rioba Chacha, ameitaka jamii kutambua kuwa shirika hilo ni mali ya umma na si mali ya chama chochote cha siasa.
Hata hivyo, amesisitiza kuwa ni muhimu kufahamu kuwa kwa chama kilichopo madarakani pamoja na serikali yake, TBC itaonekana kutoa kipaumbele zaidi kwa uongozi uliopo kutokana na uhitaji wa umma kufahamu kinachoendelea serikalini.
Dkt. Rioba amesema wananchi wana haki ya kujua kila kinachofanywa na serikali yao, kwani maamuzi na shughuli za serikali zinaathiri moja kwa moja maisha yao ya kila siku.
Amesema kutokana na hilo, taaluma ya habari hulazimisha shirika hilo kuelekeza nguvu zaidi katika kuhabarisha wananchi kuhusu utekelezaji wa shughuli na mipango ya serikali.
Dkt. Rioba ameeleza kuwa mtazamo huo ndiyo unaofanya TBC mara nyingi kuonekana kutoa nafasi kubwa kwa serikali na chama kilichopo madarakani, hali inayosababisha baadhi ya watu kulinasibisha shirika hilo na Chama Cha Mapinduzi (CCM) au kulipa majina yanayoashiria kukiegemea chama hicho au serikali.
Dkt. Rioba ameyasema hayo leo Februari 6, 2026, katika mahojiano maalumu kuhusu mafanikio ya miaka 10 ya mageuzi ya TBC, akijibu swali lililotaka kufahamu sababu zinazofanya shirika hilo kwa muda mrefu lionekane kuhusishwa zaidi na CCM au kuonekana kuwa upande wa serikali.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Dkt. Ayub Rioba Chacha, ameitaka jamii kutambua kuwa shirika hilo ni mali ya umma na si mali ya chama chochote cha siasa.
Hata hivyo, amesisitiza kuwa ni muhimu kufahamu kuwa kwa chama kilichopo madarakani pamoja na serikali yake, TBC itaonekana kutoa kipaumbele zaidi kwa uongozi uliopo kutokana na uhitaji wa umma kufahamu kinachoendelea serikalini.
Dkt. Rioba amesema wananchi wana haki ya kujua kila kinachofanywa na serikali yao, kwani maamuzi na shughuli za serikali zinaathiri moja kwa moja maisha yao ya kila siku.
Amesema kutokana na hilo, taaluma ya habari hulazimisha shirika hilo kuelekeza nguvu zaidi katika kuhabarisha wananchi kuhusu utekelezaji wa shughuli na mipango ya serikali.
Dkt. Rioba ameeleza kuwa mtazamo huo ndiyo unaofanya TBC mara nyingi kuonekana kutoa nafasi kubwa kwa serikali na chama kilichopo madarakani, hali inayosababisha baadhi ya watu kulinasibisha shirika hilo na Chama Cha Mapinduzi (CCM) au kulipa majina yanayoashiria kukiegemea chama hicho au serikali.
Dkt. Rioba ameyasema hayo leo Februari 6, 2026, katika mahojiano maalumu kuhusu mafanikio ya miaka 10 ya mageuzi ya TBC, akijibu swali lililotaka kufahamu sababu zinazofanya shirika hilo kwa muda mrefu lionekane kuhusishwa zaidi na CCM au kuonekana kuwa upande wa serikali.