Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,153
- 137,160
Tatizo letu wabongo tunadharau sana utafikiri hapa bongo wote ni maofisa ndio maana wanadharau hata manesi wetu hapa bongo. Kipi bora kutapeli watu au kufanya kazi halali
Unajua sisi wakati mwingine huwa nadhani akili zetu haziko sawa kabisa.
Na sijui nani tu aliyetuaminisha kuwa baadhi ya kazi ni kazi za hovyo!
Mtu anajihangaikia kujitafutia rizq yake halali huku akikuhudumia wewe halafu wewe huyo huyo eti unamdharau kwa kazi anayoifanya. Kama vipi si ujifanyie mwenyewe yote hayo unayoenda kwa wengine kufanyiwa....
Wakati mwingine huwa tuna upumbavu wa kijinga sana (as if kuna upumbavu wa akili).