MasharubuMYJ
Member
- Sep 26, 2018
- 15
- 44
Mimi ni mwanaume wa miaka 35, nilioa mwaka 2009 kabla ya kuoana tulipima na wote tulionekana tupo salama.
Tukazaa watoto wawili, mwaka 2013 mke alianza kuumwa, alikuwa anatibiwa homa inarudia rudia, baada ya hali kuzidi akashauriwa kupima ukimwi mwaka 2015 na ndipo akagundulika kuwa ameathirika, na mimi nikapima zaidi ya mara tatu nikaonekana ni negative.
Kwa muda wote huo tumekuwa tukitumia mipira katika tendo la ndoa kimsingi tangu nilivyooa sikuwahi kuchepuka shida niliyonayo mimi kwa sasa najawa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu hadi nimepungua kiukweli, sioni radha yoyote kwenye tendo, sipati msisimko wowote kwake moyo umekufa kabisa.
Nikiwa nae karibu ndio najawa na mawazo, sioni mapenzi yoyote kwake kibaya zaidi hajawahi kuniambia alipataje na nikimuuliza anaanza kulia hadi kuchukua sumu kutishia kujiua ninashindwa nifanyaje nikijiangalia na umri wangu bado mdogo.
Naomba ushauri wenu wadau nifanyaje kwa sababu yeye anaonekana ana njaa kubwa ya tendo la ndoa na mimi hali ndio hivo.
Tukazaa watoto wawili, mwaka 2013 mke alianza kuumwa, alikuwa anatibiwa homa inarudia rudia, baada ya hali kuzidi akashauriwa kupima ukimwi mwaka 2015 na ndipo akagundulika kuwa ameathirika, na mimi nikapima zaidi ya mara tatu nikaonekana ni negative.
Kwa muda wote huo tumekuwa tukitumia mipira katika tendo la ndoa kimsingi tangu nilivyooa sikuwahi kuchepuka shida niliyonayo mimi kwa sasa najawa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu hadi nimepungua kiukweli, sioni radha yoyote kwenye tendo, sipati msisimko wowote kwake moyo umekufa kabisa.
Nikiwa nae karibu ndio najawa na mawazo, sioni mapenzi yoyote kwake kibaya zaidi hajawahi kuniambia alipataje na nikimuuliza anaanza kulia hadi kuchukua sumu kutishia kujiua ninashindwa nifanyaje nikijiangalia na umri wangu bado mdogo.
Naomba ushauri wenu wadau nifanyaje kwa sababu yeye anaonekana ana njaa kubwa ya tendo la ndoa na mimi hali ndio hivo.