Mke wangu hana hobby ya kitu chochote

Mke wangu hana hobby ya kitu chochote

God bell

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2011
Posts
590
Reaction score
211
Kwanza niwatakie lunch njema. Kabla hatujaoana aliniorodheshea hobbies zake kama kusafiri, kuangalia tamthilia, movies, usafi wa ndani na mazingira ya nje, outing. Tumeingia kwenye ndoa mwaka wa 5 sasa hayuko interested na kitu chochote. Jumatatu hadi ijumaa yuko busy kazini. Jumamosi anaenda sokoni kufanya shopping. Jumapili kwenye ibada.

Nikimuliza ni wimbo gani anaupenda uwe wa dini au kidunia hajui manake hapendi kuangalia hata TV, hata taarifa ya habari huwa namlazimisha.

Hajui kujiremba anavaa kawaida sana. Nikimwambia outing anasema bora hiyo hela tununue chakula tupike hapa nyumba. Hata usafi wa nyumba sio wa kiviile saana.

Yeye akiona watoto wameoga wameshiba ndo starehe yake basi, hata kuwatembelea marafiki huwa namlazimisha.

Nimejaribu kumuliza hana jibu anaona kama namuonea na siyo kwamba anachoka sana iwe ndo sababu kwani msichana wa kazi tunae. Na sio kwamba tuna umri mdogo hapana, tulioana tukiwa na umri wa kuitwa mama na baba.

NISHAURINI NIMESHINDWA KUMWELEWA HUYU MKE WANGU
 
IF ITS NOT BROKEN DON'T FIX IT..

bado sioni tatizo lake
sanasana wewe umeanza gubu

unataka awe na hobby ya kwenda taarabu na mashangingi ya mjini
wamtafutie vibuzi?

au awe na hobby ya kwenda bar na kunywa hadi anasinzia?

get over it....
 
Kwanza niwatakie lunch njema. Kabla hatujaoana aliniorodheshea hobbies zake kama kusafiri, kuangalia tamthilia, movies, usafi wa ndani na mazingira ya nje, outing. Tumeingia kwenye ndoa mwaka wa 5 sasa hayuko interested na kitu chochote. Jumatatu hadi ijumaa yuko busy kazini. Jumamosi anaenda sokoni kufanya shopping. Jumapili kwenye ibada. Nikimuliza ni wimbo gani anaupenda uwe wa dini au kidunia hajui manake hapendi kuangalia hata tv, hata taarifa ya habari huwa namlazimisha. Hajui kujiremba anavaa kawaida sana. Nikimwambia outing anasema bora hiyo hela tununue chakula tupike hapa nyumba. Hata usafi wa nyumba sio wa kiviile saana. Yeye akiona watoto wameoga wameshiba ndo starehe yake basi, hata kuwatembelea marafiki huwa namlazimisha. Nimejaribu kumuliza hana jibu...anaona kama namuonea na siyo kwamba anachoka sana iwe ndo sababu kwani msichana wa kazi tunae. Na sio kwamba tuna umri mdogo hapana, tulioana tukiwa na umri wa kuitwa mama na baba. NISHAURINI NIMESHINDWA KUMWELEWA HUYU MKE WANGU

Ama kweli kwenye miti hakuna wajenzi!!!!!!!!!!!!

Ningekutana na mwanamke huyu ningejihesabu mwenye bahati kubwa!!!!!
 
Kwanza naomba nikuulize swali,anafanya kazi gani?ama ana proffession gani?hapa itatusaidia kukupa jibu zuri
 
^^
Samahani nauliza tu,,Anakuzidi umri?
^^

Kweli mkuu hili ni swali la msingi sana

Kila siku huwa ninawaambia wale wanaotaka kuoa,jaribu kutafuta mwanamke ambae mnaendana umri,yale ya kuoa mwanamke amekuzidi miaka 10 au wewe umemzidi huo umri lazima itakuwa kilio kwako
Kitendo cha kukaribiana umri kitawafanya mitazamo yenu kuwa angalau sawa,sio mmoja anawaza kuvaa pedo na kwenda disco wewe unawaza kujenga nyumba

Hiki ndio kinamkuta huyu bwana mdogo!
 
....
Labda anahasira debe mia...usikute hafurahii tendo la ndoa..
 
Mi ningekuwa na mke kama huyo ningefurahi sana.

Mke asiye na usumbufu wa vi"obby" safi sana. Ogopa kuwa na mke mwenye "obby" ya kulala misibani, kugegedwa mchana, kuiba vijiko bar, au mpenzi wa ngumi na kareti.
 
Shauri yako ukianza kumpushi atapushika hadi utakuja kuomba ushauri wa kuwa mkeo kacharuka.

Uwe unamwambia mapema, watu wengine shughuli za kazi zinachosha sana na wakipata dakika wanaona raha kupumzika nyumbani, ndio maana kuna take-away.

I hope wewe ni mtu unaepanga mapema labda hapo utamnyanyua kidogo, na kutembelea marafiki je nao wanawatembelea? Unajua mawasiliano ya simu siku hizi yamebadilisha maisha ya watu wengi sababu zamani ilikuwa mtu mkutane ndio muongee vizuri.

Pia ujiangalie usije ukaingia katika wimbi la kuwa na namba 2 huko nje eti ule starehe usizopata kwa mkeo.

Hobby zitajionyesha tu kama anazo, au muulize ana interest ya nini na nino katika maongezi yenu then shughulikia. Kumbuka nje kuna magonjwa.
 
Kwanza niwatakie lunch njema. Kabla hatujaoana aliniorodheshea hobbies zake kama kusafiri, kuangalia tamthilia, movies, usafi wa ndani na mazingira ya nje, outing. Tumeingia kwenye ndoa mwaka wa 5 sasa hayuko interested na kitu chochote. Jumatatu hadi ijumaa yuko busy kazini. Jumamosi anaenda sokoni kufanya shopping. Jumapili kwenye ibada. Nikimuliza ni wimbo gani anaupenda uwe wa dini au kidunia hajui manake hapendi kuangalia hata tv, hata taarifa ya habari huwa namlazimisha. Hajui kujiremba anavaa kawaida sana. Nikimwambia outing anasema bora hiyo hela tununue chakula tupike hapa nyumba. Hata usafi wa nyumba sio wa kiviile saana. Yeye akiona watoto wameoga wameshiba ndo starehe yake basi, hata kuwatembelea marafiki huwa namlazimisha. Nimejaribu kumuliza hana jibu...anaona kama namuonea na siyo kwamba anachoka sana iwe ndo sababu kwani msichana wa kazi tunae. Na sio kwamba tuna umri mdogo hapana, tulioana tukiwa na umri wa kuitwa mama na baba. NISHAURINI NIMESHINDWA KUMWELEWA HUYU MKE WANGU
huyo ndo anafaa sasa kama hujui.
 
Kwanza niwatakie lunch njema. Kabla hatujaoana aliniorodheshea hobbies zake kama kusafiri, kuangalia tamthilia, movies, usafi wa ndani na mazingira ya nje, outing. Tumeingia kwenye ndoa mwaka wa 5 sasa hayuko interested na kitu chochote. Jumatatu hadi ijumaa yuko busy kazini. Jumamosi anaenda sokoni kufanya shopping. Jumapili kwenye ibada. Nikimuliza ni wimbo gani anaupenda uwe wa dini au kidunia hajui manake hapendi kuangalia hata tv, hata taarifa ya habari huwa namlazimisha. Hajui kujiremba anavaa kawaida sana. Nikimwambia outing anasema bora hiyo hela tununue chakula tupike hapa nyumba. Hata usafi wa nyumba sio wa kiviile saana. Yeye akiona watoto wameoga wameshiba ndo starehe yake basi, hata kuwatembelea marafiki huwa namlazimisha. Nimejaribu kumuliza hana jibu...anaona kama namuonea na siyo kwamba anachoka sana iwe ndo sababu kwani msichana wa kazi tunae. Na sio kwamba tuna umri mdogo hapana, tulioana tukiwa na umri wa kuitwa mama na baba. NISHAURINI NIMESHINDWA KUMWELEWA HUYU MKE WANGU

Anaonekana ni Anti social tu na hakuna jengine, kaa nae chini muongee.
 
Mkataa jema Baya linamwita! Huo wema waje na utulivu wake unataka kuubadili!?😕😱
 
Mmmh... Yan wewe ungepata.mwanamke wa hivi for sure ungeimba haleluyah....

Kila weekend shopping ya nguo na viatu!
Kila mwezi safari ya mbali (mkoani na hata nje ya nchi)
Vitchen party haviishi, mashoga lukuki na muhudhuriaji wa kila sherehe hata zisizomhusu....
Mavazi kama ya "Mayasa"
Akitoka job anashinda kwenye TV (tamthilia na bongo movie)

Wallah Mwenye bahati habahatiki....

"If you can't win her join her"
 
Kuna watu wapo hivyo sio wa kujichanganya na watu yeye busy na mambo yake. Na akili yake inawaza watoto wake na ni mchumi hataki kupoteza pesa kwa outing
 
na ungekuwa na mke mwenye "obby" ungetujazia "seva" humu, maana inaonekana una gubu kweli.😡😡
 
Back
Top Bottom