Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,538
- 6,032
WanaJF,
Nimeingia leo KLH kwa MwanaKIJIJI na badala ya kupata ya makala niliyokuwa natafuta, nikaishia kusikiliza miziki ya zilipenda. Humo ndani nikafika na kukuta wimbo wa Patric Balisidya. Katika nyimbo zake nyingi, huu wa "NI MASHAKA" leo umenifanya niwe mnyonge sana. Naufahamu kwa miaka mingi ila miaka yote nilikuwa nashindwa kujua anaimba nini (ninamatatizo ya kuelewa mtu anaimba nini). Leo nimeusikiliza na kutafakari maneno yake. Inasikitisha sana kuwa tangu miaka ile hadi leo uonevu uko pale pale. Si ajabu wengine wanaoonea (mafisadi), wakati huo na wao walikuwa wanaonewa. Cha kusikitisha zaidi ni hili neno "WEMA HAWANA MAISHA". Ukiusikilza haraka haraka unaweza kusema watu kama Mwakyembe, Zitto, Mama Malecela, Dr. Slaa na wale wote wanaopigania HAKI YA MTANZANIA kila siku wanaweza KUKAA TAMAA. Lakini kabla hawajafanya hivyo nawaomba wakaangalie ile film ya Antonio BANDERAS iitwayo "The 13th Warrior (1999)." Humo kuna VIKING mmoja pamoja na kuwa alikuwa kachanjwa chale yenye SUMU na yule Kibibi Gura Malikia, na akawa mgonjwa hoi, walipomletea VITA mlangoni, alisimama na kuchukua Silaha yake na kwenda pigana (samahani kama nimechanganya) na walimuomba na kumwambia kuwa anaweza kufa alisema " ... binadamu POA ni yule anayeishi na akifa, vizazi vitamkumbuka na kumuwekea ukumbusho kama wa SANAMU, Mnara, Nyimbo nk. na si kuishi maisha marefu...." Mafisadi mnaotumia VITISHO, Mauwaji na taka nyingine kama za Mugabe mjue HISTORIA itawasau au itawakumbuka kwa upande wa HITLER, Savimbi, Stalin Joe, nk na si Upande wa Mashujaa kama Sokoine, Nyerere, Sankara, Ngwabi na Mashujaa wote wanaopingana na NYIE kwa sasa. Naomba huu wimbo uwe changamoto kwa wanaJF popote pale walipo. They will kill your body but your soul will keep GOING STRONG. Kwa bahati Tanzania siyo Russia maana huko kweli Mungu hayupo na SOUL za watu wema hupotea kimoja.... Kweli dawa ni moja tu nayo ni kuwa BEGA KWA BEGA na WEMA wetu. Mwenye kuweza kuweka maneno ya huu wimbo ntamshukuru sana.
Nimeingia leo KLH kwa MwanaKIJIJI na badala ya kupata ya makala niliyokuwa natafuta, nikaishia kusikiliza miziki ya zilipenda. Humo ndani nikafika na kukuta wimbo wa Patric Balisidya. Katika nyimbo zake nyingi, huu wa "NI MASHAKA" leo umenifanya niwe mnyonge sana. Naufahamu kwa miaka mingi ila miaka yote nilikuwa nashindwa kujua anaimba nini (ninamatatizo ya kuelewa mtu anaimba nini). Leo nimeusikiliza na kutafakari maneno yake. Inasikitisha sana kuwa tangu miaka ile hadi leo uonevu uko pale pale. Si ajabu wengine wanaoonea (mafisadi), wakati huo na wao walikuwa wanaonewa. Cha kusikitisha zaidi ni hili neno "WEMA HAWANA MAISHA". Ukiusikilza haraka haraka unaweza kusema watu kama Mwakyembe, Zitto, Mama Malecela, Dr. Slaa na wale wote wanaopigania HAKI YA MTANZANIA kila siku wanaweza KUKAA TAMAA. Lakini kabla hawajafanya hivyo nawaomba wakaangalie ile film ya Antonio BANDERAS iitwayo "The 13th Warrior (1999)." Humo kuna VIKING mmoja pamoja na kuwa alikuwa kachanjwa chale yenye SUMU na yule Kibibi Gura Malikia, na akawa mgonjwa hoi, walipomletea VITA mlangoni, alisimama na kuchukua Silaha yake na kwenda pigana (samahani kama nimechanganya) na walimuomba na kumwambia kuwa anaweza kufa alisema " ... binadamu POA ni yule anayeishi na akifa, vizazi vitamkumbuka na kumuwekea ukumbusho kama wa SANAMU, Mnara, Nyimbo nk. na si kuishi maisha marefu...." Mafisadi mnaotumia VITISHO, Mauwaji na taka nyingine kama za Mugabe mjue HISTORIA itawasau au itawakumbuka kwa upande wa HITLER, Savimbi, Stalin Joe, nk na si Upande wa Mashujaa kama Sokoine, Nyerere, Sankara, Ngwabi na Mashujaa wote wanaopingana na NYIE kwa sasa. Naomba huu wimbo uwe changamoto kwa wanaJF popote pale walipo. They will kill your body but your soul will keep GOING STRONG. Kwa bahati Tanzania siyo Russia maana huko kweli Mungu hayupo na SOUL za watu wema hupotea kimoja.... Kweli dawa ni moja tu nayo ni kuwa BEGA KWA BEGA na WEMA wetu. Mwenye kuweza kuweka maneno ya huu wimbo ntamshukuru sana.