“baba D nina mimba"
Sikuwaza chochote kibaya nikamuuliza tu sasa kwanini hukunambia muda wote na hiyo mimba ina muda gani? Akanijibu kuwa inakaribia mwezi sio yako.
Alooo! Nyie watu kumbe kuna mambo yanauma hivi nilihisi kama nimetobolewa moyo na kitu cha baridi niliishiwa nguvu masikio yalikuwa kama yameziba, namsikia kwa mbali analia sana ananiomba nimsamehe na ana mpango wa kuitoa tu nikamuuliza mmekutana mara ngapi na huyo mtu akanambia mara 3
Nilikata simu kwakweli nikatulia kama nusu saa nafikiria jinsi alivyokuwa akigegedwa mke wangu yani nilikuwa nasikia hadi sauti za mahaba kichwani ndugu zangu haya mambo kumbe ndo yanauma hivi.
Nilipiga sana simu ilikuwa inatumika kama dakika 20 hivi alionesha yupo busy kuna mtu kama wanajadiliana, badae akapiga simu mwenyewe yani simple eti baba D nilikuwa nakutania tu nijue msimamo wako.
Sijawasilina nae mpaka leo hii namuonea huruma sana mwanangu sijui nafanyaje ila nina homa mwili hauna nguvu, yani kwa maelezo yale naona hakuna utani ni tukio lipo na huenda wamejadiliana na huyo malaya mwenzake watoe mimba.
Inauma aise mke wangu kachakatwa, hapo sidhani kama kuna utani
Nishaurini nifanye nini sijamtafuta hadi sasa hivi na leo naenda kunywa pombe kwa mara ya kwanza.
Ukweli mtupu hakuna utunzi.