Mke wangu amenizidi mshahara

Mke wangu amenizidi mshahara

kwanza umeandika kishari shari, kiugomvi ugomvi, dizaini kama unamkoa hivi.... hizi ndoa jamani, ehhh mungu zisimamie. kama mimi ndio mkeo, huo utumbo siwezi kuukubali hata iweje, akikubali mkeo, atakua kiazi kama wewe.... akope pesa, yeye, mlipaji yeye, ili wewe ufaidike maana unataka kumzidi kipato kwa mgongo wa huyo huyo mkeo... kweli stupid...
 
Hahahahahaha, dah mkuu umenifanya nicheke sana. Kwa hiyo wewe tatizo lako ni kwamba anakuzidi mshahara na sio kama analeta madhara mengine?
 
kwanza umeandika kishari shari, kiugomvi ugomvi, dizaini kama unamkoa hivi.... hizi ndoa jamani, ehhh mungu zisimamie. kama mimi ndio mkeo, huo utumbo siwezi kuukubali hata iweje, akikubali mkeo, atakua kiazi kama wewe.... akope pesa, yeye, mlipaji yeye, ili wewe ufaidike maana unataka kumzidi kipato kwa mgongo wa huyo huyo mkeo... kweli stupid...
kwa bahati mbaya umeshazeeka bila kuwahi kukutana na mwanaume ambaye umempenda sana na ndiomaana unaona kama haiwezekani. Umri wako ushapita, waachie vijana.
 
Hahahaha nmecheka sana, ila inaonekana mkuu una Elimu nzuri ila ulipo hapakustahili, hongera kwa kujiongeza....hapa hujatumia mfumo dume wala nini ila umeona mbali kuwa mkeo kukuzidi kipato ipo siku ataota mapembe....ndo ujanja wa Capitalism huo unachofanya, safi sana, keep up
 
Hahahaha wakati unamuoa hukujua kuwa ana mshahara mkubwa kuliko wewe?
 
Wadau,

Mke wangu amenizidi mshahara, kwa mfano: kama mimi napokea mshahara sh laki moja basi yeye anapokea laki mbili-ukijumlisha na house allowance, transport na pesa nyingine zisizo na kichwa wala miguu.

Hii kiukweli siipendi kabisa toka muda mrefu kama mwanaume, sasa nimekuja na mkakati ufuatao wa kumzidi kipato mke wangu nitahitaji mawazo yenu.

Nataka nimshauri mke wangu aende akachukue mkopo bank (mkubwa tu kwa mshahara wake) na baada ya kumchukua mkopo ukichanganya na akiba tuliyonayo nataka tufungue kampuni( tayari nimeshaanza michakato michakato)

Ambayo mimi nitakuwa msimamizi mkuu wa uendeshaji wa kampuni. Mapato yote yatakayokuwa yakiingia mimi ndio nitakuwa controller kwakuwa yeye kazi yake inambana sana na hawezi kupata nafasi ya kufatilia kwa undani sana biashara inavyoenda.

Kwa mkakati huo hapo juu basi mke wangu atakuwa anakatwa pesa bank kutoka kwenye mshahara wake (kwa miaka mitano mfululizo) huku mimi mshahara wangu ukiwa vile vile-hapo nitakuwa nimeshampiga pigo la kwanza

Kwa kipindi hicho chote mi ndio nitakuwa controller wa ofisi na mpaka inaisha hiyo miaka mitano ya kukatwa pesa ya mkopo na bank basi kampuni yetu itakuwa imekwisha simama na ina generate faida nzuri hivyo hata akishamaliza mkopo na kuanza kulipwa mshahara wake mi nitakuwa naingiza pesa nyingi kwenye kampuni-Pigo la pili

Kampuni isipofanikiwa nitafanya nini?
Nitanunua kiwanja, baada ya hapo nitamwambia akachukue mkopo tena bank mkubwa mara dufu ya ule ambao atalipa hata kwa miaka 10, kisha tunajenga apartments za kupangisha mi ndio nitakuwa mpokeaji wa kodi.

Mwanamume ni mwanaume tu wadau na usikubali mwanaume tu.Wadau usikubali mkeo aukuzidi pesa atakuwa na kiburi

Karibuni
Nimeishia kutabasamu kwa namna unavyopiga mahesabu ya kumpiga bao mkeo.
 
Back
Top Bottom