Mke wangu anaenda Ughaibuni for good

Mke wangu anaenda Ughaibuni for good


Kwa argument hii hata wale dada zetu wanaosimama mabarabarani usiku pia wanajiingizia kipato halali so si shame job
?

Unajua maana ya rizq 'halali' wewe? Sidhani kama unajua.

Licha ya kutojua kwako, umalaya si haramu sehemu zote duniani. Zipo sehemu ambapo umalaya ni moja ya shughuli rasmi tena yenye kutozwa kodi kabisa.

Na madhali mtu kaamua kujikita huko ili kujipatia mkate wake sioni kwa nini asijivunie kutoa huduma kwa watu wanaoihitaji huduma anayoitoa.
 
Hi wadau,
Sasa inaniwia ugumu kumuachia aende. Hebu put yourself in my shoes ingekuwa wewe ungelifanya nini,ukizingatia invitation imeshafika na process za visa na tiketi zinaendelea, naomba ushauri on a serious note kwa wadau

Depressed hubby


Sent from my iPhone using JamiiForums

Put yourself in her shoes..., ungekuwa wewe na kuna safari ya muhimu kwako na mwenza wako anakuzuia kwenda ungefanyaje ? Pia kwenye hio paragraph yako sijui hio for good imetoka wapi.
 
Hahahahaaaaaaaa, mnikungulyabhashashi ulemhola ong'wise?! Na mie uje uniongezee kwenye list yako ya wabeba box mkuu.
Mbeba box mtarajiwa huyo. Nipe jina lake nimwandikishe kwenye daftari la wabeba box.
 
Unajua maana ya rizq 'halali' wewe? Sidhani kama unajua.

Licha ya kutojua kwako, umalaya si haramu sehemu zote duniani. Zipo sehemu ambapo umalaya ni moja ya shughuli rasmi tena yenye kutozwa kodi kabisa.

Na madhali mtu kaamua kujikita huko ili kujipatia mkate wake sioni kwa nini asijivunie kutoa huduma kwa watu wanaoihitaji huduma anayoitoa.

Sijui unamaanisha nini kujua maana ya hiyo kitu na kila kazi ina context yake ya ku-determine uhalali na uharamu wake.Nilipoweka reference ya dada zetu nilimaanisha our TZ context na si huko unakotaja.Kwa Busara ya Mu7 vitu vinavyokubalika na wazungu si lazima viwe na maana sawa kwetu.Naomba unijibu kwa argument yako dada zetu wanafanya kazi halali?Wanaishi kwenye vyumba vya kupanga,kula na kusomesha wakati mwingine kwa biashara hiyo.
 
Put yourself in her shoes..., ungekuwa wewe na kuna safari ya muhimu kwako na mwenza wako anakuzuia kwenda ungefanyaje ? Pia kwenye hio paragraph yako sijui hio for good imetoka wapi.

Nimekataa safari 2 za ughaibuni for family reasons mpaka kupelekea mausiano mabovu na kaka yangu aliye ughaibuni,think bigger


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nimekataa safari 2 za ughaibuni for family reasons mpaka kupelekea mausiano mabovu na kaka yangu aliye ughaibuni,think bigger


Sent from my iPhone using JamiiForums

Inategemea mtu unakwenda kufanya nini na malengo yenu katika maisha.., Life ni kushauriana na kupanga mikakati pamoja hii dunia ishakuwa kijiji na ughaibuni panaweza kuwa rahisi kufika / kuonana au ku-communicate kuliko hata mtu aliyepo misasi.

Pangeni mikakati yenu muelewane, kumkatalia mtu kitu ambacho anaona ni opportunity kwake kunaweza kuleta chuki na ugomvi mbeleni ambao hautaisha kamwe.
 
Ana hofu ya Mungu ila mlezi wake ughaibuni amekuwa sio msaada kwake kwa mda mrefu Kama Miaka 6 nliyoishi nae,sasa ghafla anataka kumchukua na yeye aende huko bado hajamwambia atakachokwenda fanya huko

Sent from my iPhone using JamiiForums

Tegemea maumivu ewe kijana...
 
Sijui unamaanisha nini kujua maana ya hiyo kitu na kila kazi ina context yake ya ku-determine uhalali na uharamu wake.Nilipoweka reference ya dada zetu nilimaanisha our TZ context na si huko unakotaja.

Hata kama ni Tanzania, kama hiyo biashara haijaharamishwa na sheria, nini ubaya wake? Na kama ina ubaya, kwa nini huo ubaya uonekane katika upande mmoja tu wa mtoa huduma. Mtaka huduma naye je?
Kwa Busara ya Mu7 vitu vinavyokubalika na wazungu si lazima viwe na maana sawa kwetu.
Museveni ni mjinga tu kama walivyo Waafrika wengine. Halafu sisi Waafrika ni wanafiki sana. Hapa wewe unadokeza kuwa umalaya ni jambo lililokubalika na Wazungu kama vile hapa kwetu haukubaliki. Hii migesti yote iliyojaa kila kona ya nchi ni madanguro bubu na sote tunajua nini kinachoendelea humo. Lakini tunajifanya kama vile tuna maadili sana na kwamba mambo fulani fulani hayakubaliki kwetu. Umalaya usingekuwa unakubalika hizo gesti zilizoenea kama uyoga zisingekuwepo, watoa huduma nao wasingekuwepo kwa wingi hivyo, na watafuta huduma nao wasingekuwepo. Kumbuka, hakuna biashara ya upande mmoja tu. Muuzaji hawezi kuwepo bila mnunuzi.

Naomba unijibu kwa argument yako dada zetu wanafanya kazi halali?

Halali kwa mujibu wa nini na nani? Kwa mujibu wa sheria? Na hivi huwa wanafanya hiyo kazi peke yao?

Wanaishi kwenye vyumba vya kupanga,kula na kusomesha wakati mwingine kwa biashara hiyo.

Kama hiyo ndo shughuli inayowaingizia rizq halali, I can't knock their hustle. Lakini siwezi kuwa naenda kununua huduma zao halafu eti nijifanye nawadharau. Huo utakuwa unafiki wa daraja la kwanza!!!!!!!!!!
 
Hi wadau,
Mi ni mgeni Hapa JF ila napenda kushare Jambo linaloninyima usingizi.Mke wangu anataraji kusafiri kwenda ughaibuni ifikapo mwezi wa nane,nimezaa nae mtoto mmoja na naishi nae katika mji mkoa mmoja Hapa Tz.Safari yake hii imegubikwa na utata kutokana na kwamba mlezi wake amemwita na hajui atachukua mda gani huko ughaibuni,Maisha yetu Hapa bongo si mazuri sana,na yeye anashawishika kumwacha mtoto kwa mzazi wake na kwenda ughaibuni.Sasa inaniwia ugumu kumuachia aende. Hebu put yourself in my shoes ingekuwa wewe ungelifanya nini,ukizingatia invitation imeshafika na process za visa na tiketi zinaendelea, naomba ushauri on a serious note kwa wadau

Depressed hubby


Sent from my iPhone using JamiiForums
Fimbo ya mbali?


Hivi niulize... Mke anachukuliwaje na mlezi wakati mume anaachwa?

Huyo Si wako
 
Kama ni mkeo utasemaje hujui anaenda kufanya nn?je doc au invitation letter inayomruhusu kuomba viza inasemaje?

Huyo si mke wako, nadhani ni hawara yako ndo maana mlezi wake amekuwa na nguvu za kumwita ughaibuni bila ya kukushirikisha, kwa vile hana sababu ya kufanya hivyo, na kuwa hata huyo mtoto kisheria za dini ni wa mama...si wako abadan.

Tafuta mke uoe mzee!
 
Maisha ni kutafuta popote pale muache aende ila usisahau kumpa nasaha naamini atakuelewa tu ila pia kitu kimoja ukizingatie mkeo akiondoka usiingize mwanamke mwingine ndani ya nyumba yenu hata kama kwa siri akija kujua amekuacha mazima.

Vipi K yako bado ina ganzi kwa mmeo?
 
If i were you.. For a good reason, hiyo safari ningeiblock for a good reason....

How comes wife aende sehem bila kujua afuatacho wala kurudi ni lini? Itaniuma....

Unajua hata kwetu ni nje ya nchi ukiwa nchi za watu...

She better stay home for good.


Hiyo ndoa imevunjika kwenda kuishi ng'ambo ni sawa na uchawini kutoka ni shida na kule tokana na misukosuko ya nchi mpya na mahangaiko ya kujiweka sawa kukabili maisha mapya wakati bwana hayupo kufungua pochi au kugawa tunda la katikati ili apate msaada kwa wenyeji lazima. Angekuwa chuoni sawa kule ni safe lakini sio mtaani na hana mme yuko single, unless she is God fearing woman kwa wakristo ni born again kwelikweli na kwa waisilamu swala tano kweliweli ndio atasalimika
 
Welp, kila siku mimi nakutana na watu wanaojivunia kazi zao.
haya hongera zao.. but there is a lot in their heads..!

most of them ukichunguza utakuta wana elimu ndogo... haiwezekani ujivunie kazi isiyokulipa..

hata kama mazingira ya kazi yawe mazuri vipi, watu wanaangalia maslahi!
 
Back
Top Bottom