PreGE2025 Mkitaka reforms mkapige kura

PreGE2025 Mkitaka reforms mkapige kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Kuweni waangalifu. Hii ni dormant ID. Ipo tangu 2011. Hii ni ID ya kazi. Wenye D mbili bila shaka mtakuwa mmenielewa. Kuweni waangalifu!

View attachment 3364754
Waache waje..

Na ukiona hivi, maana yake dawa ya sindano za NO REFORMS NO ELECTION zimeingia sawasawa, wanatoka kupima upepo, kutafuta opinion....

Ukiona hivi, ujue ni giza limeingia kwa popo kutoka walikojificha...

Wewe hebu angalia tu hoja zake. Ni purely za ki - CCM...

Hana hata akili za kufikiri vyema...

Kwamba, tuingie kwenye uchaguzi kwa sheria na tume ileile iliyokwisha ku - prove failures halafu utegemee matokeo tofauti..?

Huyu jamaa Dr Adam Francis bila shaka udaktari wake ni wa kupewa tu na si wa kutumia akili darasani...

Ushauri wake huu, laiti ungekuwa ndio enzi za kina Nelson Mandela, basi South Africa mpaka leo ingekuwa bado chini ya wazungu wabaguzi wa rangi...!!

Ushauri wake huu, ungekuwa ndio wa enzi za Julius K. Nyerere na TANU yake, basi Tanganyika mpaka leo ingekuwa chini ya ukoloni wa Mwingereza...!!

Dr Adam Francis sikiliza bwana

Ule woga na utu kidogo wa kuruhusu chaguzi huru, za haki na za wazi kwa kiwango fulani kama ilivyokuwa back in 2015 na kurudi nyuma kwa sasa Tanzania haupo na hauwezekani tena...!!!

And actually the reason is very simple, na ni kwamba, CCM wameshakula nyama za watu na hawawezi kuacha kula asilani kwa maneno laini na ya kubembeleza unless itumike nguvu kuwafanya waache...!!

Kwa hiyo your advice is nonsense and it can't be accepted by free minded people..

Vita imeanza na haitakoma mpaka uhuru wa pili wa Tanganyika upatikane. We understand kwamba, you don't care anymore. Mnaweza kuendelea na kufanya mliyozoea kufanya, kujiweka kuwa viongozi kwa nguvu pasipo ridhaa ya wananchi. Endeleeni, lakini mna muda mfupi sana kufurahia matunda ya udhalimu wenu and THE PAYBACK IS COMING FAST BEFORE YOU...

Waambie CCM wenzakohivi, kama ina wanachama watiifu 13,000,000 kama inavyojidai, kwanini waogope uchaguzi huru, wa haki na wa wazI? Kwani wanaogopa ku - champion electoral system reforms kuanzia ktk katiba hadi kwenye sheria zetu za uchaguzi..?

Ni rahisi tu. Watanzania tunataka hicho, kisha twendeni kwenye uchaguzi kwa pamoja. Ashindae, ashinde kwa haki na ashindwaye, ampongeze aliyeshinda.

Mr Dr Adam Francis ugumu kwenye hili uko wapo? Kwanini mnang'ang'ania kuishi mkiwa mbeba roho ya wizi na dhuluma ndani yenu? Hamuogopi hukumu ya HAKI ya adhabu yenu toka kwa mwenyezi Mungu iliyo mbele yenu..?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
No election no reform, kura yangu ni ya thamani kubwa sana nitailinda kwa uwezo wangu wote!
 
Katika siasa, kaulimbiu na propaganda ndizo karata zinazounogesha mchezo wa uchaguzi. Kila mshindani wako anapochanga karata zake, timu yako lazime ichange karata zako. Hiki ndicho kilichotokea kuelekea October 2025.

Wakati CHADEMA wanaendelea na campaign ya No reform no election, CCM wamekuja na ilani ya uchaguzi inayoahidi katiba mpya ambayo kimsingi ndio reforms zinazodaiwa. Kwa lugha rahisi hili ni tamko thabiti kuwa, MKITAKA REFORMS, MKAPIGE KURA.

Sasa mpira upo kwa wapiga kura, kuhusu njia gani waitumie kupata reforms, kwa kushiriki uchaguzi kama wanavyohimizwa na CCM? Au kwa kuzuia uchaguzi kama wanavyohimizwa na CHADEMA. Nachelea kusema kama mnayo nia thabiti ya kuleta mabadiliko ya katiba, basi njia rahisi kati ya hizi ni kuchagua CCM.

Kwa faida ya wasomaji, Misingi na Malengo Kuu ya Ilani 2025-2030 ni kama ifuatavyo:
1. Kuendeleza Uchumi wa Viwanda na Biashara Ndogo (TEHAMA)
Kuimarisha mazingira ya biashara na kukuza uwezo wa viwanda vya ndani, pamoja na kuwawezesha wafanyabiashara wa TEHAMA kupitia mikakati ya kifedha na kiutawala.

2. Uboreshaji wa Huduma za Kijamii Vijijini
Kupanua upatikanaji wa maji safi, huduma za afya, elimu bora, na nishati kwenye maeneo ya vijijini kwa kuzingatia ufanisi na uendelevu.

3. Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.
Kupanda miti milioni 100 kila mwaka ili kudumisha misitu, kudumisha mazingira, na kuongeza mvua .

4. Kuimarisha Diplomasia ya Kiuchumi na Usalama wa Taifa
Kukuza ushirikiano wa kimataifa, kulinda rasilimali za taifa (gesi, madini, misitu), na kuimarisha usalama wa ndani na nje.

5. Katiba Mpya ya Muungano
Kwa mara ya kwanza, Ilani ya CCM imeipa kipaumbele kuongoza mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano ndani ya miaka mitano ijayo, ikilenga kujibu mahitaji ya kisasa kijamii, kiuchumi, na kisiasa
Chadema hawana sifa ya kushiriki uchaguzi.Wakiruhusiwa kushiriki uchaguzi nafungua kesi mahakamani
 
No reforms No election, ni wito wa mabadiliko ya uchaguzi au campaign against personality? It looks tunaongelea vitu viwili tofauti?
1. Ni wito wa mabadiliko ya mfumo mzima wa chaguzi zetu zote zinazotupatia viongozi wa kusimamia rasrimali asili zetu kwa maendeleo yetu wananchi na sio "mabadiliko ya uchaguzi" tu kama unavyowaza wewe...

2. You are asking if it's a campaign against personality, right..?

The answer is big YES. Kinachotoka ndani ya moyo wa mtu ndicho kinacho introduce na ku define personality ya mtu huyo. Ulichokiandika hapa kinatoka moyoni mwako, ndiyo personality yako. Tukipinga hoja zako, maana yake na personality (haiba) yako inakuwa destroyed moja kwa moja..!

So, be very carefully with what comes in your mind through your mouth because it can either destroy your reputation (personality) or maintain it..​

#NoReformsNoElection
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Katika siasa, kaulimbiu na propaganda ndizo karata zinazounogesha mchezo wa uchaguzi. Kila mshindani wako anapochanga karata zake, timu yako lazime ichange karata zako. Hiki ndicho kilichotokea kuelekea October 2025.

Wakati CHADEMA wanaendelea na campaign ya No reform no election, CCM wamekuja na ilani ya uchaguzi inayoahidi katiba mpya ambayo kimsingi ndio reforms zinazodaiwa. Kwa lugha rahisi hili ni tamko thabiti kuwa, MKITAKA REFORMS, MKAPIGE KURA.

Sasa mpira upo kwa wapiga kura, kuhusu njia gani waitumie kupata reforms, kwa kushiriki uchaguzi kama wanavyohimizwa na CCM? Au kwa kuzuia uchaguzi kama wanavyohimizwa na CHADEMA. Nachelea kusema kama mnayo nia thabiti ya kuleta mabadiliko ya katiba, basi njia rahisi kati ya hizi ni kuchagua CCM.

Kwa faida ya wasomaji, Misingi na Malengo Kuu ya Ilani 2025-2030 ni kama ifuatavyo:
1. Kuendeleza Uchumi wa Viwanda na Biashara Ndogo (TEHAMA)
Kuimarisha mazingira ya biashara na kukuza uwezo wa viwanda vya ndani, pamoja na kuwawezesha wafanyabiashara wa TEHAMA kupitia mikakati ya kifedha na kiutawala.

2. Uboreshaji wa Huduma za Kijamii Vijijini
Kupanua upatikanaji wa maji safi, huduma za afya, elimu bora, na nishati kwenye maeneo ya vijijini kwa kuzingatia ufanisi na uendelevu.

3. Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.
Kupanda miti milioni 100 kila mwaka ili kudumisha misitu, kudumisha mazingira, na kuongeza mvua .

4. Kuimarisha Diplomasia ya Kiuchumi na Usalama wa Taifa
Kukuza ushirikiano wa kimataifa, kulinda rasilimali za taifa (gesi, madini, misitu), na kuimarisha usalama wa ndani na nje.

5. Katiba Mpya ya Muungano
Kwa mara ya kwanza, Ilani ya CCM imeipa kipaumbele kuongoza mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano ndani ya miaka mitano ijayo, ikilenga kujibu mahitaji ya kisasa kijamii, kiuchumi, na kisiasa
Kwahiyo WEWE ulienda kusomea UJINGA mpaka level ya PHD?? Sio kwa matapishi haya ambayo walitakiwa wapost akina LUKAS 🤔🤔🤣🤣 kweli Kuna safari ndefu ya watu waanaojiita wasomi!! Yaani mtoa Uzi ana very POOR REASONING 😅😅😅🤣🤣🤔🤔
 
Ndio maana CCM inataka kufanya mabadiliko ya katiba, kwasababu sio chama cha kinyonyaji.
Ni kweli ccm wanaweza kufanya mabadiliko ya katiba, je ni mabadiliko yanayotakiwa na wananchi ama ni mabadiliko ya hila ili kusema tumeshaleta katiba mpya?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
5. Katiba Mpya ya Muungano
Kwa mara ya kwanza, Ilani ya CCM imeipa kipaumbele kuongoza mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano ndani ya miaka mitano ijayo, ikilenga kujibu mahitaji ya kisasa kijamii, kiuchumi, na kisiasa
Kwani katiba mpya si ilishaandikwa na CCM tokea 2014 ilisubiri kura ya maoni? Sasa mchakato mpya wa nini tena?

Yaani bunge lenye CCM 100% unatarajia litunge katiba yenye maslahi kwa nchi? Hilo litakua chaka la kupigia pesa tu.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Januari 02, 2015 - Aliyekuwa Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete alimteua George Mcheche Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, sasa Rais Samia amemtua kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania

Wanaojiita wanachama wa CCM someni hapa,kama hamtanielewa nitawaelewesha.

No Reforms,No election
 
Januari 02, 2015 - Aliyekuwa Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete alimteua George Mcheche Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, sasa Rais Samia amemtua kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania

Wanaojiita wanachama wa CCM someni hapa,kama hamtanielewa nitawaelewesha.

No Reforms,No election
Uteuzi huu unakutatiza nini?
 
Kwani katiba mpya si ilishaandikwa na CCM tokea 2014 ilisubiri kura ya maoni? Sasa mchakato mpya wa nini tena?

Yaani bunge lenye CCM 100% unatarajia litunge katiba yenye maslahi kwa nchi? Hilo litakua chaka la kupigia pesa tu.
Kutoka katika misaafu rasmi ya CCM, ni sera ipi uliyoiona inahatarisha maslahi ya nchi? Umezungumzia katiba mpya kukwama, Je, wabunge wa CHADEMA kususa kuendelea na majadiliano, hakukuwa na mchango kukwamisha mchakato? Si vyema kukipachika chama sifa ambayo huwezi kuithibitisha.
 
Hatudanganyiki, No Reforms No Election ndiyo mpango mzima.
 

Attachments

  • KURA YAKO.jpg
    KURA YAKO.jpg
    46.8 KB · Views: 9
Ni kweli ccm wanaweza kufanya mabadiliko ya katiba, je ni mabadiliko yanayotakiwa na wananchi ama ni mabadiliko ya hila ili kusema tumeshaleta katiba mpya?
Katiba mpya ni muafaka wa kitaifa, sio sera ya chama kimoja cha siasa. Katiba nzuri inatakiwa ijunuishe mawazo ya makundi yote ya wananchi, sio wanasiasa peke yao.
 
Katiba mpya ni muafaka wa kitaifa, sio sera ya chama kimoja cha siasa. Katiba nzuri inatakiwa ijunuishe mawazo ya makundi yote ya wananchi, sio wanasiasa peke yao.
Uko sahihi, tatizo kubwa wananchi wa nchi hii huwa hawana uthubutu wa kuweka wazi madai yao. Wanasiasa ndio wamekuwa wakifanya kazi hiyo. Kwasasa tunaona wanasiasa ndio wenye uthubutu wa kutaka katiba mpya, hayo makundi mengine yako kimya, ila siku mchakato ukianza utashangaa kuona hata ambao hawajawahi kutamka kwa bahati mbaya Katiba mpya, wakiwa mstari wa mbele kuonyesha walivyokuwa wanataka katiba mpya!

Matokeo yake na kuingiza mambo ya kuokoteza na hila za ccm. Ngoja tuone, ikiletwa katiba mpya ya kiccm bado tutaendelea kuidai hiyo katiba mpya.
 
Katika siasa, kaulimbiu na propaganda ndizo karata zinazounogesha mchezo wa uchaguzi. Kila mshindani wako anapochanga karata zake, timu yako lazime ichange karata zako. Hiki ndicho kilichotokea kuelekea October 2025.

Wakati CHADEMA wanaendelea na campaign ya No reform no election, CCM wamekuja na ilani ya uchaguzi inayoahidi katiba mpya ambayo kimsingi ndio reforms zinazodaiwa. Kwa lugha rahisi hili ni tamko thabiti kuwa, MKITAKA REFORMS, MKAPIGE KURA.

Sasa mpira upo kwa wapiga kura, kuhusu njia gani waitumie kupata reforms, kwa kushiriki uchaguzi kama wanavyohimizwa na CCM? Au kwa kuzuia uchaguzi kama wanavyohimizwa na CHADEMA. Nachelea kusema kama mnayo nia thabiti ya kuleta mabadiliko ya katiba, basi njia rahisi kati ya hizi ni kuchagua CCM.

Kwa faida ya wasomaji, Misingi na Malengo Kuu ya Ilani 2025-2030 ni kama ifuatavyo:
1. Kuendeleza Uchumi wa Viwanda na Biashara Ndogo (TEHAMA)
Kuimarisha mazingira ya biashara na kukuza uwezo wa viwanda vya ndani, pamoja na kuwawezesha wafanyabiashara wa TEHAMA kupitia mikakati ya kifedha na kiutawala.

2. Uboreshaji wa Huduma za Kijamii Vijijini
Kupanua upatikanaji wa maji safi, huduma za afya, elimu bora, na nishati kwenye maeneo ya vijijini kwa kuzingatia ufanisi na uendelevu.

3. Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.
Kupanda miti milioni 100 kila mwaka ili kudumisha misitu, kudumisha mazingira, na kuongeza mvua .

4. Kuimarisha Diplomasia ya Kiuchumi na Usalama wa Taifa
Kukuza ushirikiano wa kimataifa, kulinda rasilimali za taifa (gesi, madini, misitu), na kuimarisha usalama wa ndani na nje.

5. Katiba Mpya ya Muungano
Kwa mara ya kwanza, Ilani ya CCM imeipa kipaumbele kuongoza mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano ndani ya miaka mitano ijayo, ikilenga kujibu mahitaji ya kisasa kijamii, kiuchumi, na kisiasa
Watz hawahitaji Katiba mpya, wanahitaji huduma nzuri za afya, elimu bora, pesa za kuweka kujikimu kimaisha na kuweza kufurahia na familia zao.
 
Akili za ng'ombe ni za ng'ombe tu,hv mwaka jana nchi ilikuwa kwenye nn sio kwenye uchaguzi? nn kilitokea ww mwenye mtindio wa ubongo,naona kama vile umeweka kichwa pembeni umegeuza mnduku wako ndio unautumia kufikiri.Mm nakwambia NO REFORMS NO ELECTION ni muhimu hata kwako na kizazi chako ambacho naamini ipo siku kitakulaumu na kusikitika kwa ugonjwa ulioupata unaosababisha ww kunatumia mnduku kufikiri NO REFORMS NO ELECTION itakusaidia ili siku Moja Ukatibiwe India baada ya kuathirika na ugongwa unaoitwa CCM.Wenye Masters wanaambiwa hawajui kusoma kwenye uchaguzi ila wanaotumia minduku ndio wanajua kusoma ila CCM ni janga kamili kabisa kwa Taifa.
Huna haja ya kutukana.....ongea kwa hoja
 
Kutoka katika misaafu rasmi ya CCM, ni sera ipi uliyoiona inahatarisha maslahi ya nchi? Umezungumzia katiba mpya kukwama, Je, wabunge wa CHADEMA kususa kuendelea na majadiliano, hakukuwa na mchango kukwamisha mchakato? Si vyema kukipachika chama sifa ambayo huwezi kuithibitisha.
Jibu swali, mchakato wa katiba mpya si ulifikia stage ya kura ya maoni je ulikwama wapi?
 
Kwahiyo WEWE ulienda kusomea UJINGA mpaka level ya PHD?? Sio kwa matapishi haya ambayo walitakiwa wapost akina LUKAS 🤔🤔🤣🤣 kweli Kuna safari ndefu ya watu waanaojiita wasomi!! Yaani mtoa Uzi ana very POOR REASONING 😅😅😅🤣🤣🤔🤔
Kwanza, safari yangu ya shule ilikuwa ni kusoma kutibu maradhi ya binadamu, sio kusoma No reform, No election. Pili itikadi za kisisas siyo kipimo ya akili za watu, kama ukomo wako wa kufikiri umeishia kuwa No reform no election ndio IQ test. Basi unatatizo kubwa la akili linalohitaji ukatibiwe. Mwisho; lugha zisizo na staha zinakudhalilisha, watu waungwana hujibu hoja kwa hoja, kutukana ni kielelezo cha uduni wa fikra.
 
1. Ni wito wa mabadiliko ya mfumo mzima wa chaguzi zetu zote zinazotupatia viongozi wa kusimamia rasrimali asili zetu kwa maendeleo yetu wananchi na sio "mabadiliko ya uchaguzi" tu kama unavyowaza wewe...

2. You are asking if it's a campaign against personality, right..?

The answer is big YES. Kinachotoka ndani ya moyo wa mtu ndicho kinacho introduce na ku define personality ya mtu huyo. Ulichokiandika hapa kinatoka moyoni mwako, ndiyo personality yako. Tukipinga hoja zako, maana yake na personality (haiba) yako inakuwa destroyed moja kwa moja..!

So, be very carefully with what comes in your mind through your mouth because it can either destroy your reputation (personality) or maintain it..​

#NoReformsNoElection
Siku utakapojifunza kutofautisha agenda na personality utakuwa umepevuka kwenye siasa. Siasa sio mapenzi, kwamba unachagu wako na kukubaliana kufa na mapungufu yake. Siasa ni jukwaa la kujadili maswala yahusuyo maisha ya watu wetu. Hoja nzuri inachukuliwa nakutelekezwa bila kujali imetolewa na nani? Dr Slaa ali-campaign kutoa elimu bure akiwa anagombea urais, ingawa mwanzo CCM walisema haiwezekani alipokuja JPM alitekeleza. Hiyo ndio siasa yenye tija.
 
Back
Top Bottom