Mke ni nani? Rafiki au ndugu?

Mke ni nani? Rafiki au ndugu?

mke si ndugu yako na wala si rafiki yako. Mfano; ukifa wewe mwanaume siku ya mazishi wakisema ndugu wa marehemu wasimame yeye hawezi kusimama na wakisema rafiki wa marehemu wasimame pia hawezi kusimama ila wakisema mke wa marehemu asimame basi atasimama. Kwa hiyo mke sio ndugu wala rafiki yako bali ni mke wako. Asanteeee!
 
Wife is a partner.

Look. We have three DIFFERENT people here: (1) a born relative - naturally, (2) a friend - socially (3) a spouse (wife/husband) - legal intimacy.

Often it happens that a friend of opposite sex may turn into a spouse. So Mke ni Mke...(mara nyingi ni rafiki aliyepanda cheo).
 
Huu msemo huwa unanitatiza sana kwa nini mwanamume anaambiwa awaache baba na mama yake aambatane na mkewe ndio maana wazazi wa mke bado wanakuwa benet kwenye ndoa ya mtoto wao au vipi embu baelezee

Nafikiri hii inatokana na tofauti ya kisaikolojia zaidi
kati ya mwanamke na mwanaume.

Kimsingi (primal level) kwa mwanamke kujenga
mahusiano ni muhimu wakati mwanaume kujenga
himaya ndiyo kitu muhumu.

Mwanamke japokuwa anakuwa ameolewa yeye
anauwezo waku-maltitask familia yake na ile ya
kwao, pia hupenda kuendeleza uhusiano na
familia iliyomlea kwa miaka mingi.

Kwa mwanaume kujenga mji wake ndiyo kitu
muhimu kule alikotoka mmiliki wa ile himaya ni
baba yake. Yeye akishaoa huwa hana lake kule
zaidi ya kusaidia kama kuna matatizo.
 
Kama Mke ni Ndugu, kwa nini Wanandoa Wanadivorce? Undugu hauvunjwi.

Kama ni Marafiki, kwa nini Mnazaa watoto na kuishi pamoja hadi mwisho wa wakati. Marafiki si lazima wawe hivyo.

Ndahani yuko yuko inbetween yaani ni: NDUGURAFI
 
Kama Mke ni Ndugu, kwa nini Wanandoa Wanadivorce? Undugu hauvunjwi.

Kama ni Marafiki, kwa nini Mnazaa watoto na kuishi pamoja hadi mwisho wa wakati. Marafiki si lazima wawe hivyo.

Ndahani yuko yuko inbetween yaani ni: NDUGURAFI
kwa hiyo wanaosema kuwa mwanamke katuka ubavuni mwa mwanaume wako sahihi? Je kwanini wanaume wanatunyanyasa?
 
du, kweli hatupendeki, hayta kiasi cha kuutoaa uhai wetu kwa ajili ya wenzetu
 
Mke siyo ndugu wala rafiki wala adui. Mke ni wewe jinsi ulivyo ndivyo mke alivyo! Hapa namaanisha mke na si vingine.
Tatizo sasa wengi wanaingilia huko wakijifanya wake kumbe siyo. Akiolewa na mtu mwenye pesa halafu zikiisha wanaondoka; huyo hakuwa mke, bali mjasiriamali mmoja aliyeingia kwa ngozi ya mke ktk maisha ya huyo mume.
 
MKE NI NDUGU RAFIKI, undugu unaweza kufa kwa kutalikiana urafiki ukabaki kwa watoto kama mlibahatika kuzaa, MUNGU akiwa amewajaalia kuishi maisha mkazikana basi undungu kamili unakuwepo unafuta urafiki. kabla ya hapo chochote chaweza kutokea hasa kwa ndoa za kisasa vinginevyo ujaaliwe kupata mke aliyetoka ktk familia ya waungwana naye pia akawa na tabia hiyo, kwani si kila sheikh anazaa mtoto sheikh
 
mke si ndugu yako na wala si rafiki yako. Mfano; ukifa wewe mwanaume siku ya mazishi wakisema ndugu wa marehemu wasimame yeye hawezi kusimama na wakisema rafiki wa marehemu wasimame pia hawezi kusimama ila wakisema mke wa marehemu asimame basi atasimama. Kwa hiyo mke sio ndugu wala rafiki yako bali ni mke wako. Asanteeee!

Nimeamini wewe ni Prof..........

Umenena vyema kabisa Prof......................
 
Mke ni adui yako unaelala nae kitanda kimoja:A S 465::A S 465::A S 465:
 
Mke siyo ndugu wala rafiki wala adui. Mke ni wewe jinsi ulivyo ndivyo mke alivyo! Hapa namaanisha mke na si vingine.
Tatizo sasa wengi wanaingilia huko wakijifanya wake kumbe siyo. Akiolewa na mtu mwenye pesa halafu zikiisha wanaondoka; huyo hakuwa mke, bali mjasiriamali mmoja aliyeingia kwa ngozi ya mke ktk maisha ya huyo mume.

maisha ya leo hii mbona ipo sana? Wanawake wengi tunaolewa ili tufanyiwe kitchen party, send off na harusi. Matokeo yake tukiingia kwenye ndoa tunakuwa hatuna uvumilivu wala mapenzi ya dhati.
 
Mke ni Mke, ndani ya uanamke wake (ndoa), ndio urafiki na undugu unapojengwa.
 
"if you love me be my friend first" Celine Dion.
Mke mke! Mume mume!
Upendo = mapenzi.
Kwahiyo katika kuwa na mme au mke hayo mengine ni matokeo tu na yanasolution.
Kama uadui hata wazazi wako wanaweza kuwa. Japo kwa wengine mke huwa hata kijakazi na wengine mume huwa ATM. Basi nyeusi ibaki kuwa nyeusi na nyeupe iwe nyeupe.

"KWANI NANI HUFANYA MTIHANI AKITEGEMEA KUFELI?"
 
Back
Top Bottom