Mkurugenzi alivyoibua vituko kesi ya Kafulila

Mkurugenzi alivyoibua vituko kesi ya Kafulila

MKURUGENZI BABATI REUBEN MFUNE ALIVOIBUA VITUKO KESI YA KAFULILA HUKU MBUNGE ALOTANGAZWA AKIKATAA KUTOA USHAHIDI KUTHIBITISHA USHINDI WAKE.

Haya ndio maswali na majibu mahakamani wakati aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kigoma kusini ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa wilaya hiyo kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Babati baada ya uchaguzi huo. Kesi Kafulila anasema yeye ndiye aliyepata kura nyingi kwa mujibu wa matokeo ya fomu za kila kituo na chati au jedwali la matokeo ya kila kituo. Kafulila anadai kupata zaidi ya kura 34000 dhidi ya 32000 za Hasna Mwilima huku Hasna na msimamizi wakidai Hasna ndiye aliyepata kura zaidi ya 34000 dhidi ya 33000 za Kafulila kama matokeo yalivotangazwa

WAKILI:Unajua kusoma na kuandika.

MSIMAMIZI: NDIO

WAKILI: Matokeo ya ubunge alotangaza alishinda nani?

MSIMAMIZI :Hasna Mwalima wa CCM

WAKILI:Matokeo hayo yalipatikana baada ya kujumlisha fomu zipi?

MSIMAMIZI :Baada ya kujumlisha fomu na21B kutoka kila kituo kwa vituo vyote 382. ndipo Hasna akapata zaidi ya kura 34, 000na Kafulila zaidi ya kura 33000.

WAKILI : Hizo fomu unazijua?

MSIMAMIZI : Nazijua na kwasasa zililetwa mahakamani kwa amri ya Jaji.

WAKILI: Ukiziona hizo fomu utazikumbuka?

MSIMAMIZI : Ndio

WAKILI : Mhe Jaji naomba msimamizi apewe hizo fomu hapo

WAKILI: Una Hakika hizo fomu zikijumlishwa sasa hivi zitaleta Jumla ya matokeo uliyotangaza?

MSIMAMIZI : Sisi tulijumlisha kwa kutumia mashine

WAKILI : Kwani unahisi mashine na kawaida zinatoa jumla tofauti?

MSIMAMIZI : Hapana lakini nachosisitiza tulipojumlisha kwa kutumia mashine siku hiyo hayo ndio yalikuwa matokeo na vyama vya CCM, TADEA, DP na ACT wagombea wake walisaini.

WAKILI: Unaweza kutusomea matokeo ya kila fomu hizo ulizoshika ili tuone kama tutapata jumla uliyotangaza?

MSIMAMIZI :Siwezi

WAKILI : Kwann wakati unajua kusoma? au ni kiburi

MSIMAMIZI : Hapana, matokeo tulishajumlisha siku ya majumuisho baada ya uchaguzi na Kafulila alikuwepo sasa sijui unataka nini.

WAKILI : Umesema fomu hizo ndio ulizitumia kujumlisha na ndio zilitoa matokeo uliyotangaza na ndio umekuja kuthibitisha hapa mahakamani, Je upo tayari fomu hizo ziwe sehemu ya ushahidi wa mahakama ili zitumike kuhakiki matokeo uliyotangaza?

Akasimama wakili wa serikali Malata : Mhe Jaji wakili wa Kafulila asitake kutumia fomu za tume kuthibitisha madai yake, haiwezekani na hatupo tayari.

WAKILI: Kwa hiyo msimamizi unaposema ulitangaza matokeo hayo kwa fomu hizo na haupo tayari mahakama kuzitumia kama ushahidi wako maana yake nini?

MSIMAMIZI : Nimeshaeleza

WAKILI: Wakati unajibu madai ya KAFULILA kwanini hukuambatanisha fomu zako kama KAFULILA alivoambatanisha zake? na kukupa nakala?

MSIMAMIZI : Sikuona umuhimu kwa sababu mnazo nakala za mawakala wenu ambazo nisawa na tulizonazo

WAKILI : Kwa hiyo matokeo ya ushahidi tuliyonayo nisawa na fomu zako?

MSIMAMIZI : Ndio

WAKILI : Unafahamu jedwali la matokeo ya kila kituo?

MSIMAMIZI : Sifahamu kwasababu halipo kisheria

WAKILI: Naomba usome barua ya Mkurugenzi aliyokuandikia November 24, 2015

MSIMAMIZI : Imeandikwa nimpatie David Kafulila jedwali la matokeo ya kila kituo ya siku ya majumuisho.

WAKILI : Kwanini umesema hujui kitu hicho wakati Mkurugenzi wa uchaguzi alikuelekeza kwa barua umpatie Kafulila

MSIMAMIZI : Sikumwelewa Mkurugenzi wa uchaguzi labda aulizwe mwenyewe

WAKILI :Hiyo barua ulijibu?

MSIMAMIZI : Hapana, kwasababu Mkurugenzi wa uchaguzi alielekeza kitu ambacho hakipo

WAKILI : Kwanini hukumjibu hivyo?

MSIMAMIZI : Sikuona umuhimu huo

WAKILI : Naomba usome barua yako ya tarehe 13 Nov 2015

MSIMAMIZI :Imeandikwa toka msimamizi kujibu barua ya Kafulila aliyotaka chati hiyo ya matokeo ambapo imejieleza kuwa nilijibu chati hiyo imeshatumwa tume ya Taifa ya uchaguzi makao makuu

WAKILI : Awali ulisema hicho kitu hukijui sasa ulitumaje kitu usichokijua?

MSIMAMIZI : Hii chati au jedwali tulituma siku ile ile kwa njia ya mtandao

WAKILI : Kwanini ulisema hukijui

MSIMAMIZI. Haipo kisheria

WAKILI : Sasa barua ya Mkurugenzi tume ya Nov 24, Mkurugenzi anakuelekeza umpatie chati au jedwali hilo Kafulila wakati barua yako ya Nov 13 unasema ulishatuma Tume. Nani anajichanganya Kati yako msimamizi na Mkurugenzi wa Tume?

MSIMAMIZI : Labda aulizwe Mkurugenzi mwenyewe wa Tume

WAKILI :Kwanini ulihamishwa baada ya kuharibu matokeo?

MSIMAMIZI : Nilikuwa na likizo na hivyo baada ya likizo baada ya uchaguzi na baada ya likizo kwisha Disemba nikaunganishwa uhamisho January.

WAKILI : Mhe Jaji nimemaliza maswali yangu.

Tunapotezeana mda tu!!!!
Kama hali ndiyo hiyo basi huyo Husna ajitahidi kutumia kamshara kake vizuri maana soon atakabidhi ofisi kwa Kafulila
 
Kwa mahakama hizi na majaji hawa wenye mrengo wa yule aliyegombeaga URAIS kupitia chama flani.Kafulila akishinda naomba nipigwe BAN..

Hapa nauona Mtego wa uhuru wa mahakama,Mwanza Hakimu ameshindwa kutumia Haki yake ya uhuru wa kufanya maamuzi kwa taaluma aliyosomea.Ngoja tusubiri na huyu je atatenda kulingana na taaluma yake au Bahasha ya Khaki?
 
MKURUGENZI BABATI REUBEN MFUNE ALIVOIBUA VITUKO KESI YA KAFULILA HUKU MBUNGE ALOTANGAZWA AKIKATAA KUTOA USHAHIDI KUTHIBITISHA USHINDI WAKE.

Haya ndio maswali na majibu mahakamani wakati aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kigoma kusini ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa wilaya hiyo kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Babati baada ya uchaguzi huo. Kesi Kafulila anasema yeye ndiye aliyepata kura nyingi kwa mujibu wa matokeo ya fomu za kila kituo na chati au jedwali la matokeo ya kila kituo. Kafulila anadai kupata zaidi ya kura 34000 dhidi ya 32000 za Hasna Mwilima huku Hasna na msimamizi wakidai Hasna ndiye aliyepata kura zaidi ya 34000 dhidi ya 33000 za Kafulila kama matokeo yalivotangazwa

WAKILI:Unajua kusoma na kuandika.

MSIMAMIZI: NDIO

WAKILI: Matokeo ya ubunge alotangaza alishinda nani?

MSIMAMIZI :Hasna Mwalima wa CCM

WAKILI:Matokeo hayo yalipatikana baada ya kujumlisha fomu zipi?

MSIMAMIZI :Baada ya kujumlisha fomu na21B kutoka kila kituo kwa vituo vyote 382. ndipo Hasna akapata zaidi ya kura 34, 000na Kafulila zaidi ya kura 33000.

WAKILI : Hizo fomu unazijua?

MSIMAMIZI : Nazijua na kwasasa zililetwa mahakamani kwa amri ya Jaji.

WAKILI: Ukiziona hizo fomu utazikumbuka?

MSIMAMIZI : Ndio

WAKILI : Mhe Jaji naomba msimamizi apewe hizo fomu hapo

WAKILI: Una Hakika hizo fomu zikijumlishwa sasa hivi zitaleta Jumla ya matokeo uliyotangaza?

MSIMAMIZI : Sisi tulijumlisha kwa kutumia mashine

WAKILI : Kwani unahisi mashine na kawaida zinatoa jumla tofauti?

MSIMAMIZI : Hapana lakini nachosisitiza tulipojumlisha kwa kutumia mashine siku hiyo hayo ndio yalikuwa matokeo na vyama vya CCM, TADEA, DP na ACT wagombea wake walisaini.

WAKILI: Unaweza kutusomea matokeo ya kila fomu hizo ulizoshika ili tuone kama tutapata jumla uliyotangaza?

MSIMAMIZI :Siwezi

WAKILI : Kwann wakati unajua kusoma? au ni kiburi

MSIMAMIZI : Hapana, matokeo tulishajumlisha siku ya majumuisho baada ya uchaguzi na Kafulila alikuwepo sasa sijui unataka nini.

WAKILI : Umesema fomu hizo ndio ulizitumia kujumlisha na ndio zilitoa matokeo uliyotangaza na ndio umekuja kuthibitisha hapa mahakamani, Je upo tayari fomu hizo ziwe sehemu ya ushahidi wa mahakama ili zitumike kuhakiki matokeo uliyotangaza?

Akasimama wakili wa serikali Malata : Mhe Jaji wakili wa Kafulila asitake kutumia fomu za tume kuthibitisha madai yake, haiwezekani na hatupo tayari.

WAKILI: Kwa hiyo msimamizi unaposema ulitangaza matokeo hayo kwa fomu hizo na haupo tayari mahakama kuzitumia kama ushahidi wako maana yake nini?

MSIMAMIZI : Nimeshaeleza

WAKILI: Wakati unajibu madai ya KAFULILA kwanini hukuambatanisha fomu zako kama KAFULILA alivoambatanisha zake? na kukupa nakala?

MSIMAMIZI : Sikuona umuhimu kwa sababu mnazo nakala za mawakala wenu ambazo nisawa na tulizonazo

WAKILI : Kwa hiyo matokeo ya ushahidi tuliyonayo nisawa na fomu zako?

MSIMAMIZI : Ndio

WAKILI : Unafahamu jedwali la matokeo ya kila kituo?

MSIMAMIZI : Sifahamu kwasababu halipo kisheria

WAKILI: Naomba usome barua ya Mkurugenzi aliyokuandikia November 24, 2015

MSIMAMIZI : Imeandikwa nimpatie David Kafulila jedwali la matokeo ya kila kituo ya siku ya majumuisho.

WAKILI : Kwanini umesema hujui kitu hicho wakati Mkurugenzi wa uchaguzi alikuelekeza kwa barua umpatie Kafulila

MSIMAMIZI : Sikumwelewa Mkurugenzi wa uchaguzi labda aulizwe mwenyewe

WAKILI :Hiyo barua ulijibu?

MSIMAMIZI : Hapana, kwasababu Mkurugenzi wa uchaguzi alielekeza kitu ambacho hakipo

WAKILI : Kwanini hukumjibu hivyo?

MSIMAMIZI : Sikuona umuhimu huo

WAKILI : Naomba usome barua yako ya tarehe 13 Nov 2015

MSIMAMIZI :Imeandikwa toka msimamizi kujibu barua ya Kafulila aliyotaka chati hiyo ya matokeo ambapo imejieleza kuwa nilijibu chati hiyo imeshatumwa tume ya Taifa ya uchaguzi makao makuu

WAKILI : Awali ulisema hicho kitu hukijui sasa ulitumaje kitu usichokijua?

MSIMAMIZI : Hii chati au jedwali tulituma siku ile ile kwa njia ya mtandao

WAKILI : Kwanini ulisema hukijui

MSIMAMIZI. Haipo kisheria

WAKILI : Sasa barua ya Mkurugenzi tume ya Nov 24, Mkurugenzi anakuelekeza umpatie chati au jedwali hilo Kafulila wakati barua yako ya Nov 13 unasema ulishatuma Tume. Nani anajichanganya Kati yako msimamizi na Mkurugenzi wa Tume?

MSIMAMIZI : Labda aulizwe Mkurugenzi mwenyewe wa Tume

WAKILI :Kwanini ulihamishwa baada ya kuharibu matokeo?

MSIMAMIZI : Nilikuwa na likizo na hivyo baada ya likizo baada ya uchaguzi na baada ya likizo kwisha Disemba nikaunganishwa uhamisho January.

WAKILI : Mhe Jaji nimemaliza maswali yangu.

Tunapotezeana mda tu!!!!
acha shanga wewe! Kwani maswali yaliulizwa na wakili wa tumbili pekee? Kwanza thibitisha ulichoandika.
 
Hata akishindwa Dunia itakuwa imejua ukweli wa Mambo

Dunia kujua ukweli haisaidii maana hata kule Burundi dunia nzima wanafahamu vizuri sana kuliko huo uchaguzi wa Kigoma ila hadi sasa hiyo dunia haijafanya lolote kwa Nkurunzinza
 
Hapa nauona Mtego wa uhuru wa mahakama,Mwanza Hakimu ameshindwa kutumia Haki yake ya uhuru wa kufanya maamuzi kwa taaluma aliyosomea.Ngoja tusubiri na huyu je atatenda kulingana na taaluma yake au Bahasha ya Khaki?
Mkuu hivi unafikiri huyo Msimamizi kiburi anakitolea wapi?!!.Hapa jamaa kashinda lakini je,haki itatendeka?Muda ndio utakua mwamuzi wa mwisho..
 
Hivi Wenje hajakata rufaa au sheria haziruhusu.
Ninaweka marekebisho ya post yangu:
Ile ya Wenje mahakama ilungana na washtakiwa (CCM) kukataa kupokea form namba 21b kama ushahidi. Hii ya Kafulila mahakama imekubali ila ilikuwa kwa mbinde sana
 
Kama hawako tayari kushindwa kwa nini uwa wanaleta sanduku la kura mbele yetu?

Kila la heri Kafulila haki itasimama.
 
Kweli ni maajabu yaani nilitumia fomu hizo hizo kujumlisha na kupata mshindi, lakini kwa sasa sitaki kuzisoma na msizijulishe tena hapa nahakamani!!!!!!!!!!!!!!!!!

Unaweza kuwa na cheo kikubwa na mamlaka makubwa sana na fedha nyingi za kutupa and yet ukawa KILAZA, TEMBERE au KIAZI wa kutupa kabisa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom