House of Commons
JF-Expert Member
- Oct 1, 2013
- 2,189
- 2,206
MOYO WANGU UNAUNGUA, SINA RAHA TENA!
Nimeoa mwanamke ambaye nimeishi naye miaka mitano hadi sasa. Wakati tunaingia katika mahusiano nilimkuta tayari ana mtoto ambaye alizalishwa na mwanaume mwingine na akamkimbia.
Kwa kuwa nilimpenda sana naye akanipenda sikuona mtoto kama kikwazo katika mahusiano yetu. Niliendelea kumpenda yeye pamoja na mtoto wake na kuwatunza wote vizuri.
Maisha yetu yalikuwa ya furaha sana, lakini miaka miwili iliyopita niligundua kumbe bado anawasiliana na mwanaume ambaye alimzalisha akamkimbia.
Nilimkanya, akaniambia hakuna chochote zaidi ya kutaka kujua hali ya mwanaye. Siku moja wakati nachungulia simu yake niliona kuna ujumbe kutoka kwa huyo mzazi mwenzie ambaye anamsifia kuwa sasa hivi amekuwa mtamu na anajua kukatika mauno.
Moyo ulinienda kasi sana, kwa ujasiri niliamua kumuuliza ambapo alikubali kuwa ni kweli amefanya naye mapenzi ila nimsamehe hatarudia tena.
Kuanzia hapo, nimekuwa sina raha katika ndoa yangu, moyo wangu unaungua kwa sababu mara kadhaa naendelea kuona wakiwasiliana.
Naomba ushauri wako, nifanyeje? Nitasoma comment zote kwani nahitaji kuokoa moyo wangu
Au nikanyage tu maisha yaendelee?
Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana, I feel it. Ni kweli lazima uumie.
1.Kwa Maslahi ya watoto wenu, endelea kukaa nae ila control stress zako ingawa sio rahisi maana si rahisi kufuta unalolifahamu kuhusu mkeo na x wake
2. Acha kufuatilia nyendo za mkeo (puuza na endelea na shughuli zako)
3. Make any possible means kumfanya x wa mkeo afahamu kuwa wewe unalifahmu hilo kwamba wapo bado wanaendelea na mahusiano, that will call his senses to stp
4. Acha kuendelea kulalamika kwa mkeo kuhusu mahusiano yao. Mara inapotokea mkafanya mgogoro huo, ongea kama mwanaume, usiongee kama hawala, wewe ndio mme. Speak with authority, black and white
5. Take measures, kama huyo mtoto walio zaa unae, force your wife to send the child to his/her father as soon as possible
6. Think of seperation, kwa sababu hili linaweza kukuingiza kwenye shida zinazotokana hasira na kufanya matukio mabaya yanayoweza kukuweka jela.
Ni ushauri tu, chagua unachhona kinakufaa
