Mke wangu ni HIV Positive

Mke wangu ni HIV Positive

Jamani jamani jamani....nimedhihirisha unyanyapaa uko kila sehemu...kwanini mumshauri aachane nae., naomba sababu moja..sawa najua ndoa yaweza kuvunjwa., je mnajua anampenda kiasi gani mkewe.? Mnajua huyo mwanamke aliupata ktk mazingira gani..au mnaassume ni umalaya.? Jaribu kujiweka wewe ktk nafasi ya huyo mwanamke..je weww uliyekwenye ndoa..tuseme we ni mwanaume umepata maambukiz haijalishi ni kwa njia ipi..je ni sahihI mkeo akikukimbia.? Hizo ni roho mbaya na mwenyez Mungu hapendi ..mfano tuutoe kwa sajuki thou yy hawakua na magonjwa hayo..je wastara allivyovunjika mguu angekataa kumuoa kisa ulemavu ambao hapo awali hakua nao..Mungu si athuman sajuki huyo huyo kaja kuumwa na huyo mkewe ndo kahangaika nae.. USHAURI wangu umeshafunga ndoa..alounganisha Mungu mwanadam asilitenganishe haijalishi n matatizo gani..huwezi jua mbeleni Mungu atakupa majaribu gani na mkeo huyo huyo unayemuona hafai akakufaa kuliko ndgu yako...mpende mkeo.mpe moyo..mfariji..ukimwi si kufa leo wala kesho..kuna watu wanadunda mjini anatumia septrine tu..kinga ziko juu kiasi kwamba ht kutumia ARV bado..atazaa salama coz kuna dawa za kuzuia maambukizi kwa mtoto atalea watoto wake vizuri iwpo tu hutomnyanyasa na kumnyanyapaa..kuna watu nawafahamu wameishi maisha km yako..cha muhimu ni kufuata ushauri wa wataalamu hutoambukizwa..nakutakia siku njema..mshukuru Mungu kwa kila jambo na hakika utazichota baraka..usihukumu kabla hujahukumiwa hujui ya mbeleni...karibu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Supervisor kama imethibitika huyo mkeo ana Ukimwi, kwanini unadhani ni busara kuendelea na Ndoa?
Mm nakushauri vunja hiyo ndoa, halafu kama ni maswala mengine ya kusaidiana kimaisha yaendelee kama kawaida.

Mkeo akikukimbia utajisikiaje..endapo umepata maambukizi.?
 
Last edited by a moderator:
Kama angekuwa ni mwanaume ndo kaathirika, mke wake hata asingeomba ushauri wowote zaidi ya kuchukua begi lake na kuondoka hata bila kuaga. Wanaume tuna huruma sana jamani.*
Jikaze kaka.
 
Dah pole sana, kama binadamu wa kawaida i understand how u feel! Pia hongera kwa ujasiri uliouonyesha kwa mkeo na watu wote humu jamvini. Ni vema mkarudia tena kupima ili muwe na uhakika zaidi....wanaume wachache sana wenye ujasiri kama wako kaka, i realy admire you
 
Habari zenu wana JF.

Poleni na mihangaiko ya wiki nzima na leo hatimaye mmerejea kulijenga taifa. Jamani nimejitokeza leo kuwaeleza true story ya maisha yangu na kama kuna ushauri basi nitaupokea. Mimi nilioa kwa ndoa takatifu mwez Sept 2012. Ilipofika Nov 2012 Mke wangu alipata ujauzito na kila m2 kati yetu akawa na furaha.

Sasa ilipofikia muda wa kwenda clinic kama ilivyo ada mnatakiwa kuwa wote ili kuweza kupata nasaha na hatimaye kupima maambukizo ya HIV. Baada ya yote tukapima na yeye Mke wangu akakutwa anaishi na virus va UKIMWI na mimi niko salama kabisa. Kwel alilia sana na Nurse akapata shida sana ya kumbembeleza hatimaye akatulia na tukatoka akwa na uso wa tabasamu bandia.

Tulipofika nyumban kilio kilianza upya na mimi nikionekana usoni sina hata lepe la hofu wakati moyoni nilikuwa naumia sana. Baadae ucku akaniomba kuwa kwa sababu Kanisani tulifundishwa kuwa ndoa yaweza vunjwa kama mmoja wapo akionekana ni malaya. Ki ukwel mimi nilimkatalia nikamwambia Mi ni wake mpaka kifo kitakapo tutenganisha, wala hakuamini macho yake.

Kwa sasa anaonekana yuko at least normal ki akili na leo ameenda kazini. Yeye binafsi ni muumini mzuri na anapenda kwel kuimba na kumsifu Mungu. Naomba ushauri wenu tafadhali.

Pole sana supervisor kwa yaliyokupata lakini pia nikupongeza kwa kuonyesha moyo wa ushujaa wa kuonekana hujashitushwa na hilo au kuanza kumlaumu mkeo,kwani hiyo haimaanishi si mwaminifu kwenye ndoa inawezekana alisha pata virus kabla ya kuoana au aliupata kwa njia nyingine kwani hata kuongezwa damu,kuchangia vitu venye ncha kali mtu anaweza pata nk.

Ni vema ukaendelea kumpenda mkeo na kuendelea kuishi naye japo anasema mliambiwa mnaweza kuachana mmoja wenu akiwa malaya lakini nijuavyo kama ni wakristo mtu anaweza mwacha mke kwa sababu ya uzinzi lakini akae bila kuoa au kuolewa hata mwenzake atakapofariki.Kumbuka viapo vyenu ulisema utampenda mkeo katika shida au raha.

Supervisor shida siyo wewe tu imekupata kuna wengine wake/waume zao walipata ajali wakapooza mgongo pamoja na miguu,wengine wamebaki na mguu moja,wengine wenzi wao wamekuwa vipofu baada ya kumwagikiwa machemical machoni wakiwa sehemu za kazi,wengine wana magonjwa yasiyopona na wanaishi nao,vumulia ndugu Mungu azidi kuwape neema.

Endelea kumfariji mkeo asiwe na mawazo solong wewe unampenda asihofu,vyakula venye kujenga mwili ni muhimu.
Lakini pia unaweza kumuomba uwe unatumia kinga wakati wa tendo la ndoa ili asije kukuambukiza na wewe,hata kama ikitokea akatangulia mbele za haki wewe uwatunze wanao Mungu akiwajalia.

Kwa hospital najua mama atapewa vidonge vya kumkinga mtoto kabla ya kujifungua na mtoto atapewa baada ya kuzaliwa,la muhimu baada ya kuzaliwa mtoto asimnyonyeshe akifika miezi 4 atumie njia zingine,na hii ni kutokana na ukweli kwamba wapo watoto wengi tu huzaliwa wakiwa hawana HIV hata kama mama zao wanao,wakati ikifika zaidi ya miezi 4 fizi zake huwa ngumu kuelekea kuota meno kwenye miezi ya mbele kidogo anaweza akawa anachubua ziwa la mama wakati wa kunyonya na kumeza damu yenye HIV toka kwa mama.

Kadri anavyo chukulia hali hiyo kuwa ya kawaida anaweza kuishi miaka mingi kuliko akiwa na mawazo maana CD4 zaweza shuka haraka sana ni vema kuwaona mara kwa mara wataalam wa afya watawapa ushauri.
 
Habari zenu wana JF.

Poleni na mihangaiko ya wiki nzima na leo hatimaye mmerejea kulijenga taifa. Jamani nimejitokeza leo kuwaeleza true story ya maisha yangu na kama kuna ushauri basi nitaupokea. Mimi nilioa kwa ndoa takatifu mwez Sept 2012. Ilipofika Nov 2012 Mke wangu alipata ujauzito na kila m2 kati yetu akawa na furaha.

Sasa ilipofikia muda wa kwenda clinic kama ilivyo ada mnatakiwa kuwa wote ili kuweza kupata nasaha na hatimaye kupima maambukizo ya HIV. Baada ya yote tukapima na yeye Mke wangu akakutwa anaishi na virus va UKIMWI na mimi niko salama kabisa. Kwel alilia sana na Nurse akapata shida sana ya kumbembeleza hatimaye akatulia na tukatoka akwa na uso wa tabasamu bandia.

Tulipofika nyumban kilio kilianza upya na mimi nikionekana usoni sina hata lepe la hofu wakati moyoni nilikuwa naumia sana. Baadae ucku akaniomba kuwa kwa sababu Kanisani tulifundishwa kuwa ndoa yaweza vunjwa kama mmoja wapo akionekana ni malaya. Ki ukwel mimi nilimkatalia nikamwambia Mi ni wake mpaka kifo kitakapo tutenganisha, wala hakuamini macho yake.

Kwa sasa anaonekana yuko at least normal ki akili na leo ameenda kazini. Yeye binafsi ni muumini mzuri na anapenda kwel kuimba na kumsifu Mungu. Naomba ushauri wenu tafadhali.

Pole sana. Rudieni kupima mara tatu yaani kila baada ya miezi mitatu. Ningeshauri muende sehemu tofauti. Ikibainika ni kweli yeye ana ukimwi na wewe huna fanya hivi:-
1. Usijidanganye kwa kuonyesha huruma yako kwa nje wakati kwa ndani unaumia; sikiliza moyo wako unasemaje.
2. Usimlaumu wala kuhoji ukimwi ameupata wapi, hii haitakusaidia
3. Usiwashirikishe watu wengine, hili suala la kuamua wewe na yeye.
4. Kubalianeni kuachana bila vurugu, msaidie kujua atakaa wapi na kuishi vipi.
5. Usiache kumfariji na kumpa moyo wa kuendelea kuishi kwa matumaini akimtegemea Mungu wake.
6. Mshuruku Mungu wako kwa kukulinda na hili; usijione wewe ni zaidi ya wengine; wasaidie wenye mahitaji na wagonjwa wa ukimwi. Tafuta mke mwingine, uwe mwangalifu na mwaminifu.
 
katika mambo yanayohitaji busara ya kiroho na kiimani sana kuyashauri sana mojawapo ni hil
Mi nikusaidie tu kuwaombea!
 
Jamani jamani jamani....nimedhihirisha unyanyapaa uko kila sehemu...kwanini mumshauri aachane nae., naomba sababu moja..sawa najua ndoa yaweza kuvunjwa., je mnajua anampenda kiasi gani mkewe.? Mnajua huyo mwanamke aliupata ktk mazingira gani..au mnaassume ni umalaya.? Jaribu kujiweka wewe ktk nafasi ya huyo mwanamke..je weww uliyekwenye ndoa..tuseme we ni mwanaume umepata maambukiz haijalishi ni kwa njia ipi..je ni sahihI mkeo akikukimbia.? Hizo ni roho mbaya na mwenyez Mungu hapendi ..mfano tuutoe kwa sajuki thou yy hawakua na magonjwa hayo..je wastara allivyovunjika mguu angekataa kumuoa kisa ulemavu ambao hapo awali hakua nao..Mungu si athuman sajuki huyo huyo kaja kuumwa na huyo mkewe ndo kahangaika nae.. USHAURI wangu umeshafunga ndoa..alounganisha Mungu mwanadam asilitenganishe haijalishi n matatizo gani..huwezi jua mbeleni Mungu atakupa majaribu gani na mkeo huyo huyo unayemuona hafai akakufaa kuliko ndgu yako...mpende mkeo.mpe moyo..mfariji..ukimwi si kufa leo wala kesho..kuna watu wanadunda mjini anatumia septrine tu..kinga ziko juu kiasi kwamba ht kutumia ARV bado..atazaa salama coz kuna dawa za kuzuia maambukizi kwa mtoto atalea watoto wake vizuri iwpo tu hutomnyanyasa na kumnyanyapaa..kuna watu nawafahamu wameishi maisha km yako..cha muhimu ni kufuata ushauri wa wataalamu hutoambukizwa..nakutakia siku njema..mshukuru Mungu kwa kila jambo na hakika utazichota baraka..usihukumu kabla hujahukumiwa hujui ya mbeleni...karibu

Umenisisimua na ushauri wako Mungu atakulipa muda wako ulioutumia
 
Last edited by a moderator:
kuna member aliwahi kuja na hii scenario miezei kama miwili hiv imepita,ID yake imenitoka nashauri mods wakuunganishe nae ili akushauri yeye na mumewe walifanya nini kupita hapa kwa amani!
wadau mnaomkumbuka huyu dada nisaidieni,mi nahisi anaweza kuwa in a very good position kumshauri mleta mada!
 
Pole sana rafiki naomba ufuate ushauri wa Lokissa na wengine wenye mapenzi mema na mungu akipenda utavuka salama katika jaribu hili.
 
Mnatakiwa kupima kila baada ya 3 kwa haya majibu mliyopewa halafu ikiwa ni +ve ndiyo
unaamini kuwa mwenzako anao.

Epuka kupima sehemu ambazo si rasmi
yaani unakuta sehemu kipimo 5000/-
Nenda Angaza,Hospitali ya (M), (W) & Vituo
vya Afya ambapo huduma hizi hutolewa bure


Jueni wazi huo si mwisho wa Maisha pia huna
sababu ya kuvunja Ndoa magonjwa ktk
Dunia hii ni mengi na watu wanaishi vizuri tu.
Ukimwacha sio ufumbuzi,kesho utaoa nawe
ukawa na tatizo utaachwa.

Kuna maradhi yanayotisha kama Ini,Kisukari,Presha,Anemia(Sickle Cell) n.k lakini watu wana
ishi vizuri sana.
Msijihukumu maana nafasi nzuri mnayo kujua
kama kweli ni +ve.
 
Kama angekuwa ni mwanaume ndo kaathirika, mke wake hata asingeomba ushauri wowote zaidi ya kuchukua begi lake na kuondoka hata bila kuaga. Wanaume tuna huruma sana jamani.*
Jikaze kaka.

Mmmmh aibu huoni
 
Umenisisimua na ushauri wako Mungu atakulipa muda wako ulioutumia

Thank u..I hve close relatives of mine wanashida km yako..na wanamiaka 15 ya ndoa sasa..wanalea mtoto vzr na amezaliwa bila maambukizi..ukihitaji ushauri sisite.na nna umia sana kuona unyanyapaa humu ndani ilhali hujui kesho yako...
 
Thank u..I hve close relatives of mine wanashida km yako..na wanamiaka 15 ya ndoa sasa..wanalea mtoto vzr na amezaliwa bila maambukizi..ukihitaji ushauri zaidi nipm..am health personel..na nna umia sana kuona unyanyapaa humu ndabi ilhali hujui kesho yako...

I wish kama ningekuwa karib na ww kwa ushauri zaid. U know what? ilitaka hata asitumie dawa ya kinga ili afe yeye na mtoto maana haoni faida ya kuishi na anajuta kuwa amenipotezea malengo lkn nikamwambia malengo yangu yako Mbinguni na sio Duniani nikamwambia kufa sio option either unaumwa au mzima
 
Nlisha wahi kuwa na girlfriend zaidi ya mwaka mmoja alikuwa akiishi na mambukiz ya virusi vya ukimwi lakn bado mi sikuambukizwa.
Pata ushauri wa watalamu wa mambo ya afya utaweza kuishi na mkeo bila kukuambukiza na watoto mkitaka mtazaa tena na tena na hawata kuwa na maambukizi. Tafadhal mpende mkeo.
 
Supervisor; Upo DSM?

Kuna vipimo vya namna 2 au 3 vya HIV. Nadhani Capilary na Determine. The second is more accurate and effective. Kama upo DSM nashauru kwanza uende Hospitali zinazoaminika. Ukipenda tunaweza kuwasiliana kwa hilo nikakusaidia.

Juu ya ushauri unaohitaji, kuna mambo mengi ya kimsingi ya kuzingatia:

1. Ipime nafsi yako na kuwa mwaminifu kwako mwenyewe ni nini unahitaji. You are the boss of your life and in control. Unajua furaha yako na amani yako inahitaji nini.

2. Angalia Mtazamo wako wa Kiroho unakuongoza vipi katika hili.

3. Je akili yako inakuambiaje? Unajitambua? Mke wako ana nafasi gani katika malengo yako na maisha yako kwa ujumla? Jibu unalo wewe.

4. Lakini pia unayo changamoto juu ya afya yako ya mwili. Ni namna gani utaishi na mkeo bila kuathiri furaha yenu na afya zenu.

5. Kuna suala zima la mtoto atakayezaliwa. Unalichukulia vipi? Utapenda mtoto apate mapenzi ya wazazi wote? Je Mke wako anakupenda kweli? Na kama ndivyo ni nini kilisababisha akawa HIV Positive na wewe negative. Je wewe ni mwaminifu katika ndoa yako?

6. Juu ya kiapato na mali: Je mkeo anachangia au amechangia kiasi gani katika mafanikio ya familia. Je unajua kuwa ana haki ya kugawana mali nawe kama mkiachana no matter what? Je ana msaada kiasi gani katika kufanikisha malengo yako ya kupata fedha na mali?

7. Vipi kuhusu maendeleo yako ya kazini na ya kwako wewe binafsi? Anao msaada wowote?

8. Unao ndugu; jamaa na marafiki; wapo wanajamii na wanajuiya unaoishi nao na pia majirani. Ukiweka katika mizani unalionaje hili?

9. Na vipi kuhusu suala zima na burudani na relaxation k. je anayonafasi gani?

10. Mwishoni, ni nini malengo yako makuu katika maisha? Ni nini unkihitaji? Je unajitambua? Unatambua maana halisi ya maisha?

Huitaji kutujibu maswali haya, lakini yatakusaidia wewe katika kufikia maaumzi yako.

Good luck na tunakuombea. Ukihitaji ushauri wangu zaidi au kuniona kwa jambo lolote au kusaidiana kihali na mali, tafadhali ni PM.
 
Last edited by a moderator:
mkuu nakushauri urudie kupima katika hospitali nyingine kwani mara nyingine huwa wanakosea timing ya kusoma majibu,
ikiwa mkeo bado ana maambukizi si jambo geni wapo wengi wenye hali kama yenu(discoduct),mpende mkeo,ishini kwa kufuata ushauri wa daktari na wataalam wa afya,mnaweza kuwa na watoto zaidi ya mmoja ambao ni HIV negative mkifuata ushauri wa daktari,jipe moyo mkuu kwani majaribu hayana budi kuja.
MUHIMU:USIMTANGAZE MKEO KWA WATU,IWE SIRI YENU NA WATAALAM TUU.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom