Safi sana kuhusu maisha ya Patrick. Nafurahi kusikia hiyo ingawa inasikitisha sana. Naamini huyo mke waliachana maana mimi binafsi nilimfahamu Patrick akiwa anaishi Tandika Nyumba za NHC pembeni ya Magorofa ya Tandika. Alikuwa akipiga mziki na dada wa-Kizuru. Bahati mbaya hatukufahamu yote hayo tukadhani hakuwahi hata kuoa!
1. Patric alikuwa na mke saafi sana aliyekuwa akiitwa Lidia, na ndio maana aliwahi kutunga wimbo mmoja safi sana unaitwa "Dada Lida",
2. huyu Mwanamama wa Ki-zulu, kwa jila la "Ninie" alikuwa muimbaji wa Afro 70 wa muda mrefu sana, ambaye alikuwa ameamini sana in kipaji cha Patric cha muziki mpaka akawa hataki kurudi kwao, baada ya mambo kuanza kumuendea vibaya Patric kimuziki, alikimbiwa mpaka na ndugu zake wa karibu ambao alikuwa akipiga nao Afro 70, lakini ni huyu mama peke yake alisimama naye mpaka mwisho, ingawa mwishoni alikuwa akitumia sana ganja na huyu mama,
Maisha ni tambara bovu, ninakumbuka enzi za Patric akiongea na ku-hang out mpaka na mawaziri, hata kuonana na Mwalimu akiwepo chamwino kwake haikuwa taabu, ninakumbuka enzi zake akienda kurekodi album Nairobi na kurudi na vidudu, Patric ndiye aliyekuwa bina-adam wa kwanza kwangu kumuona amevaa Raizoni na Bugaluu au Pekosi, Patric ndiye mtu wa kwanza kunipeleka muziki nikiwa in the teenager, ninakumbuka hiyo siku yaani mara yangu ya kwanza kuona live bendi ya muziki ilikuwa bendi yake inapiga kwenye ukumbi wa kikosi cha Anga, Ukonga, mara yangu ya kwanza kuona watu wazima wanacheza mziki wa Dansi na hasa kukumbatiana, I was lost wallahi! maana pale waliletwa wasichana toka shule ya Jangwani yaani Hosteli,
He was a good man na pia alikuwa na mapungufu yake kama Bin-adam, alikuwa ni mstaarabu na pia alikuwa na heshima sana kwa wengine na hasa ndugu zake, ndio maana aliwaingiza wote kwenye bendi yake na kuwaleta mjini kutoka Dodoma, I mean ingawa maisha yalipokuja kumgeuka wote walimkana kabisaaa,
Patric alipenda sana muziki wa aina ya Osibisa, na alikubalika sana ki-muziki, maana nakumbuka hata ile siku Lwambo alipokuja bongo, alimpa nafasi sana ya kupiga naye pale uwanja wa taifa, lakini mwisho wa maisha yake ulikuwa ni fedheha kubwa sana, ukweli alichanganyikiwa kabisaa Mungu amuweke mahali pema!
Very very stupid with Mgonja.
Unafahamu kwamba sasa hivi Mgonja ni kama omba omba?
Ooh yah! siku moja niliwahi kumuona kwenye viwanja vya bunge Dodoma, yaani viongozi wetu wamemgeuza Ze -Comedy! Kweli mshahara wa Dhambi ni mauti!