Mke wangu ananipiga makofi kila ninapochelewa kurudi nyumbani, nifanyaje jamani nimechoka!

Sasa usrudi lala hukohuko akikuuliza kulikoni mwambia ulichelewa ukaogopa kuchezewa vitasa.
 
Wadau huyu ni Beira baby boy anatuzuga na id mpya, kama sio yeye ni Sexless, nishajua thread/nyuzi zao hazinaga mashiko.Hawa watu wa hovyo sana kila siku nyuzi za kutunga za hovyo na kufanya JF kupoteza mvuto. Unashindwa kuelewa nani yupo serious na anahitaji msaada na kumaanisha alichoandika.
 
Hapa ndipo ninapo pata mashaka kuhusu uanamume wako, maana ninahisi tunazidi kupungua kwa kasi ya Standard Gauge......

Kwani, wewe ndie ulie oa ama umeolewa...?

Kwani, unaishi na mke ama bondia...?
Naishi na mke, kama sio kama siwezi kumdunda ila nahofia kuishia segerea na watoto wangu kupata shida.
 
Mimi ni mwanaume niliejaaliwa kuwa na watoto wawili wakike na wa kiume na mke wangu nimemuoa miaka kumi iliyopita huko mkoani iringa, shughuli zangu ni fundi seremala katika hizi kampuni za ujenzi za kichina zilizotapakaa hapa jijini dar ambazo tunajenga nyumba mbalimbali za miradi ya jamii.

Sasa mara nyingi pesa huwa tunalipwa kwa kila wiki, sasa hapa kati huwa napigika sana yaani nakuwa sina pesa hivyo ni lazima nijiongeze kwa kufanya kazi za ziada pindi ninapotoka kazini ile saa kumi, sasa najikuta nakuwa huko mitaani mpaka saa mbili au saa tatu usiku ndipo namaliza kazi zangu za ziada na kupata pesa then naelekea home.

Lakini ninapofika nyumbani nakumgongea mke wangu anifungulie mlango nikiingia ndani tu maneno yanaanza, nikimjibu kuwa nilipitia sehemu kufanya kazi maana nimerudi kazini nikiwa sina pesa naambulia vibao usoni napigwa mpaka nalia ndugu zangu huku nikiambiwa na mke wangu...usinijibu mimi nakwambia...roho inaniuma sana ndugu zangu naomba mnishauri nifanye nini ili kuepukana na vipigo hivi mimi jamani?.
Piga ua huyo si mwanamke bali ni mme mwezako. Nawe mwoneshe ubabe wako.
 
Fake story 'cause mademu was kununu (iringa) hawana swagga hizo.......
 
Labda na wewe umesha-copy mambo ya wanaume wa Dar es salaam mkuu!!!!

Chips yai zimeshamaliza nguvu za mwili wako?

Anyway
1. Kuna mambo mengine hayawezi kwenda usipotumia busara. Kama unavyokubali kichapo.
Hongera kwa busara zilizopitiliza.

2. Kuna mambo ukiyaendekeza na kuyafumbia macho, yatakuumiza.
Mf. Kuchapwa makofi, tena mbele ya watoto.

3. Ukiendelea kukubaliana na hali hiyo utapangiwa hata siku za kupata unyumba.
Wanawake hawakurupuki wanapotaka kuanza tabia flani, huo mwanzo wake na alipofikia usipojinasua, umekwisha.

Amini usiamini ipo siku mambo mengine yatafuata tu.

Ushauri wangu.
Siku akithubutu kukupiga tena, toa kipigo heavy kwake ili ajue ulikuwa unamuacha tu,(ila uangalie sehemu za kupiga usije ukamdhuru mkeo)
Amini yote yataisha.
 
Back
Top Bottom