Mkurugenzi wa Jiji Amtumbua Mganga Mfawidhi kwa kuwakimbia wagonjwa na kwenda kula Pasaka

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha,Dkt Maulid Madeni amemtumbua wadhifa wake Mganga Mfawidhi wa kituo cha Afya cha Ngarenaro,Dkt.Japhet Kivuyo na kuwa Mganga wa kawaida kwa kosa la kutoroka kazini na kwenda kula pasaka na kuwaacha solemba wagonjwa waliokuwa wakisubiri kutibiwa

Tayari dkt Madeni amemteua Dkt David Mng'anya kushika nafasi yake huku akiunda tume ya kuchunguza tukio hilo na tabibu wengine katika jiji la Arusha wenye tabia kama hiyo ya kutoroka kazini bila taarifa hasa siku za sikukuu.

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa hatua hiyo imekuja kufuatia sauti iliyonaswa na kurushwa kwenye mitandao ya kijamii ,ambapo mkuu huyo wa kituo alisikika akibishana na viongozi wa Kamati ya siasa ya ccm kata ya Levolosi waliotembelea kituoni hapo wakitekeleza majukumu yao, akidai yupo kanisani na hawezi kurudi kazini kwa sababu ni kipindi cha sikukuu.

" Hatua ya kwanza tuliochukua ni kumvua uongozi ili iwe fundisho kwa tabibu wengine wenye Tabia kama hii ,wananchi wanapaswa kuhudumiwa muda wote kwa Massa 24 na si vinginevyo"Alisema Dkt Madeni

Dkt,Madeni aliwaomba radhi wananchi waliopatwa na adha hiyo ambao walikuwa katika kituo hicho cha afya wakihitaji Huduma ya matibabu.

"Kauli aliyoitoa si majibu ya kiuongozi yeye.kama kiongozi anapaswa kuwa kioo cha jamii ,kama ingetokea akaja mgonjwa mahututi na akafia pale nini kingetokea "

IMG_20190422_200334.jpeg
 
Sawa Mkurugenzi.

Mwenzako wa Itinga kawakataza Madaktari kuwawekea wagonjwa madrip au sindano.
Hahaha

Mwingine hataki bendera za chadema wilayani kwake.

Yani yeye jambo la Msingi ambalo kaona alisimamie kaona ni bendera. Chadema wenyewe haaruhusiwi kufanya kampeni

Ila huyu kiazi kashindwa ku recall kilichomtokea baba yake Lipumba na CuF yake .


Ukija huku dsm mwenzake jiji chafuu kila kona ila amekomaa na Pierr.
Hahaha
 
Sawa Mkurugenzi.

Mwenzako wa Itinga kawakataza Madaktari kuwawekea wagonjwa madrip au sindano.
Hahaha

Mwingine hataki bendera za chadema wilayani kwake.

Yani yeye jambo la Msingi ambalo kaona alisimamie kaona ni bendera. Chadema wenyewe haaruhusiwi kufanya kampeni

Ila huyu kiazi kashindwa ku recall kilichomtokea baba yake Lipumba na CuF yake .


Ukija huku dsm mwenzake jiji chafuu kila kona ila amekomaa na Pierr.
Hahaha
Mkuu msipende kutetea uzembe kazini. Majibu ya Dkt hayakuwa mazuri. Ni vema ukiwa kiongozi you mmust behave as one. Ndiyo hayo hayo ya Prof Assad, kiburi kiburi, kisa wewe ni professional
 
Mkuu yale majibu ya yule kada yalikua mazuri...mtu amekaa kazini mpk saa 9 jioni anaondoka unamwita kwa command ingekuwa kwako ungejisikiaje?
Mkuu unapokuwa kiongozi wa serikali haijalishi, muda wote unatakiwa uwe kiongozi na ndiyo maana kiapo kinasema hata kama umestafu kazi au kuacha uongozi you should behave like a leader! Dr alitakiwa aoneshe maturity yake na ujiniasi badala ya kuangukia mtego wa mwanasiasa, mwanasiasa kazi yake ni siasa, so alitakiwa kuwa calm!
 
Hivi ni nani alie msafi chini ya jua hili? Kwann huyo mkurungenzi hakufuata sheria za kumuadabisha? Tunajua hapa mwatetea uvundo haya la siegi limetoka wapi hapa kama si kutetea upuuzi na ushetwani? Kiburi cha siegi kiko wap? Tatizo lenu hamtaki kuambiwa ukweli... Ntasema kweli daima fitina kwangu mwiko!
Mkuu msipende kutetea uzembe kazini. Majibu ya Dkt hayakuwa mazuri. Ni vema ukiwa kiongozi you mmust behave as one. Ndiyo hayo hayo ya Prof Assad, kiburi kiburi, kisa wewe ni professional
 
Hivi ni nani alie msafi chini ya jua hili? Kwann huyo mkurungenzi hakufuata sheria za kumuadabisha? Tunajua hapa mwatetea uvundo haya la siegi limetoka wapi hapa kama si kutetea upuuzi na ushetwani? Kiburi cha siegi kiko wap? Tatizo lenu hamtaki kuambiwa ukweli... Ntasema kweli daima fitina kwangu mwiko!
Hakuna msafi na diyo maana kiongozi lazima uwe mtumishi
 
Sasa kama unaona kuwa Prpf Assad ana kiburi.

Basi hakuna hata haja ya kuendelea kubishana na wewe.
Upo level nyingine .
Upo ndungai level.
Prof Assad ni kiburi sana. Wewe umeambiwa tuyamalize hiyo kauli siyo unakiburi unasema msinitishe hahaha, kweli akili si mpaka uwe professor
 
No...sio kweli,nafikiri tukiendekeza hizi tabia wataambiwa hata namna ya kutibu...tambua huyu Dr ni mwanadamu anafanya kazi na anachoka...hawa watu wa chama wamefika wakati daktari ametoka....na kumbuka hiki kituo kina doctors 5 tu kwa mujibu wa kiongozi wa MAT wakati uhalisia wanatakiwa wawe 27...mtu kafanya kazi mpk jioni anakwenda jipumzisha mnavamia kituoni na mnaongoea maneno ya command...kwanza intention yao ilikua mbaya na ndio maana walirecord...pili kuna chain of command kwenye afya,sio kila mtu ana mamlaka ya kupiga simu kwa dr na akafanya unavyotaka.
Mkuu unapokuwa kiongozi wa serikali haijalishi, muda wote unatakiwa uwe kiongozi na ndiyo maana kiapo kinasema hata kama umestafu kazi au kuacha uongozi you should behave like a leader! Dr alitakiwa aoneshe maturity yake na ujiniasi badala ya kuangukia mtego wa mwanasiasa, mwanasiasa kazi yake ni siasa, so alitakiwa kuwa calm!
 
Back
Top Bottom