Mke raha jamani

Mke raha jamani

Ukifikia umri wa uzee kama wangu, utaenjoy zaidi! Just be faithful to each other and God help you!
 
Yani binadamu hatupendi kusikia taarifa nzuri za ndoa. Tunataka tusikie mabaya tu ya ndoa ndo roho zetu kwatuuu. Mtu akishukuru kwa ajili ya ndoa yake, utasikia tu "ndoa yako ina muda gani ", " subiri baada ya miaka 5 tuone " eeeeh. Mwaego shukuru tu kwa ndoa yako hata kama ina mwezi. Kuna watu wanaoana asubuhi jioni ndoa chaliii. Majaribu ni kawaida tu hata kwa ambao hawapo kwenye ndoa. Na asiyeshukuru kwa kidogo hata kwa kikubwa hatoshukuru. Mbarikiwe mwaego

Umeona ee,humu mwenzangu hawataki kuskia mazuri ya ndoa.Ukionesha kwamba ndoa ina raha wanaanza kukutabiria mabaya.Hivi furaha ya watu ni ndoa kuvunjika eti.Mungu azidi kutupigania wanandoa wote.
 
Umeona ee,humu mwenzangu hawataki kuskia mazuri ya ndoa.Ukionesha kwamba ndoa ina raha wanaanza kukutabiria mabaya.Hivi furaha ya watu ni ndoa kuvunjika eti.Mungu azidi kutupigania wanandoa wote.
Amen mpendwa,
 
Zipo raha za kua ndani ya ndoa lakini pia usiwashauri tu ambao hawajoa kua waoe eti kwa sababu ndani ya ndoa/ kua na mke ni raha.

Zipo karaha na vitimbi vya ndani ya ndoa ambavyo huwakuta wanandoa wengi zaidi.

Ni vyema kama ungeweka Raha na Karaha zipatikanazo ndani ya ndoa ili huyu unayemshauri ambaye bado hajui ndoa ni nini awe na uhuru mkubwa wa kuamua, je aingie kwenye ndoa au La!
sasa wasiwasi wa nini sasa ndoa ni kutimia akili za kichwani na kuipeleka kama biblia inavyotuambia kwamba mwanaume ni kichwa cha nyumba na mkewe amheshimu baasi ila mkiingiza maigizo ya filum za kikorea lazima muone ngumu
 
subiri bado muda wa kulia

Hhahahaha ukiwa negative lazima upate impact yake coz utaishi kwa kijiahami ila ukiwa huru baasi mambo yatakuwa murua uwazi na ukweli ndani ya ndoa ni muhimu sana na kuacha maigizo ndoa nyingi sasa hivi zinavunjiaka coz ya kuiga
 
Afadhali hata leo nimekutana na thread ya raha za ndoa, maana humu kila siku ni majanga tu.

Hongera sana mkuu na Mungu azidi kuwapigania iwe raha daima.
 
acha kabisa hyo kijineno ina raha sana sometimes hata mtu anakuambia samahan hamaanishi lakini unajikuta umeanza kulegeza mnunoo,

kuna ile mtu anakusogelea hata kama umenunaje anakushika mkono anakutizama kidogo kama dakika moja then akuita jina lako, mke wangu, mpenzi n.k then anasema nisamehe/ naomba unisamehe najutia hili kosa sikustahili kukufanyia hivi najisikia moyo unajuta, tehtehteh akiona unazingua bado anakukumbatia closeeee anaongezea nisamehe please naahidi kujirekebisha aaaahhh weee utaishia tu alafu mi thipeendi unaniuzigi kama nini kwanini ulifanya hivyo niache huko wakati ushajichekesha tehtehteh( siri hyo nmewapa)

Hiii kawaida sana kwenye ndoa hahahahahahahhhh
 
Zipo raha za kua ndani ya ndoa lakini pia usiwashauri tu ambao hawajoa kua waoe eti kwa sababu ndani ya ndoa/ kua na mke ni raha.

Zipo karaha na vitimbi vya ndani ya ndoa ambavyo huwakuta wanandoa wengi zaidi.

Ni vyema kama ungeweka Raha na Karaha zipatikanazo ndani ya ndoa ili huyu unayemshauri ambaye bado hajui ndoa ni nini awe na uhuru mkubwa wa kuamua, je aingie kwenye ndoa au La!

Kweli kabisa mkuu!!!,huyu jamaa ameegemea upande mmoja tu.
 
AH WAPI! mi mwenyewe kishanuka huko ndo maana nimejikuta tu Hapa jf usiku wote huu,
baada ya muda mfupi utakuja na part 2 ya uzi huu itaKAyosomeka
SIOI TENA!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom