Mkoa wa Mtwara unafaa kuishi na biashara?

Mkoa wa Mtwara unafaa kuishi na biashara?

Delegate

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2012
Posts
331
Reaction score
203
Ndugu zangu
kuna mada inaendelea hapa jamvini kuhusu ushauri wa kurejea Tanzania,wote mliotoa ushauri nawashukuru sana na kwa taarifa tu ni kwamba nimeamua kurejea nyumbani!
sifahamu kuhusu mikoa mingi lakini kwa kuwa nina uwezo wa kuishi maisha yoyote yale ninatamani sana kwenda kuishi mtwara
najua mtwara ni mkoa uliosahauliwa sana na serikali yetu,lakini kwa kuwa kuna watu wanaishi ningependa kujua maisha ya palea yakoje??je wenyeji wa pale wanapenda wageni???je wana nia ya dhati ya kujiletea maendeleo?fursa za biashara zikoje pale??natamani kuijua mtwara!
 
Mtwara sijafika ila navyosikia sio ile ya zamani...watatuambia waliopo huko ila sasa inategemea ni biashara gani unazotaka kuzifanya maana ungeweka wazi hata sie wa mikoa mingine tungesema yetu kulingana na huku tulipo...na mayb kwa biashara unayofikiria ingefaa zaidi kwa mikoa ambayotungekutajia... Karibu bongo
 
tatizo la bei,linatokana na tatizo la kutokuwa na ushindani,barabara kutokamilika kwa wakati.
 
Inafaa kwa biashara yoyote kwan mabadiliko yameanza kuonekana after vyuo kufunguliwa na baadae mafuta na gesi.
 
Mtwara imebadilika sana, sana.
Fursa za biashara zipo nyingi tu, kwani wageni ni wengi sana. Sasa hivi Mtwara hakuna hoteli nzuri inayotoa huduma ya chakula, chakula kinapatikana kwa mama ntilie na kwenye mabaa mishikaki na chipsi. Kuna ongezeko la nyumba za kulala wageni lakini bado nyingi hadhi yake ni ya chini. Bado wananchi hawajaona fursa ya kulima mbogamboga na kufuga kuku na mbuzi, bado nyanya zinalimwa nje ya mkoa na kuletwa kwa malori ambazo hazitoshelezi soko. Matunda ni machache sana sokoni hata yaliyopo ni ya kiwango cha chini sana.
 
Asikudanganye mtu mtwara ni mji mzuri sana kuishi hasa kwa mtu anaefanya biashara aina yoyote .ila sio kwa mkulima! Binafsi niliishi mtwara kwa miaka sita ni wafanyabiashara tu wenye maisha ya uhakika na si wakulima.

Mtwara ni mji wenye maisha ghali sana kuliko arusha isipokuwa tu chumvi na mpenzi manake kwa shiling 500 unapata mpenzi hata kwa mkopo pia hadi utakapo pata . Ukitaka kuoa unatoa elfu 10 hadi 30.

Vitu madukani bei ya juu mno na vinatoka dar na msumbiji.

Viazi vya kutengeneza chips vinatoka dar . Nyama ya ngombe wanakula matajiri .

Kipato cha wananchi wa kawaida ni cha chini mno isipokuwa wachache wenye mashamba ya korosho wanapata nafuu kipindi cha msimu wa korosho.

Wakazi wa mtwara hasa vijana ni wavivu mno hawapendi kilimo isipokuwa wazee wanaolima jembe la mkono mazao kama mihogo mtama mpunga na vijana wachache kwenye uvuvi

Kuhusu Wakazi wa mtwara si wabaguzi ila ni tegemezi mno maana ukifika tu mtwara ukiwa mgeni wazee watakuomba wawe wazazi wako makaka na wadada uwe ndugu yao ili mradi tu unawajali kuwapa 500 ya unga sukari ya msokoto au dagaa
 
Mtwara imebadilika sana, sana.
Fursa za biashara zipo nyingi tu, kwani wageni ni wengi sana. Sasa hivi Mtwara hakuna hoteli nzuri inayotoa huduma ya chakula, chakula kinapatikana kwa mama ntilie na kwenye mabaa mishikaki na chipsi. Kuna ongezeko la nyumba za kulala wageni lakini bado nyingi hadhi yake ni ya chini. Bado wananchi hawajaona fursa ya kulima mbogamboga na kufuga kuku na mbuzi, bado nyanya zinalimwa nje ya mkoa na kuletwa kwa malori ambazo hazitoshelezi soko. Matunda ni machache sana sokoni hata yaliyopo ni ya kiwango cha chini sana.

umenena kweli kaka,hali ya hewa ikoje huko?
 
umenena kweli kaka,hali ya hewa ikoje huko?

Mtwara ina mabonde mengi yenye rutuba ya ajabu na maji mengi ya kutosha. Mfano bonde la mto Ruvuma ni kubwa ambalo linakaribia bonde la mto Kilombero kwa ukubwa, lakini ni sehemu ndogo sana iliyoendelezwa kwa ajili ya kilimo na ufugaji.

87L5y921UPN5 vavau7Oq1MV1ydoMon49vBwb7N3T0Wk4lEInE47GvwOBxhcJBAGMTjcVgMBoPBYDGY1wKHw LxuNe2QTwOj8PhcXgcFodGozFYLBaLRaHRaDQai8NisVg0CoXFYHA4HA6LxWKxuP8Ci8VgMRg8DovHYfFY7CAOR8DjSUQilUQmDw29hjg4SCISBnHY6OTkTD5f9 aFa1c6u9pa2i5D0AgoEYcm4TE8Fu11IP1fmX8yFOSICUkAAAAASUVORK5CYII=
 
Asikudanganye mtu mtwara ni mji mzuri sana kuishi hasa kwa mtu anaefanya biashara aina yoyote .ila sio kwa mkulima! Binafsi niliishi mtwara kwa miaka sita ni wafanyabiashara tu wenye maisha ya uhakika na si wakulima.

Mtwara ni mji wenye maisha ghali sana kuliko arusha isipokuwa tu chumvi na mpenzi manake kwa shiling 500 unapata mpenzi hata kwa mkopo pia hadi utakapo pata . Ukitaka kuoa unatoa elfu 10 hadi 30.

Vitu madukani bei ya juu mno na vinatoka dar na msumbiji.

Viazi vya kutengeneza chips vinatoka dar . Nyama ya ngombe wanakula matajiri .

Kipato cha wananchi wa kawaida ni cha chini mno isipokuwa wachache wenye mashamba ya korosho wanapata nafuu kipindi cha msimu wa korosho.

Wakazi wa mtwara hasa vijana ni wavivu mno hawapendi kilimo isipokuwa wazee wanaolima jembe la mkono mazao kama mihogo mtama mpunga na vijana wachache kwenye uvuvi

Kuhusu Wakazi wa mtwara si wabaguzi ila ni tegemezi mno maana ukifika tu mtwara ukiwa mgeni wazee watakuomba wawe wazazi wako makaka na wadada uwe ndugu yao ili mradi tu unawajali kuwapa 500 ya unga sukari ya msokoto au dagaa

Mkuu hebu funguka kidogo, bei ya vyumba vya biashara ikoje? Nyumba za kuishi (say chumba kimoja na sebule), bei za chakula zikoje, Mchele, mahindi, nyama, na vitu vingine vinavyofanya mjasiriamali asonge!
 
Nimeishi Mtr three years wakati nasoma chuo kikuu cha Stella Maris (SAUT), hakuna mji wenye mzunguko wa pesa kama Mtwara, tatizo wenyeji wa huko ni wavivu na hawawathamini wageni. Hali ya maisha ipo juu sana kuanzia vyakula mpk nyumba za kuishi, ila ktk dunia ya sasa mafanikio ni uthubutu, hebu nenda kapiganie ktk kile unachokiamini ila jiepushe sana na starehe ktk mji huo!
 
Umesema kweli kabisa na mzunguko wa hela mdoogo sana. Pia bado wanapenda ushirikina. Kwa mgeni tena unayeanza maisha sikushauri uende huko maana unahitaji utaowaajiri wawe wanajituma na kiasi fulani kukutia moyo pia majirani na jamii nzima. Kwa mtu uliyeishi nchi za mchakamchaka utakata tamaa. Kama unapenda kusini nenda iringa, njombe au mbeya kilimo kitakutoa hata biashara kidogo zinafaa na maisha sio expensive.
Asikudanganye mtu mtwara ni mji mzuri sana kuishi hasa kwa mtu anaefanya biashara aina yoyote .ila sio kwa mkulima! Binafsi niliishi mtwara kwa miaka sita ni wafanyabiashara tu wenye maisha ya uhakika na si wakulima.

Mtwara ni mji wenye maisha ghali sana kuliko arusha isipokuwa tu chumvi na mpenzi manake kwa shiling 500 unapata mpenzi hata kwa mkopo pia hadi utakapo pata . Ukitaka kuoa unatoa elfu 10 hadi 30.

Vitu madukani bei ya juu mno na vinatoka dar na msumbiji.

Viazi vya kutengeneza chips vinatoka dar . Nyama ya ngombe wanakula matajiri .

Kipato cha wananchi wa kawaida ni cha chini mno isipokuwa wachache wenye mashamba ya korosho wanapata nafuu kipindi cha msimu wa korosho.

Wakazi wa mtwara hasa vijana ni wavivu mno hawapendi kilimo isipokuwa wazee wanaolima jembe la mkono mazao kama mihogo mtama mpunga na vijana wachache kwenye uvuvi

Kuhusu Wakazi wa mtwara si wabaguzi ila ni tegemezi mno maana ukifika tu mtwara ukiwa mgeni wazee watakuomba wawe wazazi wako makaka na wadada uwe ndugu yao ili mradi tu unawajali kuwapa 500 ya unga sukari ya msokoto au dagaa
 
Mbona mtwara wachaga wamepiga kambi siku nyingi? Guest houses, bars, some shops ni za wachaga. Ila maisha mtwara mjini ni ghali sana baada ya kugundua gesi.


Mkuu huyo atakuwa hapajui Mtwara! Wachaga wanavyoutikisa mji ule vile yeye anasema hakuna wachaga?
 
Umesema kweli kabisa na mzunguko wa hela mdoogo sana. Pia bado wanapenda ushirikina. Kwa mgeni tena unayeanza maisha sikushauri uende huko maana unahitaji utaowaajiri wawe wanajituma na kiasi fulani kukutia moyo pia majirani na jamii nzima. Kwa mtu uliyeishi nchi za mchakamchaka utakata tamaa. Kama unapenda kusini nenda iringa, njombe au mbeya kilimo kitakutoa hata biashara kidogo zinafaa na maisha sio expensive.



Acha kumtisha mwenzako bila sababu, nahisi wewe unaongea kwa imaginations lakini haujafika Mtwara bado.Huo ushirikina unaousemea sijui umeushuhudia wapi. Nimeishi Mtwara Miaka 3 na bado huwa nakwenda huko mara kwa mara lakini huwezi kuniambia ushirikina wa Mtwara unaufikia ule wa kupiga nondo wa Mbeya na Iringa au wa kuua Albino wa Shinyanga.
Kwa miaka ya hivi karibu ni mkoa huu wazi kabisa naona maendeleo yake yanavyokwenda kwa kasi ya ajabu na watu wanamiminika kuinvest huko, kwa miaka michahce sana ijayo mikoa ya Lindi na Mtwara itakuwa populated sana kutokana na ugunduzi wa gesi pamoja na ujenzi wa viwanda kama cha theruji cha Dangote na cha mbolea ambavyo very soon vikishakamilika vinaanza uzalishaji. Hivyo ndugu mleta hoja usitishwe na huyu mdau nakushauri nenda physically ukafanye upembuzi yakinifu wewe mwenyewe uone. Tena nakushauri fanya haraka maana soon viwanja mjini bei yake itakuwa haishikiki sasa hivi tu kukipata lazima ujipange.

Wazo la investment kwenye kilimo cha mboga mboga na mahotel na guest house nakushauri ufanyie kazi kama wadau walivyosema hapo juu hii biashara itakulipa sana. Kuhusu ukarimu wa wamakonde wala usitie shaka ni wakarimu sana sema kupiga mizinga kwao ni kama sehemu ya maisha yao.
 
Umesema kweli kabisa na mzunguko wa hela mdoogo sana. Pia bado wanapenda ushirikina. Kwa mgeni tena unayeanza maisha sikushauri uende huko maana unahitaji utaowaajiri wawe wanajituma na kiasi fulani kukutia moyo pia majirani na jamii nzima. Kwa mtu uliyeishi nchi za mchakamchaka utakata tamaa. Kama unapenda kusini nenda iringa, njombe au mbeya kilimo kitakutoa hata biashara kidogo zinafaa na maisha sio expensive.

Hapo Mama Joe umechemka ndugu yangu, ni Heri aende Mtwara kuliko huko unakomwambia aende, huko wenyeji ni wajanja kuliko na hawataki mgeni aingize ushindani kwenye biashara zao, hawachelei kumpiga kipapai, labda apeleke biashara mpya kabisa ambayo wao hawaijui, lakini sjui aende kuuza hardware, sijui ajenge hotel wale ndugu zangu wana ukabila wa kuzidi mpaka wanabore! Mtwara ya sku hizi inafunguka sana, na ni sehemu yenye fursa mpya kwa mtu anayeanza ni nzuri zaidi ushindani mdogo na hivyo ni rahisi kukita mizizi kuliko hiyo mikoa mikubwa, labda aingie na mtaji mkubwa sana, hasa kwenye kilimo na ufugaji.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom