Mke wangu kachachamaa anataka tuachane!


Mkuu kwa dunia ya leo bado una haya mawazo jaman!
 
eti umekuja kuomba ushauri.hebu nihamie kwingine.
Kila la kheri kaka.Tekeleza mila kaka.Bahati nzuri umeoa mke ambaye haujui haki zake.
Wewe ni mkataa kwenu.
Umazitupa mila na desturi zenu na ndio maana unatokwa na povu kwa mila za wengine ambazo hazikuhusu
 
marehemu kaka yako alipima???????swali lingine...hivi huko kwenu tarehe mnazotumia zimeshafika ANGALAU 1900?swali la mwisho tafadhali......unaishi misitu ya kongo au tanzania hii hii?

Hahahaha well said mkuu
 

Kama hataki kukubaliana na mila zenu, achana naye. Wewe endelea na huyo mke wa marehemu ili udumishe mila. Utapata mke mwingine. haina shida.
 
Ni nani kakwambia kwamba kaka yangu kafa kwa ukimwi?
Nishasema kafa kwa ajali mwezi uliopita

kwani aliyekufa kwa ajali hawezi kuwa alikuwa nao kabla we una hakika gani na afya yake? Mila nyingine inabidi zifutwe tu hali ya sasa au we mwenzetu unaishi nchi gani, mana nashangaa eti mpaka leo hii bado hizo mila na desturi........tafakari na chukua hatua!!!!!! Achana na mambo ya kizamani
 
 
Basi isiwe nongwa tutapima huo ukimwi ili yaishe
 
 
 
Ni nani kakwambia kwamba kaka yangu kafa kwa ukimwi?
Nishasema kafa kwa ajali mwezi uliopita

Kwa hiyo umetamani mabaki ya hilo gari na mali nyingine ndio maana unajifanya umeshikilia mila!! loooo hebu uwe na haya kidume wewe! Unaonekana wazi huna upendo zaidi ya kutamani vya kaka yako, nyie ndio mnaowatamanigi shemeji zenu!

Acha bana, endelea kumtunza mke wa marehemu na watoto wake na umuheshimu kama shemeji; USIMRITHI na kumfanya mkeo.
 

Watu watakuja na yao, cha msingi ni kuzingatia mila na nafsi maana kwa mfano kama wewe ni Muislam sijaona shida kuoa mke wa kaka, kama mkristo mke ni mmoja tu. Namkubali Zuma kwa africa nzima maana yeye ndio pekee amekataa kuwa mzungu kwa kudumisha mila mke kadhaa.
 
siku hizi nimeokoka na kuacha matusi otherwise ungenikoma
 

Buluu hapo mh! mwe! wonders shall never cease
 
Cheeeee!!!Yaani izo mila potofu bado ipo!! Ebu acha ujinga wewe. Mpeni huyo mwanamke uhuru wa kuamua aolewe na nani na ivi hujui kuwa ni matusi kumuoa mke wa kakao?Na vipi kuhusu magonjwa!!! Lol!!Ebu badilikeni bwana
 
 
Kuna kijana namfahamu yeye alimlea Mke wa marehemu rafiki yake ambae alikuwa mjamzito, alijifungua na jamaa akalea mtoto na mama yake na akamsomesha mtoto hadi leo hii jamaa ana mke wake na huyo mke wa mareheu rafiki yake alishaolewa kitambo na amini usiamini jamaa hakuwahi tembea na huyo dada hata siku mojs!Kumbuka alikuwa mke wa rafiki tu, sasa wewe kaka yako!!!!!!!!!!!!Ebu acha uhuni bwana
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…