Dume rijali la JF naja kwenu dah mwenzenuu, ndoa yangu miaka 7 mke wangu kamganda Mume wa mtu!
Mwaka jana niligundua kuwa mke wangu kuna mwanaume anamahusiano naye, ni baba mtu mzima na wanafanya kazi sehemu moja. Niliiongea na mke wangu tukagombana sana lakini mwisho aliniomba samahani na kuniambia kuwa hawezi kurudia tena. Mimi nilimsamehe na kila kitu kilikuwa vizuri.
Mwaka huu mwezi 3 nilikuja kugundua kuwa bado hawajaachana kwani nilikuta meseji mke wangu akimtumia huyo mwanaume picha za uchi, niliumia sana kwani anatumia simu yake na hiyo simu watoto wetu wanaichezea, nilipomuuliza alibadilisha password na kuniambia nisimfuatilie yeye si mtoto. Alinijibu vibaya sana hata nilipoongea na Mama yake kumuambia mambo ya binti yake haikusaidia chochote, hivyo niliamua kumtafuta yule mwanaume.
Nilimtafuta kistaarabu kama mwanaume mwenzangu kumuambia kuhusu mimi kujua mahusiano yao na kumuomba aachane na familia yangu kwani tuna watoto watatu na ndoa yetu ina miaka 7sasa, alionyesha kunielewa na kuniambia atakata mawasiliano na mke wangu.
Kweli ni kama waliachana kwani mke wangu alirudi akaninunia kuwa nisimfuatilie, mimi nilijua kama yameisha lakini juzi nimetumiwa meseji na mke wa huyo mwanaume akinambia kuwa mke wangu anamsumbua sana mume wake.
Akanitumia screenshot mke wangu analalamika kuwa hawezi kumuacha ni bora kuvunja ndoa yake lakini si kumuacha yeye, kwa kweli jana nimempa kipigo cha mbwa msikitinii.. Yoweee usiku wote