Mkopo toka benki ya Stanbic

m2me

Member
Jul 23, 2012
63
15
Wadau,

Naomba ufafanuzi wa sheria juu ya mikopo ya taasisi za fedha.
Nilichukua mkopo Stambic Bank kwa dhamana ya mshahara kutoka kwa mwajiri wangu lakini kabla sijamaliza mkopo huo kumetokea kuyumba kwa uchumi hapa kazini hali iliyopelekea kukosa mishahara kwa zaidi ya miezi sita sasa kutokana na shirika ninalofanyia kazi kutegemea wafadhili kwa 100%

Kutokana na hali hiyo mambo kadhaa yamejitokeza na kupelekea nijiulize maswali yafuatayo;

1. Ni kwanini kuwe na adhabu wakati benk inafahamu kuwa kwa sasa sina mshahara na dhamana yangu ni mshahara?

2. Kwa nini adhabu hiyo isianze kutumika baada ya tarehe ya mwisho ya urejeshaji mkopo (Oct, 2015)? Kwani katika kipindi hiki harakati ninazofanya zinaweza kuzaa matunda na hata nikaweza kurejesha kiasi chote hata kabla ya tarehe hiyo.

3. Mwajiri anawajibika vipi na deni hilo? Au nini msaada wake kisheria?

4. Je, ni sawa kisheria benk kupiga mnada mali za familia kama shamba, nyumba/gari amabavyo nimevipata nje ya mkopo huo?

5. Je, ni sahihi benk kuendelea kunipiga ‘fine’ hata baada ya kuonesha nia ya kurejesha kidogo kidogo kwa kadri ninavyopata?

Majibu ya maswali hayo yatanipa mwanga wakuu, naomba kuwasilisha.
 
Mkuu m2me wakati tunachukua mkopo kuna mkataba huwa tunasign ila wengi wetu hatusomi kilichoandikwa embu jaribu kuchukua ule mkataba usome kipengele hadi kipengele inawezekana ukapata majibu ya maswali uliyouliza.
 
Last edited by a moderator:
Nashukuru mkuu, ngoja niitafute ILA nakumbuka baada ya kuisaini ilirudishwa bank kwa ajili taratibu nyingine za kupatiwa mikopo na wala hatukurudishiwa mimi pamoja wafanyakazi wenzangu ambao tulichukua mkopo kwa wakati huo. Tulichopatiwa ni karatasi inayoonesha jinsi makato yatakavyokuwa yakifanyika. Yote kwa yote, nakumbuka hakuna kipengele kilichokuwa kikigusa hayo maswali yangu hapo juu.
 
Hivi ile bima inayolipiwa katika makato ya mkopo inasimamia nini hasa?
 
Mkuu m2me wakati tunachukua mkopo kuna mkataba huwa tunasign ila wengi wetu hatusomi kilichoandikwa embu jaribu kuchukua ule mkataba usome kipengele hadi kipengele inawezekana ukapata majibu ya maswali uliyouliza.

Shida zinatufanya tusisisitizie kusoma. Na zile terms and conditions ni nyingi mno na jamaa wanafanya kusudi kuziweka kwa small fonts uone uvivu na shida kuzisoma.
 
Mkuu rudi benki watakupatia hizo form huwa tunasign copy mbili. Zilirudishwa bank kwa ajili ya approval tu.
 
Nashukuru kwa michango yenu wakuu.. hapa nimefanikiwa kupata copy ya mkataba huo niliyo scan kabla ya kujaza (pdf)... kwa pamoja tushirikishane katika uelewa kwani kila nikiusoma sipati jibu la maswali yangu ya hapo juu.
 

Attachments

  • fomu za mkopo stanbic.pdf
    1.3 MB · Views: 195
Nashukuru mkuu, ngoja niitafute ILA nakumbuka baada ya kuisaini ilirudishwa bank kwa ajili taratibu nyingine za kupatiwa mikopo na wala hatukurudishiwa mimi pamoja wafanyakazi wenzangu ambao tulichukua mkopo kwa wakati huo. Tulichopatiwa ni karatasi inayoonesha jinsi makato yatakavyokuwa yakifanyika. Yote kwa yote, nakumbuka hakuna kipengele kilichokuwa kikigusa hayo maswali yangu hapo juu.
zili nakala zinatakiwa kuwa tatu ambopo ukishasaini wewe pamoja na mwajiri moja unatakiwa upewe wewe nakala moja pmj na mwajiri wako moja kama hujapewa fuatilia ni muhimu sana kuwa na nakala yako.
 
Mkuu

Nimepitia kipengele cha nane cha mkataba huo kinaonyesha kuwa pande husika hazina budi kuwasiliana kwa maandishi ikiwa kutatokea jambo lolote, hivyo tunaomba utujuze kama kipengele hicho kimetekelezwa?.

Huo ni Mchango wangu, lakini nategemea wajuzi zaidi watakuja kutoa ufafanuzi juu ya suala hili kwa manufa ya wakopaji wengine wa sasa na wajao.
 
Nashukuru mkuu, ngoja niitafute ILA nakumbuka baada ya kuisaini ilirudishwa bank kwa ajili taratibu nyingine za kupatiwa mikopo na wala hatukurudishiwa mimi pamoja wafanyakazi wenzangu ambao tulichukua mkopo kwa wakati huo. Tulichopatiwa ni karatasi inayoonesha jinsi makato yatakavyokuwa yakifanyika. Yote kwa yote, nakumbuka hakuna kipengele kilichokuwa kikigusa hayo maswali yangu hapo juu.

Ilitakiwa na wewe pia ubaki na nakala.......anyway kuna mambo kadhaa.... kwanza kwa uzoefu nilionao kama ni mkopo ambao haukuhusisha hati ya shamba or something like that unaweza kusepa na uwe tayari tu kupigiwa simu ila hawawezi kukufanya chochote zaidi ya kukutoa kwenye gazeti after some months or years hivyo usiogope kabisa.....

Pili kwa upande wa stanbic wana policy zao za kusubmit luku number ao namba ya dawasco kama ulisabmit wanakufatilia nyumbani kwako unless kama umepanga na unategemea kuhama hapo unapokaa ni vyema ila, utakuwa umemwachia landloard msala....... Hilo la kwanza nina jamaa yangu kashapiga bank tatu walipomtafuta kwenye simu hawakuweza kumpata na ni tokea 2010, so kama ni jasiri chukua option number 1.
 
Kwa mujibu wa sheria ya fedha unapokopa unapaswa kulipa endapo utakwama kulipa kwa mfululizo miezi 3 utakua umevunja mkataba na Mali ulizoweka dhamana zitakamatwa na dalali alieteuliwa na taasisi husika Kwa kukupa notisi ya siku 14, endapo mwajiri ndio mdhamini wako na ukafukuzwa kazi au kampuni ikafilisika Hazina zako za mafao Kama nssf zitatumika kulipa deni lako Kama hazitatosha taasisi ya fedha itaenda mahakamani kuomba kibali cha kukamata mali zako husika,...
Mara nyingi kutokana na uelewa Mdogo wa wakopaji wengi wamekuwa wakinyanyasika na mada lali either Kwa kunyang'anywa Mali zao bila notisi ya siku14 au kukamatiwa Mali ambazo si dhamana ya mkopo.
 
wandugu, nimejaribu zaidi ya mara nne kuomba mkopo benk lakini sikufanikiwa, kila nikifanya mchakato wa mkopo kwa ajili ya jambo fulani mchakato unavurugika katika hatua za mwisho kabisa na mara baada ya muda nafanikiwa kufanya jambo nililokusudia bila mkopo, mara ya mwisho nilifanya mchakato wote mwisho kabisa bank wakaniambia wamesimamisha mikopo kwa muda na ilikuwa imebaki miezi miwili kufikia deadline ya mipango yangu ajabu muda ulifika na nikafanikisha jambo hilo bila hata mkopo. nimekuwa nikijiuliza kwa nini inanitokea hivi nimekosa majibu.
 
Ilitakiwa na wewe pia ubaki na nakala.......anyway kuna mambo kadhaa.... kwanza kwa uzoefu nilionao kama ni mkopo ambao haukuhusisha hati ya shamba or something like that unaweza kusepa na uwe tayari tu kupigiwa simu ila hawawezi kukufanya chochote zaidi ya kukutoa kwenye gazeti after some months or years hivyo usiogope kabisa.....

Pili kwa upande wa stanbic wana policy zao za kusubmit luku number ao namba ya dawasco kama ulisabmit wanakufatilia nyumbani kwako unless kama umepanga na unategemea kuhama hapo unapokaa ni vyema ila, utakuwa umemwachia landloard msala....... Hilo la kwanza nina jamaa yangu kashapiga bank tatu walipomtafuta kwenye simu hawakuweza kumpata na ni tokea 2010, so kama ni jasiri chukua option number 1.

Aksante mkuu kwa ushauri wako, sikusubmit luku number wala ile mamlaka ya maji......
 
Mkuu hakuna mawasiliano yoyote kati ya benk na mwajiri au mimi mkopaji zaidi ya simu ya dalali!
 
Mkuu

Nimepitia kipengele cha nane cha mkataba huo kinaonyesha kuwa pande husika hazina budi kuwasiliana kwa maandishi ikiwa kutatokea jambo lolote, hivyo tunaomba utujuze kama kipengele hicho kimetekelezwa?.

Huo ni Mchango wangu, lakini nategemea wajuzi zaidi watakuja kutoa ufafanuzi juu ya suala hili kwa manufa ya wakopaji wengine wa sasa na wajao.

Mkuu, hakuna mawasiliano yoyote kati ya benk namwajiri au mimi mkopajizaidi yasimu ya dalali!
 
Back
Top Bottom