Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,935
- 30,280
MKONO WA BURIANI WA MAMA SYKES KWANGU
Hii picha nimepiga na mama Bi. Zainab Sykes tarehe 12 January 2021 nyumbani Mbezi.
Nilikuwa natoka kufanya kipindi cha Mapinduzi ya Zanzibar, Studio za Clouds Plus, nikaona kheri nimpitie Mama Sykes kumwamkia.
Nimemkuta ameshika mashafu yake anasoma ambayo ndiyo hiyo kwenye picha kaishika kwa mikono yake miwili.
Alikuwapo na mama mdogo Bi. Hawa tukazungumza kiasi cha kuzungumza na kama kawaida mama akanitembeza Memory Lane akinikumbusha mumewe Bwana Ally Sykes na kunichekesha.
Siku ile mvua kubwa ilikuwa imenyesha.
Nikaagana na mama na akaniombea dua na kunikumbusha nisipotee sana.
Ndiyo ilikuwa buriani.
Hii picha nimepiga na mama Bi. Zainab Sykes tarehe 12 January 2021 nyumbani Mbezi.
Nilikuwa natoka kufanya kipindi cha Mapinduzi ya Zanzibar, Studio za Clouds Plus, nikaona kheri nimpitie Mama Sykes kumwamkia.
Nimemkuta ameshika mashafu yake anasoma ambayo ndiyo hiyo kwenye picha kaishika kwa mikono yake miwili.
Alikuwapo na mama mdogo Bi. Hawa tukazungumza kiasi cha kuzungumza na kama kawaida mama akanitembeza Memory Lane akinikumbusha mumewe Bwana Ally Sykes na kunichekesha.
Siku ile mvua kubwa ilikuwa imenyesha.
Nikaagana na mama na akaniombea dua na kunikumbusha nisipotee sana.
Ndiyo ilikuwa buriani.