Kwakuwa umeongelea kama igizo, basi inakupasa ujue huyo mzee anampa nini cha ziada ambacho wew umeshindwa kumtimizia ili uangalie unaweza kutatua kwa njia zipi pasipo kujiingiza kuzalisha tatizo kubwa zaidi.
Fatilia historia ya maisha ya mzee sasa hivi wanatumia Sana nguvu ya tamaduni ili kumiliki wanawake wanao wa hitaji.
Kumbuka kwamba hakuna utani kutania kwa kauli ya mwanamke kwamba tuachane, tusifatiliane, nipo tayari kuvunja ndoa! Hilo ni kosa kubwa Sana kwenye mahusiano, ipo hivi mwanaume ukiyapokea matamshi hayo ukatoa msamaha ujue upo kwenye hatari na kiwango kikubwa cha kufa mapema(elewa vizuri hapo) kumbuka kwamba kwa akili hiyo ya mwanamke yupo tayari kukuua ili awe huru na huyo mzee kwakuwa wewe tayr umesha kuwa kikwazo kwenye penzi lake jipya!
Unajua mwanamke Kuna kitu kimsahaulisha kwamba huyo mzee hawezi kumuoa zaidi anatumika kingono,, swala la mahusiano ni gumu hasa inapofika hatua yatuoa maamuzi na ukichukulia ni mke wa ndoa, na tayari mnafamilia kama kiunganisho yaan kwenye Hilo unahitaji uwe na busara Sana hasa kupima faida zakuachana, hasara za kuachana, na ujipime endapo unaweza kuhimili changamoto zake ukiridhia kubaki nae,,
Kwasasa inakupasa kushirikisha wazeee wakubwa kwa umri wa huyo mzee, kisha wasilisha swala lako kwa viongozi wa Familia yako, linapozidi ongea na washenga pia viongozi wa dini hrf Pima msimamo wa mwanamke jibu utakalopata nadhani litakuwa ni jibu la busara na hekima za wazeee.
Hutakiwi kumpiga mwanamke kwa jambo ambalo amesha litolea maamuzi, ukumbuke kwamba mwanamke huwa hapendi ila anahitaji na ndiomana 90% wanalalamika hawaridhishwi kwenye mahusiano Yao, akipata hitaji lake na ameridhika nje ujue huwez kubadili maamuzi yake, na haitakiw kulazimisha mapenzi, geuka kidogo nyuma angalia kwenye mti wenye kimvuli chukua kiti kaa chini Kunywa maji maamuzi sahihi unayo wewe mwenyewe, unafikiria unaweza kutatua vipi swala lako? Hushauliwi kuacha mke ila tafuta njia salama kutetea Amani ya moyo wako na watoto wako ili wasiishi kwa kukosa malezi yako!
Yupo Mr frani alipitia changamoto kama hiyo, yeye aliacha nyumba akaondoka na nguo alizovaa tuu lkn kila siku anahakikisha Familia yake ipo salama! Sijui alitumia mbinu gani, umiza kichwa ka mkubwa