Mke hataki kusikia mumewe akimuelezea mdhaifu yake........

father-xmas

JF-Expert Member
Mar 23, 2010
835
642
Hapa majuzi nilikutana na mshikaji wangu akiwa hana raha.............kumuuliza nini tatizo..........anadai wamegombana sana na wife.................kisa eti mshikaji alimweleza wife wake kwamba enzi za ujana wake siku moja alijaribu kuvuta sigara.............lakini baada ya pafu mbili jamaa akawa kama kalewa hivi akashindwa hadi kutembea ikabidi ashikwe huku na huku...............pia akamuhadithia mkewe kuwa akinywa tu chupa moja ya bia analewa tilalila.................Jamaa anadai baada ya maelezo hayo mkewe akamwambia..............mume wangu sisi wanawake tunapenda kuamini kuwa wanaume zetu ni superman tunasahau kuwa wameumwa na nyama kama sisi wanawake............jamaa anadai mkewe akaendelea kuwa...........eti maelezo ya mumewe yamem-put off na yanamfanya amuone mumewe kuwa yuko weak jambo ambalo linamfanya eti mke huyo amuone mumewe unatractive......................jamaa anadai kuwa wife anadai wanawake wote wanapenda kuamini kuwa wanaume zao wananguvu kuliko wao(wanawake) lakini eti wife wa jamaa anadai yeye havuti sigara lakini anaamini hata akivutwa sigara nzima hatabebwa kama mumewe alivyobebwa baada ya kuvuta pafu mbili...............................Jamaa anadai mkewe amemuomba asimuhadithia tena story za aina hii..................Jamaa naye anadai maneno ya mkewe yamejaa dharau......................

Wakulu hii kesi nimeiletwa kwenu nisikie na nyinyi mna lipi lakusema.......................................!
 
Hakuna kesi hapo...just another piece of crackass bu#$shit story telin artistic business.
 
lakini eti wife wa jamaa anadai yeye havuti sigara lakini anaamini hata akivutwa sigara nzima hatabebwa kama mumewe alivyobebwa baada ya kuvuta pafu mbili...........................................!

Nimechekaaaje....., mwambie jamaa sio wote wanawake wanaoamini hivyo kuna wale walioenda unyago wakaambiwa kuwa waabudu waume zao maana wao ni wasafi basi atakuwa ni mmoja wapo. Lakini kuna wengine who believe in imperfection makes perfect.
 
Nimechekaaaje....., mwambie jamaa sio wote wanawake wanaoamini hivyo kuna wale walioenda unyago wakaambiwa kuwa waabudu waume zao maana wao ni wasafi basi atakuwa ni mmoja wapo. Lakini kuna wengine who believe in imperfection makes perfect.

hapo bold patamfariji jamaa yangu....................tatizo litabaki kuwa mke anamuona mumewe kuwa ni dhaifu.................
 
Kila mtu anaudhaifu wake, haujaona mwanamme anaogo inzi?

hapo nilopo bold nadhani ulitaka kuandika anaogopa inzi...kama ndivyo sinabudi kusema huyo mwanaume inabidi unapoanza kumwita utangulize jina la dadake baba kwa kiingereza kisha unataja jina lake la kiume...lazma awe maji-magumu full kuomba msaada "atafuniwe"..lazma iwe type ya wanaojiita mabaunza kwa uwezo wao mkubwa wa kuvunja yai..etc
 
Pole father, ndio maana huwa tunatakiwa tujue kuna vitu vya kusema na kuwambia wenzetu kuna vingine tunamezea na kukaa navyo mioyoni mwetu,mie naeza chukia kitu kidogo sana kwa mpenzi wangu, lakini vingi navipenda inabidi nivumilie coz hakuna binadamu aliye perfect kabisaaaa
Mwambie mkeo tu umemsikia ila hujapenda alivyoichukulia hiyo issue kihivyo coz sie ni binadamu kila mtu ana ability yake katika kila kitu, mie naweza kunywa JD chupa nzima lakini bf wangu hawezi kufika hata robo chupa hii haifanyi nimdharau,coz najua kila mtu ana uwezo wake
 
Pole father, ndio maana huwa tunatakiwa tujue kuna vitu vya kusema na kuwambia wenzetu kuna vingine tunamezea na kukaa navyo mioyoni mwetu,mie naeza chukia kitu kidogo sana kwa mpenzi wangu, lakini vingi navipenda inabidi nivumilie coz hakuna binadamu aliye perfect kabisaaaa
Mwambie mkeo tu umemsikia ila hujapenda alivyoichukulia hiyo issue kihivyo coz sie ni binadamu kila mtu ana ability yake katika kila kitu, mie naweza kunywa JD chupa nzima lakini bf wangu hawezi kufika hata robo chupa hii haifanyi nimdharau,coz najua kila mtu ana uwezo wake

kuna dada niliwahi kumsikia akisema kwamba...............kuna machafu mengi amewahi kuyafanya ujanani.............lkn kamwe hawezi kumuhadithia mchumba wake sababu anajua hata huyo mchumba wake anamwambia vitu vile vinavyofanya aonekane mwanaume wa maana................ila mim nadhan bora mke wa jamaa alipoomba asihadithiwe story za aina hii sababu jamaa ameshajua kuwa zinam-put off wife............hatari ninayoiona ni mume kuanza kudanganya kuwa anaweza kufanya hata vitu ambavyo haviwezi ili wife amuone superman........................
 
Akaze buti upande wa linalowaweka pamoja heshima itarudi......hilo tu pekee ahilwezi kumfanya wife amuone jamaa weak

Opinion; (1)Wife aweza kuwa na correlation yake kichwani ndo maana anafikia hiyo apex
(2)Asimamie nafasi ya ubaba hapo home yaweza kuwa wife wake hazimiki bedtime stories halafu ye kila wakiwa chemba anampa mastory ya utotoni kibaaaaoooooooo.......hadi za manati kukatika ukiwa unalenga ndege

APIGE KAZI KIUKWELI KESHO ATACHEKEWA MPAKA JUA LICHWE
 
Jamaa yako ana allergy, ni vyema akapata ushauri wa kitabibu. Allergy sometimes zinaua, people tend to forget. Kuhusu huyo mwanamke amsamehe tu, mindhali wameoana waendelee kuheshimiana hata kama mmoja amepungukiwa hekima au ujuzi.
 
..eti maelezo ya mumewe yamem-put off na yanamfanya amuone mumewe kuwa yuko weak jambo ambalo linamfanya eti mke huyo amuone mumewe unatractive......................jamaa anadai kuwa wife anadai wanawake wote wanapenda kuamini kuwa wanaume zao wananguvu kuliko wao(wanawake)

Ndugu hapo kwenye Rangi,

Unatractive kwa sababu akinywa pombe analewa????????

Unadhani wale wanao pigana mieleka wakinywa pombe hawalewi?????????

Sijaelewa ,vizuri, Nadhani kuna sababu nyingine, Hebu waulize vizuri
 
Hii ni thread nzuri sana kwangu inayonionyesha jinsi baadhi ya wanawake wanavyowachukulia wanaume. Nilimsikia mwanamke mmoja akimwambia boyfriend wake:'Wacha kunitania.Eti umeishiwa? Wanaume wanaishiwaga?'
Umeona eh! Yapo mambo ambayo baadhi ya wanawake hawaamini kabisa kwamba yanaweza kuwatokea wanaume.

Kwa hiyo huyo rafiki yetu alipotaka kuwa mkweli kwa mkewe, mkewe aliona huo si uanaume. Pengine huyo mama ndivyo alivyolelewa. Pengine alipokuwa msichana mdogo alimsikia baba yake au kaka zake wakitamba sana juu ya ubingwa wa wanaume kwa kila kitu. Huyo bwana asiendelee na akome kueleza mambo yanayompa taabu. Asije akamwambia mkewe , kwa mfano, Ninaogopa sana nyoka au Nikila chakulab fulani najambajamba sana. Mkewe atamkimbia!

Halafu neno dogo kwa mleta post: Kwa nini umeweka dashdash nyingi kwenye post kama mtihani wa kujaza maneno wa darasa la saba?
 
Hapa majuzi nilikutana na mshikaji wangu akiwa hana raha.............kumuuliza nini tatizo..........anadai wamegombana sana na wife.................kisa eti mshikaji alimweleza wife wake kwamba enzi za ujana wake siku moja alijaribu kuvuta sigara.............lakini baada ya pafu mbili jamaa akawa kama kalewa hivi akashindwa hadi kutembea ikabidi ashikwe huku na huku...............pia akamuhadithia mkewe kuwa akinywa tu chupa moja ya bia analewa tilalila.................Jamaa anadai baada ya maelezo hayo mkewe akamwambia..............mume wangu sisi wanawake tunapenda kuamini kuwa wanaume zetu ni superman tunasahau kuwa wameumwa na nyama kama sisi wanawake............jamaa anadai mkewe akaendelea kuwa...........eti maelezo ya mumewe yamem-put off na yanamfanya amuone mumewe kuwa yuko weak jambo ambalo linamfanya eti mke huyo amuone mumewe unatractive......................jamaa anadai kuwa wife anadai wanawake wote wanapenda kuamini kuwa wanaume zao wananguvu kuliko wao(wanawake) lakini eti wife wa jamaa anadai yeye havuti sigara lakini anaamini hata akivutwa sigara nzima hatabebwa kama mumewe alivyobebwa baada ya kuvuta pafu mbili...............................Jamaa anadai mkewe amemuomba asimuhadithia tena story za aina hii..................Jamaa naye anadai maneno ya mkewe yamejaa dharau......................

Wakulu hii kesi nimeiletwa kwenu nisikie na nyinyi mna lipi lakusema.......................................!

....safi kabisa, huyo mke ana busara sana....

huyo jamaa angeendelea huenda angesema hata yai wamemvunjia. Mwambie best wako afiche madhaifu yake,
Ebo!
 
kuna dada niliwahi kumsikia akisema kwamba...............kuna machafu mengi amewahi kuyafanya ujanani.............lkn kamwe hawezi kumuhadithia mchumba wake sababu anajua hata huyo mchumba wake anamwambia vitu vile vinavyofanya aonekane mwanaume wa maana................ila mim nadhan bora mke wa jamaa alipoomba asihadithiwe story za aina hii sababu jamaa ameshajua kuwa zinam-put off wife............hatari ninayoiona ni mume kuanza kudanganya kuwa anaweza kufanya hata vitu ambavyo haviwezi ili wife amuone superman........................
Ya ni kweli kabisa, ila hakuwa na haja ya kuleta madharau ya kiasi kile, unamwambia mtu kiakili, yaani ujumbe unafika bila kumwumiza hisia zake, kwa mfano una mpenzi wako anakikwapa, huwezi mwambia hupendi watu wanaonuka kikwapa, bali utajitahidi kumnunulia zawadi za deodorant, na kumwambia unapenda harufu ya manukato yale akipaka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom