TIQO
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 13,786
- 2,102
Apana ndugu sio wote na hata wanaume vile vile japo sio wote,lakini kwenye swala la kusahau mtu alikotoka ni hulka ya mtu....
Wanawake ni viumbe dhaifu sana
Apana ndugu sio wote na hata wanaume vile vile japo sio wote,lakini kwenye swala la kusahau mtu alikotoka ni hulka ya mtu....
Dhaifu kwenye kupenda lakini ni wazuri na wenye imani sana kwa wenzi wao,ila uki wabadilikia ndio inakua mbaya..Wanawake ni viumbe dhaifu sana
sio fair bwana,mwanamke ni msaidizi wa mume. si amsaidie mume wake tu jamani.Heh! Sasa ugumu wa maisha umeanza baada ya yeye kuanza kazi? Mwanaume hajitambulishi, anatambulishwa na majukumu.
Mpe salamu zangu, muambie akaze uzi!
sio fair bwana,mwanamke ni msaidizi wa mume. si amsaidie mume wake tu jamani.
haijalishi anasave au anakesha kununulia mikorogo... jamaa kasema hatoi sio fair bwana.maisha ni haya hayaHapana tusikimbilie kuwalaumu wanawake, maelezo yake ni so general kuweza kumtupia lawama mke wake.
Kwanza ameshindwa kuthibitisha fedha ya mke wake inakwenda wapi? Yaani ana save, hajui kabisa inatumiake au mke wake anakesha kununua mawax na magold n.k
Kuna kipindi wanaume tunawajengea chuki kubwa sana wanawake lakini kutokana na kukosa mbadala inabidi wavumilie na ikitokea hali imebadilika basi mambo kama haya huanza kujiibua kama visasi hasa kama familia haina misingi ya kumjua Mungu.
Ngoja jamaa afunguke zaidi tutajua mbivu na mbichi.
haijalishi anasave au anakesha kununulia mikorogo... jamaa kasema hatoi sio fair bwana.maisha ni haya haya
by the way mbona nikikupigia simu hupokei bwana? nitamwaga pm zako hadharani
kha!! wacha mpoteza mwenzio...hapo akimtia mimba sii ndio anajiongezea mjukumu na mdomo wakulisha....wee tulizana kamatia kimada pembeni nawe awe anakuliwaza
mfumo dume upo kabla hata ya Kristo lakini kuna mifumo ambayo ni kandamizi kwa karne hii tuliofikia natambua ni muhimu kusaidiana majukumu ya kifamilia lakini mkewe kakataa hivo hawezi kumlazimisha au kutumia mabavu inahitajika busara tu.
Dhaifu kwenye kupenda lakini ni wazuri na wenye imani sana kwa wenzi wao,ila uki wabadilikia ndio inakua mbaya..
Chaz C hayo ni maelezo ya upande mmoja yapo maswali mengi sana ya kukuuliza na endapo uyapatia majibu basi angalau nitaweza kuchangia.
1.0 Umesema ndoa yenu ina miaka tisa, hongera sana. Je katika miaka tisa ambayo mkeo alikuwa hana kazi uliishi nae vipi?? Uliishi nae kibabe kwa sababu yeye hana kazi au ulimnyanyasa kwa bile yeye ni mama wa nyumbani???
2.0 Unalalamika mke wako hatoi pesa na amekuwa na kiburi. Ulitaka atoe pesa ya matumizi gani mfano??
3.0 Umeshawahi kumshirikisha katika programe ya maendeleo yoyote hapo nyumbani kwa kushirikishiana??? Mfano mke wangu nataka tuanze kufuga kuku lakini mimi nina laki tisa nataka na wewe uongezee laki tano toka kwenye mshahara wako ili tujenge banda na kuanza kufuga?? Hapa nakusudia mipango shirikishi.
4.0 Kiburi chake ni kwenye hela tu au mpaka mambo ya nyumbani yanayumba??
5.0 Kazi anayofanya ina kipato kikubwa kuliko yako?
6.0 Una uhakika kiburi cha mkeo ni kutokana na kazi peke yake au kuna makando kando??
Naomba nikomee hapo lakini kama ukifanikiwa kunijibu nadhani wanaJF wengine wanaweza kutiririka vizuri hasa upande wa ushauri.
sasa wewe, kama kazzi ya akina dada ni kuzaa kwa uchungu, huko makzini wanatafuta nini??!!.sometimes muwe mnapunguza malalamishi hata Biblia inasema mwanamke atazaa kwa uchungu,mwanaume atakula kwa jasho sasa we pambana kiume ihudumie familia siku akiamua kwa matakwa yake kusaidia its ok,hapa ndo tunapowatofautisha wanaume na wavulana vinginevyo unatafuta kuleta mitafaruku ktk ndoa.
Tuna miaka tisa sasa yenye maisha ya kawaida yenye furaha, mimi nikiwa nafanya kazi katika kampuni moja hapa tabora yeye akiwa mama wa nyumbani.
Miezi nane iliyopita alipata kazi, wana jamii naomba msaada toka apate kazi amekuwa na kiburi, anataka hela yangu ndo itumike tu yakwake wala hataki isaidie.nimemuelimisha kuhusu ugumu wa maisha lakini wapi, tatizo lolote likitokea ni mm ndo wa kusolve.. P/se help