Supervisor
JF-Expert Member
- Oct 29, 2010
- 559
- 208
- Thread starter
- #41
Supervisor; Upo DSM?
Kuna vipimo vya namna 2 au 3 vya HIV. Nadhani Capilary na Determine. The second is more accurate and effective. Kama upo DSM nashauru kwanza uende Hospitali zinazoaminika. Ukipenda tunaweza kuwasiliana kwa hilo nikakusaidia.
Juu ya ushauri unaohitaji, kuna mambo mengi ya kimsingi ya kuzingatia:
1. Ipime nafsi yako na kuwa mwaminifu kwako mwenyewe ni nini unahitaji. You are the boss of your life and in control. Unajua furaha yako na amani yako inahitaji nini.
2. Angalia Mtazamo wako wa Kiroho unakuongoza vipi katika hili.
3. Je akili yako inakuambiaje? Unajitambua? Mke wako ana nafasi gani katika malengo yako na maisha yako kwa ujumla? Jibu unalo wewe.
4. Lakini pia unayo changamoto juu ya afya yako ya mwili. Ni namna gani utaishi na mkeo bila kuathiri furaha yenu na afya zenu.
5. Kuna suala zima la mtoto atakayezaliwa. Unalichukulia vipi? Utapenda mtoto apate mapenzi ya wazazi wote? Je Mke wako anakupenda kweli? Na kama ndivyo ni nini kilisababisha akawa HIV Positive na wewe negative. Je wewe ni mwaminifu katika ndoa yako?
6. Juu ya kiapato na mali: Je mkeo anachangia au amechangia kiasi gani katika mafanikio ya familia. Je unajua kuwa ana haki ya kugawana mali nawe kama mkiachana no matter what? Je ana msaada kiasi gani katika kufanikisha malengo yako ya kupata fedha na mali?
7. Vipi kuhusu maendeleo yako ya kazini na ya kwako wewe binafsi? Anao msaada wowote?
8. Unao ndugu; jamaa na marafiki; wapo wanajamii na wanajuiya unaoishi nao na pia majirani. Ukiweka katika mizani unalionaje hili?
9. Na vipi kuhusu suala zima na burudani na relaxation k. je anayonafasi gani?
10. Mwishoni, ni nini malengo yako makuu katika maisha? Ni nini unkihitaji? Je unajitambua? Unatambua maana halisi ya maisha?
Huitaji kutujibu maswali haya, lakini yatakusaidia wewe katika kufikia maaumzi yako.
Good luck na tunakuombea. Ukihitaji ushauri wangu zaidi au kuniona kwa jambo lolote au kusaidiana kihali na mali, tafadhali ni PM.
U make me cry( ma eyes are full of tears) real umenitoa chozi Superman. Hapana mi siko DSM niko Mkoani lkn kwel tulienda Goverment hospital kupima na cjui nawezaje kuendelea kupata ushauri kutoka kwako. Nauhitaji kwel
Last edited by a moderator: