Mke wangu amepanda cheo, ananidharau

Mke wangu amepanda cheo, ananidharau

Hii ni inferiority unaionyesha, na kamwe haitaijenga ndoa yenu; inawezekana wewe ndio unaanza mjengea mtazamo hasi, baadala ya kumpongeza na kumtia moyo; kukopa bank bila taarifa inaelekea amani kwenu haipo tena kila MTU anajiamulia mambo yake;
halafu hizi tabia huwa ni za wanawake wa kichaga kwa sana... kwanini?
 
Mke wangu amepanda cheo kazini. Tangu amepata cheo anaonyesha dharau; amebadilika tabia.

Zaidi amekopa benki bila kunitaarifu. Nifanyeje?
Mabadiliko gani exactly?
Cheo kapanda kivipi (low to middle or juu kabisa)
Kabla mlishirikishana kila kitu nyumban kama mikopo ect?
Mna watoto mkuu?
 
Mke wangu amepanda cheo kazini. Tangu amepata cheo anaonyesha dharau; amebadilika tabia.

Zaidi amekopa benki bila kunitaarifu. Nifanyeje?
Kama anafanya hayo ili uumie, na wewe MPUUZE. Pesa ni zake. Akishaelewa fahari na ndoa ni maji na mafuta ataacha. Endelea kuwa baba otherwise ni hisia tu ndio zinakutuma uwe na wivu.
 
Mke wangu amepanda cheo kazini. Tangu amepata cheo anaonyesha dharau; amebadilika tabia.

Zaidi amekopa benki bila kunitaarifu. Nifanyeje?
Kama anafanya hayo ili uumie, na wewe MPUUZE. Pesa ni zake. Akishaelewa fahari na ndoa ni maji na mafuta ataacha. Endelea kuwa baba otherwise ni hisia tu ndio zinakutuma uwe na wivu.
 
asa na wewe si umuoe hausigeli iwe ngoma droo
 
We umejuaje anakudharau, isije kuwa unahisi tu unadharaulika sababu tu ya kapanda cheo. Huo ni wivu, acha wivu mtoto wa kiume mlee familia yenu. Cheo ni dhamana na ni baraka kutoka kwa Mungu
 
Nawe panda tu kwani vyeo unalipia bei gani kupanda? Tunaweza kukuchangia kama mwana jamvi mwezetu. Inaezekana kabisa mkeo kuna vitu vimempandisha vyeo....kama ni taaluma yake itabidi urudi shule na kama unamwachia anavaa kiasi cha kutamanisha mabosi zake mpaka wakampandisha na cheo sioni sababu ya kuja kutuomba ushauri. Ni hayo tu mkuu
 
halafu hizi tabia huwa ni za wanawake wa kichaga kwa sana... kwanini?
Kwani huyu anayelalamika kadharauliwa ni mwanaume Wa kabila gani? Au nae ni Wa kichaga? Na tabia za wanawake Wa kichaga ni Zipi?
 
Ukiona mahusiano yko yameanza kuwekewa vikao ujue yashkufa hayo,,,,unapoteza muda uliobaki bure
 
IMG-20170210-WA0012.jpg
 
Mke wangu amepanda cheo kazini. Tangu amepata cheo anaonyesha dharau; amebadilika tabia.

Zaidi amekopa benki bila kunitaarifu. Nifanyeje?
Dah... Wanaume wanazidi kutoweka duniani siku hadi siku..... Kuhusu za makusudi zinahitajika kuokoa Hii jinsia
 
Zama na nyakati zimebadilika......hivyo na vijana wanatakiwa wabadili mitazamo yao katika masuala ya ndoa hasa kwenye nyakati hizi ambazo wanawake na wao ni miongoni mwa wanaotafuta mkate wa kila siku........

Unatakiwa ubadilishe mtazamo kutoka kumchukulia mwanamke kama mama wa nyumbani bali unatakiwa umuone kama mtu anayekusaidia baadhi ya majukumu hapo nyumbani kupitia mshahara wake........

Mtazamo huo utakufanya ujue changamoto na mikiki mikiki anayopitia mkeo akiwa kazini ni kama wewe vile uwapo kazini.....hivyo kupambana na changamoto hizo ili maisha yaendelee kunahitaji jitihada na uvumilivu wa hali ya juu......

Inawezekana mkeo wala hajakudharau bali ni wewe umegoma kubadilisha mtazamo wako juu yake na umeshindwa kuenenda saawa na mabadiliko yake........

Inawezekana umekuwa mkali katika mambo ya kijinga na yeye ameamua kukaa kimya kwa heshima yako kama mume

Inawezekana hata wewe ulikuwa unamnyanyasa na kumsimanga zamani akiwa hana kipato na sasa umeshikwa na wivu kuona kuwa mambo mengi aliyokuwa anakusumbua ana yamaliza mwenyewe kwa mshahara wake......

Suluhu pekee la tatizo lako ni wewe kubadili mtazamo wako juu yake na kuongea naye......huyo ni mkeo ni rafiki yako....mwandani wako....msiri wako na wala sio adui yako......

Vunja ukimya sema naye.....
Umeongea point sana.. kiasi nakosa hata cha kuongezea.. kufikiri kila mtu anaweza ila kufikiri vema si kila mtu anaweza.... Maisha ya sasa yamebadilika, hivyo yafaa nasi tubadilike ili kuendana nayo.. huyu jamaa nadhani anasumbuliwa na fikra za mfumo dume, abadilike..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom