Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti ni "makadirio"

Bajeti inayotakiwa kwenda kwa nchi wahisani ni ile iliyopitishwa na bunge au rasimu(draft)yake?Kama ni rasimu basi lazima wanapelekewa tena inayopitishwa bungeni kwakuwa hata wao hujua kuwa hiyo ni rasimu ya bajeti.Kwa nini sasa hawakupelekewa?Jibu ni moja.Draft waliyokuwa nayo ilikuwa inawanufaisha viongozi kwa namna moja au nyingine.Kama iliyopitishwa na bunge ingeongeza maslahi zaidi kwa viongozi zaidi ya draft waliyonayo wahisani,je wahisani wasingepelekewa bajeti hiyo haraka mara baada ya kupitishwa na bunge?Na je hili limetokea bajeti hii tu au na zilizopita?Watanzania tunaliwa na kuibiwa na hawa wezi wa kalamu.

Tatizo hawawezi kupeleka budget iliyokwisha kupitshwa kwani inaulaji wao sasa wanapeleka draft ili wawekezaje waone vile vipaumbele vyao vinatekelezwa. Ikisha wanabadilisha kuingiza makadirio yao kama vitafunio vya bilioni 2.5, samani za bilioni 6, magari ya bilioni 10 basi maisha kula kuku kwenda mbele. Halafu tunauliza maendeleo ya tanzania yanapatikana wapi?
 
Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti

Mwananchi, Wednesday, 08 December 2010
Raymond Kaminyoge

SIKU tatu
baada ya Kundi la nchi wahisani wa maendeleo ambalo zinachangia kwenye bajeti ya Tanzania (GBS) kuibua kashfa kuwa Serikali iliwapelekea bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo, ameibuka na kusema kilichokua kimepekwa kwao ni makadirio.

Alisema bajeti iliyowasilishwa kwa Shirika la Fedha Duniani (IMF) yalikuwa makadirio ambayo yalibadilishwa katika mchakato wa kuiandaa na kwamba bajeti iliyopitishwa na Bunge ndiyo inayotambulika.


Mkulo alisema hayo jana jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika mkutano wa kitaifa wa mwaka wa majadiliano ya kisera na bajeti.


“Kuna mchakato mrefu wakati wa kuandaa bajeti, tuliwapa makadirio ya bajeti yetu mwezi Aprili mwaka huu, baada ya hapo bajeti ilipitia kwenye Baraza la Mawaziri ambalo lilifanya marekebisho. Katika kipindi hicho kuna marekebisho yalifanywa hivyo kutofautiana na makadirio tuliyowapelekea wahisani,” alisema Mkulo na kuongeza:


“
Ndiyo maana nasema sijawahi kupeleka kwa wahisani bajeti tofauti na iliyopelekwa bungeni. Nasisitiza kuwa bajeti ni moja tu ambayo ndiyo hiyo niliyowasilisha bungeni baada ya kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri,” alisema.

Alisema ni utaratibu wa kawaida wahisani kupelekewa makadirio mapema, lakini mambo hubadilika kutokana na gharama eza kuendesha Serikali kubadilika”.


“
Msidhani Mkulo ndiye anayeandaa bajeti pekee yake, Baraza la Mawaziri ndilo lenye kauli ya mwisho kuhusu bajeti ya nchi, wanaweza kubadilisha chochote wakati wahisani mlishawapelekea bajeti yenu mapema,” alisema Mkulo.

Jumatatu wiki hii, Mwenyekiti wa kundi la wahisani wa maendeleo ambalo linachangia kwenye bajeti kuu ya Tanzania (GBS), Svein Baera, katika hotuba yake ambayo Mwananchi ina nakala, alisema serikali ilipeleka IMF, bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge.


Taarifa hiyo ilitolewa huku wahisani hao wakiwa wamezuia theluthi moja ya zaidi ya dola za Marekani 800 milioni ambazo zinatakiwa zichangiwe na wahisani kwenye Bajeti Kuu ya 2010/11, wakiishinikiza Serikali iharakishe utekelezaji wa programu ya mageuzi, yakiwemo ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma.


Baera alibainisha maeneo sita kuwa ndiyo mhimili wa mjadala wao na serikali.

"Napenda kuainisha maeneo sita ya ujumbe wetu ili kuweka sawa jukwaa la majadiliano yetu haya ya mwaka. Kuna tofauti kati ya bajeti iliyowasilishwa kwa bodi ya (Shirika la Kimataifa la Fedha) IMF na ile iliyopitishwa na Bunge Julai 2010," alisema Baera.

Alisema bajeti ambayo serikali iliwasilisha kwa wahisani hao ilibeba matumaini makubwa ya kuzaa matokeo mazuri na kufanywa kama sababu ya kupitisha matumizi makubwa ya fedha zinazotokana na mapato ya ndani".


Baera alisema kukosekana kwa uwazi katika matumizi, vipaumbele, mapato na mfumo mzima wa fedha kunapunguza kuaminika kwa bajeti hiyo mbele ya wafadhili.



My take:
1. Kwa nini imemchukua Mh Mkulo siku tatu kujibu shutuma wakati jibu alikuwa nalo kwa kuwa alihusika kwenye mchakato wote?


2. Je, kwa nini Mh Mkulo anasema budget inaandaliwa na watu wengi? Ina maana anataka kusema kosa hilo sio la kwake?

3. Kwa kuwa ofisi yake inahusika moja kwa moja kwa nini anatoa majibu ya kujihami badala ya kuchukua uamuzi wa kuijuzulu?

4. Je, Mkulo anataka kutuambia kuwa bajeti sio makadirio?


Hebu tuliangalie hili wana Jf

Mm,kuna tatizo. Ina maana makadirio yao miaka yote yanalingana na actual budget?Certainly not,sasa kwanini wastuke mwaka huu kama ndiyo kawaida?
 
This is not even a CCM issue. Mustapha Mkullo is a bloody imbecile... Sio bajeti ni makadirio wakati that is just the translation of the word budget. In another issue this would be funny to see some idiot just talk none sense but its our economy, the GBS people think he is an idiot ndio maana wakatangaza kashfa kwakuona huyu mtu ni mbuzi and they are right. The man has no idea what he is doing. In five years our economy will be as ridiculous as he is, unless God or JK waingilie, and at the moment it looks like the former is more likely.
 
Mkulo inabidi ajiwajibishe kabla hajawajibishwa. Kumbe hizi ndio tricks zinazochezwa kutuibia huh!!
 
mkuu umeuliza maswali ya msingi sana. Mimi nadhani ni vyema tukiangalia maneno ya mkulo kwa maana zaidi ya mbili.
1. Imechukua siku 3 kwa kuwa;
a. Hajui kinachoendelea hivyo wasaidizi wake walilazimika kutafuta sababu
b. Walikuwa wamechakachua na ilibidi watunge sababu.

2.bajeti inaandaliwa na watu wengi ana maanisha;
a.hakuna coordination nzuri ya ku-reconcile data kutoka pande husika (inefficiency)
b.timu ya wachakachuaji ilihusisha watu nje ya wataalam wa wizara, hivyo mahesabu hayakwenda sawa

3. Kwa nini hajiuzulu? Kwa sababu;
a. Haoni kosa ni hitlafu ndogo tu iliyotokea.
B. Kosa halikusababishwa na yeye bali ile timu ya wachakachuaji walioharibu mahesabu

4. Je bajeti si makadirio?
A. Nothing is set in stone, lkn bajeti ni realistic projection
b. Hawezi kukubali kuwa ni makadirio kwani itazua maswli mengi.

Kama jibu ya maswali yako yote ni (a) basi mkulo ni incompetent arrogant unreliable leader.
Kama jibu ni (b) basi mkulo ni scapegoat na anajua hilo hivyo anatuma ujumbe kwa wahusika - he is not taking this lying down!
Nawasilisha.



i concur!
 
This is not even a CCM issue. Mustapha Mkullo is a bloody imbecile... Sio bajeti ni makadirio wakati that is just the translation of the word budget. In another issue this would be funny to see some idiot just talk none sense but its our economy, the GBS people think he is an idiot ndio maana wakatangaza kashfa kwakuona huyu mtu ni mbuzi and they are right. The man has no idea what he is doing. In five years our economy will be as ridiculous as he is, unless God or JK waingilie, and at the moment it looks like the former is more likely.

Huyu bwana alishawahi kuulizwa ni kwa nini sarafu yetu inashuka thamani kwa kasi akajibu ni sababu ya kupanda kwa thamani ya EURO na kuyumba kwa thamani ya dola. Kama kweli tatizo ndilo hilo, mbona thamani ya hela ya Kenya na Brazil zinapanda? Hebu wataalam wa uchumi mtusaidie maana mpaka leo mimi namuona mkulo kama msanii. Ama hajui anachokiongea au anatufanya watanzania majuha.
 
WAHISANI WAMEPEWA BAJETI YA MKAZO KTK MAENDELEO YA JAMII,BUNGENI IKALETWA BAJETI YA MSISITIZO KTK UMASKINI NA MATUMIZI YA CHAI ZA SERIKALI MWANANCHI AUMIE!wana JF mmesahau hata waziri Wa mambo ya ndani aliyepita MASHA alikua hajui kuna magereza mangapi tanzania?anachojua ni viti na meza simu vilivyopo ofisini kwake nyamagana
 
Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti

Mwananchi, Wednesday, 08 December 2010
Raymond Kaminyoge

SIKU tatu
Alisema bajeti ambayo serikali iliwasilisha kwa wahisani hao ilibeba matumaini makubwa ya kuzaa matokeo mazuri na kufanywa kama sababu ya kupitisha matumizi makubwa ya fedha zinazotokana na mapato ya ndani".

Baera alisema kukosekana kwa uwazi katika matumizi, vipaumbele, mapato na mfumo mzima wa fedha kunapunguza kuaminika kwa bajeti hiyo mbele ya wafadhili.



[/FONT]
Tafakari sana.
Wafadhili walielezwa kwa njia ya bajeti (makisio) kuwa matokeo yatakuwa mazuri na hivyo nao wakaona wasaidie, kumbe sivyo
yaani haikuwa realistic, na walipofika level ya bunge wakabadilisha wakijua kuwa tayari wana ahadi ya kusaidiwa na wafadhili - huu ni utapeli.
Wabunge unawaambia vyanzo vya mapato kuwa ni pamoja na wahisani kumbe wahisani wenyewe umewadanganya! Wanapostuka - eti waje ofisini!
Kibaya zaidi ni ile kwamba kuna "kukosekana kwa uwazi katika matumizi, vipaumbele, mapato na mfumo mzima wa fedha" Natoa mfano: Waziri mkuu mwaka jana alisema kuwa serikali haitanunua magari ya kifahari, inawezekana katika bajeti waliyopelekea wafadhili walisema hilo, walipokuja bungeni wakachakachua wakasema tutanunua magari ya kifahari na wafadhili wamekubaliana nasi - bunge likapitisha. Baada ya magari kunuliwa ndipo wafadhili wanashtuka, mbona hayakuwemo kwenye bajeti (makisio)?
Hapo ndipo wanasema hakuna uwazi katika masuala ya fedha!
 
Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti

My take:
1. Kwa nini imemchukua Mh Mkulo siku tatu kujibu shutuma wakati jibu alikuwa nalo kwa kuwa alihusika kwenye mchakato wote?


2. Je, kwa nini Mh Mkulo anasema budget inaandaliwa na watu wengi? Ina maana anataka kusema kosa hilo sio la kwake?

3. Kwa kuwa ofisi yake inahusika moja kwa moja kwa nini anatoa majibu ya kujihami badala ya kuchukua uamuzi wa kuijuzulu?

4. Je, Mkulo anataka kutuambia kuwa bajeti sio makadirio?


Hebu tuliangalie hili wana Jf
[/QUOT

Mheshimiwa Mkullo has bee caught with his pants down.
Uswahili umezidi na hatuhitaji longo longo.
Mtanzania wa kawaida tu inabidi ajiulize kuwa sasa inabidi mfadhili au mtu wa nje akuambie kuwa umeteleza , wewe mwenyewe hujioni?
Kwamba ni bajeti ya kwanza, ya pili au makadirio ya kwanza au ya pili is nit the issue here , but openness and consistency.

It seems Mawizara yetu haya yamejaa half cooked economists na planners ambao hawana coordinator.
 
Hayo ndiyo madhara ya kuichagua CCM na JK. Mtegemee uozo kama huo forever as long as CCM rules. Swali langu ni, je Mkullo kwenye hiyo budget estimate anayodai alipeleka ilikuwa ndogo kuliko ilie actual bugdet au kubwa? Na kama alipeleka estimate kubwa zaidi kuliko actual budget na wahisani wakatoa pesa kubwa, je hiyo excess money kwenye actual budget imeanishwa/imeoneshwa imeenda wapi? Au ni nini kilio cha wahisani kuhusu bao walilopigwa?
 
Kwanza ni aibu mno kwa bajeti yetu kuwa inachangiwa na wahisani. Au aibu naiona mimi tu?
 
budget = makadirio. Huyu mkulo kasomea wapi ambapo panasema bajet siyo makadirio? . Mkisikia nimejinyonga ni kwa sababu ya Tz kuongozwa na mambumbumbu
 
msimulaumu sana ,maana ccm na viongozi wake wameshafikia ukomo wa kufikiria na wanafanya kila kitu kama desperate house wife ,maana kama ni kweli waziri huwezi ukamwambia yule mhisani aje ofisini kwake ili wayaongee, je inamaanisha nini? je alitaka kwenda kumchakachua/kum-fisadi/kum-takukuru///??? Ni aibu sana .hawa wanafikiria uchaguzi tu na si swala jingine.N abado tuna 5yrs hapo ndio tutakoma zaidi..
 
Ukisikiliza maelezo ya mataifa wahisani, kuna uwezekano kabisa tofauti hiyo ilifanywa kwa makusudi. Tofauti ya mapato ya serikali kati ya bajeti iliyopelekwa bungeni na kwa wahisani ni shilingi bilioni 700. Katika bajeti iliyopelekwa kwa wahisani ilikuwa ni pungufu katika mapato ya serikali kwa shilingi bilioni 700. Je, haiwezekani hii ilifanywa makusudi ili kuonesha nakisi kubwa zaidi katika bajeti ya wahisani ili wahisani watoe pesa nyingi zaidi kufidia nakisi ambayo haikuwepo? Na kama wahisani wangetoa, hiyo pesa ingetumika wapi wakati haikuwepo katika ile bajeti iliyopelekwa na kupitishwa na bunge? Je, hii ni mara ya kwanza kufanya hivyo au hii imekuwa ikifanyika na miaka mingine iliyopita? Itabidi kufanyike uchunguzi wa kutosha kwa miaka iliyopita ili kubaini kama ni mara ya kwanza kufanya hivyo au imekuwa ni desturi yao, na safari hii ilikuwa utimilifu wa, 'Za mwizi 40'.
 
Nadhni mimi kma mtanzania,siko proud 2 be tanzanian..wait just wait sababu kubwa yakufeel ths way,nipale vngozi wetu include our prezd wanapokua wanatalk na public wanajua sis nimaignorante..its make me sick.


Iliwasilishwa bajeti mbadala ya CDM. tafuta utaona!!
 
ni kweli kabisa kuwa hawa jamaa akili yao yote ni jinsi ya kubaki madarakani na sio jinsi ya kuboresha maisha ya wananchi; na ndiyo maana awamu hii ya lala salama ya kiwete hatafanya kitu cha maana kwa nchi hii isipokuwa kutuibia maliasili zetu yeye akishirikiana na wakina subash wake!! Mungu mkubwa anawaona na hukumu yao wataipata hapa hapa duniani; kwani wameishaanza kuadhibiwa kwa kulazimika kunywa maji na dawa hadharani hata kwenye gwaride!!

enhe sema hapo, wanakunywa dawa???
 
Iwe ni Makadirio ama Bajeti, swali langu mimi ni... Hivi kumbe ni lazima 'daftari' letu la Bajeti/Makadirio lazima lipitishwe kwa 'Mwalimu'/Mhisani aliwekee 'pata' ndio tuweze kuendelea na mambo mengine??? Miaka 49 baada ya Uhuru hatuna chochote tunachoweza kufanya wenyewe mpaka kwanza tukinge mabakuli kwa Wahisani?? Hivi nchi zote za Dunia ya Tatu ndio zinavyofanyiwa hivyo????
 
Kama alivyozoea kuwadanya WATZ basi anafikiri hata Wazungu wanadanganyika hivyo hivyo?
 
Back
Top Bottom