Katika hali inayoashiria kwamba mambo si shwari ndani ya Chama cha mapinduzi Kikao cha Baraza la Halmashauri ya Wilaya Mkuranga leo kimevunjika majira ya saa 5.30 asubuhi muda mfupi nbaada ya kufunguliwa na Mwenyekiti wake.
Sababu za kuvunjika kikao hicho ni kuwepo kwa kundi kubwa la madiwani wasiokuwa na imani na Mkurugenzi wa halmashuri hiyo Bi. Sipora Liana. Itakumbukwa kuwa Mwezi April pia Kikao kilichoitishwa kwa dharura hakikumalizkia licha ya kuendelea mpaka saa 3 usiku.
Kiufupi Madiwani wengi walishamkataa huyu Mama muda mrefu mpaka kumlazimu aliyekuwa Waziri wa Tamisemi George Mkuchika kuingilia kati na kusuluhisha ugomvi huo lakini mgogoro uliibuka tena baada ya Mkurugenzi kumtuhumu Afisa Utumishi (Bw.Mbuba ambaye alihamishiwa ghafla wilaya ya Ngara) kwamba ameshirikiana na madiwani kuandikia barua ya isiyokuwa na jina wala sahihi na kuisambaza kwa madiwani wengine ili wamkatae Mama huyo.
Baada kufanya uchunguzi wa kutosha madiwani wakajiridhisha kwamba barua hiyo haikupita masjala kuu kwa hiyo hakukuwa na ushahidi kama hiyo barua haikuandikwa na yeye mwenyewe Mkurugenzi ili kupata sababu ya kumwondoa DHRO.
Ndipo ilipofika leo majira ya saa 5 hivi baada ya kikao kufunguliwa madiwani walitaka kujua hatima ya agenda ya kikao cha mwezi wa 4 ambapo taarifa zilipelekwa kwa Mwantumu Mahiza (Mkuu wa Mkoa wa Pwani) ili aunde tume jambo ambalo halikutekelzwa.
Baada ya kupata majibu ytasiyoridhisha Diwani mmoja baada ya mwingine wakaanzakuvua majoho na kutoka nje na mwisho wa siku walibaki madiwani 7 wafuasi wa Mwenyekiti, mkurugenzi mpamoja na Mbunge wake (Mh Adam Malima ambaye naye alikuwepo). Kwa utaratibu ni kuwa na kuwa na angalau nusu ya wajumbe ilibidi kikao kiahirishwe kwa kuwa walibaki ndani wajumbe 7 kati ya 25 walikuowepo/wanaotakiwa kuwepo.
Wanabodi ni lazima mkumbuke kuwa huyu ndio yule Mama aliyemkamatisha Mbunge na rushwa ya sijui Milioni 2?!!!! Mbunge wa Bahi Omar Badwell.
Nini kinaendelea baadae nitaendelea kuwajuza. Source Mimi Mwenyewe nilikuwepo kwenye tukio
Sababu za kuvunjika kikao hicho ni kuwepo kwa kundi kubwa la madiwani wasiokuwa na imani na Mkurugenzi wa halmashuri hiyo Bi. Sipora Liana. Itakumbukwa kuwa Mwezi April pia Kikao kilichoitishwa kwa dharura hakikumalizkia licha ya kuendelea mpaka saa 3 usiku.
Kiufupi Madiwani wengi walishamkataa huyu Mama muda mrefu mpaka kumlazimu aliyekuwa Waziri wa Tamisemi George Mkuchika kuingilia kati na kusuluhisha ugomvi huo lakini mgogoro uliibuka tena baada ya Mkurugenzi kumtuhumu Afisa Utumishi (Bw.Mbuba ambaye alihamishiwa ghafla wilaya ya Ngara) kwamba ameshirikiana na madiwani kuandikia barua ya isiyokuwa na jina wala sahihi na kuisambaza kwa madiwani wengine ili wamkatae Mama huyo.
Baada kufanya uchunguzi wa kutosha madiwani wakajiridhisha kwamba barua hiyo haikupita masjala kuu kwa hiyo hakukuwa na ushahidi kama hiyo barua haikuandikwa na yeye mwenyewe Mkurugenzi ili kupata sababu ya kumwondoa DHRO.
Ndipo ilipofika leo majira ya saa 5 hivi baada ya kikao kufunguliwa madiwani walitaka kujua hatima ya agenda ya kikao cha mwezi wa 4 ambapo taarifa zilipelekwa kwa Mwantumu Mahiza (Mkuu wa Mkoa wa Pwani) ili aunde tume jambo ambalo halikutekelzwa.
Baada ya kupata majibu ytasiyoridhisha Diwani mmoja baada ya mwingine wakaanzakuvua majoho na kutoka nje na mwisho wa siku walibaki madiwani 7 wafuasi wa Mwenyekiti, mkurugenzi mpamoja na Mbunge wake (Mh Adam Malima ambaye naye alikuwepo). Kwa utaratibu ni kuwa na kuwa na angalau nusu ya wajumbe ilibidi kikao kiahirishwe kwa kuwa walibaki ndani wajumbe 7 kati ya 25 walikuowepo/wanaotakiwa kuwepo.
Wanabodi ni lazima mkumbuke kuwa huyu ndio yule Mama aliyemkamatisha Mbunge na rushwa ya sijui Milioni 2?!!!! Mbunge wa Bahi Omar Badwell.
Nini kinaendelea baadae nitaendelea kuwajuza. Source Mimi Mwenyewe nilikuwepo kwenye tukio