Mke anashinda Kanisani !!

Hizi dini za kisasa ni za kuangalia sana, hakuna lolote huko zaidi ya kufarakanisha familia na ndoa!Hakuna dini isiyopenda kuona wawili wakiishi kwa amani na upendo!

Huyo mwanamke aambiwe tu achague moja dini yake au familia yake!
 
Fixed Point nimeipenda hii
"
ARE YOU AND YOUR SPOUSE SPEAKING THE SAME LOVE LANGUAGE?
A%20S-heart-2.gif
"

Jamani bahati mbaya kama yeye aimba taarab mimi bolingo inakuaje?
 
Hizi dini za kisasa ni za kuangalia sana, hakuna lolote huko zaidi ya kufarakanisha familia na ndoa!Hakuna dini isiyopenda kuona wawili wakiishi kwa amani na upendo!

Huyo mwanamke aambiwe tu achague moja dini yake au familia yake!

Sidhani kama dini ndio ya kulaumiwa ... hivi kuna dini za kisasa?dont think so... but i think she should set her priorities and time management is the key to her problem... the only problem i c there is if she will realize that whatever she is putting herself into could affect ppl around her...

I have a living example of this kind of woman and tell you what... she never ever think that this is a problem... she goes to the Fatwa (in the Islamic faith is a religious opinion concerning Islamic law ) everyday or 5 days a week. at the same time she neglects her children and husband... she has a teenager boy who started smoking and do all that bad boys stuff... while she is busy attending these Fatwa... once when she started preaching me on something, I told her oow come on at least I know what is going on in my own house.....
 
Hii tabia ya watu "kushikwa vibaya" na imani imekuwa kubwa sana siku hizi jamaa ikiwezekana ampeleke mkewe wa wataalam wa magonjwa ya akili(hasa Msongo)
Muhimbili. Tatitzo linatibika, kuna watu nawafahamu wamefunguliwa kutoka kwenye hali hiyo.

yaani hata wewe uliyekuwa umejujuliwa unaongea hivi, haujakoma tu, nilifikiri walikutia adabu kidogo pengine umkumbuke Mungu aliyekuumba, badala yake unawaponda wale wanaomtafuta Mungu.
 
Ubungoubungo nakuheshimu ! Sasa uliyoyasema yoote ni kweli kabisa. Swali linakuja kumheshimu Mungu ni kumdharau mumeo? Ili Mungu adhihirike kwa mumewe lazima matendo yake, tabia, na kila kitu kwanza mumewe alidhike navyo. Na kama ni otherwise sie Mungu huyo ni PEPO. Siku hizi mambo mengi yahee usikute kapata kajamaa huko kanamchelewesha anasingizia kanisa. Angekuwa Mungu huyo mume asinge complain maana kwanza roho ya Mungu ingeanza na mume kumuweka sawa ange feel confortable sana na asigelalamika.
 
Mh...

Mungu ni mmoja mwenye nafsi tatu nae alituumba kwa mfano wake, akatuagiza tuyashike na kuyatenda yale yaliyo mema..na tukijua wajibu wetu na kuufuata.

Tafsiri ya maandiko katika Kitabu cha Mungu ni pana na wawezao kutafsri ndio waliofunuliwa kuwavuta hata wale ambao imani na matendo yao yanadhirishwa kwa mambo ya mwili na roho.

Pengine dini zetu zinatafiriwa kama "Bangi" ambayo ikikulevya sana, waweza kuchangaya ya "Kaisari" na yale ya "MUNGU"...Ipo mistari inaonya:

"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamejivalia kanzu ndefu na kusalimiwa na watu kwa heshima sokoni; hupenda kuketi mahali pa heshima katika masunagogi, na kuchukua nafasi za heshima katika karamu. Huwanyonya wajane huku wakijisingizia kusali sala ndefu. Siku ya hukumu watapata adhabu kali!"

"Basi mtu akiwaambieni, Tazama, Kristo yupo hapa! au Yupo pale! msimsadiki. Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo, watafanya ishara na maajabu, ili kuwapotosha wateule wa Mungu, kama ikiwezekana. Lakini ninyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea"

Je, yatupasa kushika imani ipi, ya Kristu au ya Madhehebu na Makanisa???..

hilo ndo kosa kubwa sana la kutokuelewa Biblia, umesema WATAWAAMBIA TAZAMA KRISTO YUKO HUKU AU KULE MSIWAAMINI, wewe umeshaweka kuwa alikuwa anaongelea madhehebu. kumbuka alisema, kama vile umeme uwakavo mashariki ukaonekana magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa mwana wa Mungu, hakuwa anaongelea madhehebu hapa kuwa wale wanaohama madhehebu yasiyo ya kimungu wanakosea, alikuwa anaongelea mazingira. KUNA MTU ALISHAWAHI KUJA KWAKO KUKUAMBIA YESU AMESHASHUKA NA SASA YUKO KIMARA? AU YUKO MBAGALA, AU YESU AMESHASHUKA LEO SIKU YA MWISHO YUKO MASAKI, AU MBEZI BEACH, hii ndo ilikuwa maana yake.

ukweli unabaki palepale, kama ukiona dhehebu fulani halina njia ya kimungu, hama haraka kwasababu utakuwa unapoteza muda. madhehebu karibia yote yalivyokuwa yanaanzishwa yalikuwa na mkono wa Mungu, sasa kadiri muda unavyozidi kwenda, shetani huwa anayameng'enyua kidogokidogo baadaye anaharibu mfumo mzima wa kumwabudu Mungu, kiburi, kuabudu pesa na sanamu vinaingia, na Mungu akishaona hivyo tu ya kwamba watu sasa hawamwabudu yeye wanaabudu wafu, wanaabudu wanaowaita watakatifu, wanaabudu kupitia mwanadamu badala ya kupitia kwa Yesu, wanaombea wafu, wana kiburi cha fesha, Mungu huwa anaondoka anakwenda kwa mwanadamu mwingine ambaye atamheshimu, hivyo lile dhehebu ya kwanza linabaki kopo tu, hamna Mungu wala nini, Mungu ameshaondoka. HIVYO HAUWEZI KUWA NA AKILI TIMAMU KUSEMA KUWA UTABAKI KWENYE DHEHEBU LAKO HILIHILO MILELe, wakati pengine halina hata Mungu. utapoteza muda. ushauri ni kwamba, kama ukiona dhehebu halina Mungu, umefunguka macho ukaona hivyo, kimbia, jua hapo kuna shetani. kama hakuna Mungu basi kuna mkono wa shetani. ushauri wa bure.
 
Ubungoubungo nakuheshimu ! Sasa uliyoyasema yoote ni kweli kabisa. Swali linakuja kumheshimu Mungu ni kumdharau mumeo? Ili Mungu adhihirike kwa mumewe lazima matendo yake, tabia, na kila kitu kwanza mumewe alidhike navyo. Na kama ni otherwise sie Mungu huyo ni PEPO. Siku hizi mambo mengi yahee usikute kapata kajamaa huko kanamchelewesha anasingizia kanisa. Angekuwa Mungu huyo mume asinge complain maana kwanza roho ya Mungu ingeanza na mume kumuweka sawa ange feel confortable sana na asigelalamika.

nitamsaidia kujibu. ni vyema na lazima kumheshimu mume, lakini hauwezi kumheshimu mume katika kila kitu. jirani yangu ana tatizo la ndoa kama hiyo, mkewe anasali efatha kule mwenge. huyo jamaa kuna siku anampiga mkewe kwa sasa amemvunja mkono, kisa nini? mkewe kaamua kwenda kuokoka, yeye ana magari, ana mabiashara, kazi zao zoote anazifanya kwa madawa. akienda kwa mganga, anatakiwa aende na mkewe kama dawa wanywe wote wawili. mganga kamwambia kuwa, amshikilie huyo mkewe kwasababu mkewe ana nyota nzuri, akimuacha mkewe na mali zitaondoka. hivyo inashindikana kwake kumwacha, inashindikana kwake kumpiga juju ili aoe mwingine, kilichobaki ni kumpiga tu kila mara na mama anaishia hospitali na mkono kuvunjika. MAMA KAGOMA, HAKUNA CHA DAWA WALA MGANGA, BORA NIFE. kuna mazingira mengi sana wanawake wanakutanana nayo kwa kukusaidia, hasa kwa maisha ya Tz ambayo kati ya watu kumi, tisa walishawai kwenda kwa mganga. uchawi unaabudiwa sana tz. HIVYO HAUWEZI KUMTII MUMEO KATIKA KILA KITU, ukiona anasema kitu cha maana mtii, kama hasemi kitu cha maana hautakiwi kumtii. akisema kitu ambacho ni kinyume na Mungu usimtii, mtii Mungu kwanza aliyekuumba. sisi sote tumeoa pia. enyi wanawake, msiwatii wanaume zenu kuliko kumtii Mungu, siku ya mwisho kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. wanawake wengi ni wadhaifu wa maamuzi, akiambiwa na mumewe asiende kanisani, anakubali, akiambiwa lazima anywe dawa ya ukoo anakubali kwasababu anamwogopa mumewe sio kwamba anamheshimu, akiambiwa tigo anakubali kwasawababu anaogopa kuachwa, akiambiwa chochote anafanya kwasababu anaogopa sio kwamba anamheshimu au kumtii. hivyo inakuwa sio ndoa tena, ni kamanda wa vita ndani ya nyumba, katili mfalme bosss ndani ya nyumba, wenzie wote hawana haki yoyote.

enyi wanaume, kumbukeni kuwa, imeandikwa lazima tuwapende wake zetu, wao wakitutii sisi tunawapenda. hivyo kumpenda mtu ni to step into his shoes...jiweke kwenye nafasi yake. unatakiwa umfanyie mkeo kile ambacho wewe ungependa ufanyiwe, mpende jiran yako kama nafsi yako. kile ambacho wewe ukifanyiwa huwa unajisikia vibaya, usimfanyie mkeo. hii ndio sheria. I hope ume gain kitu fulani hapa.
 
Dunia imekwisha. Huyo mke sidhani kama ana busara. Ninamshauri huyo bwana (mumewe) aonane na mchungaji amweleze tatizo analoliona katika ndoa yake kabla ya kufanya uamuzi wowote.
 
Sio cha dini wala nini, kuna tatizo ktk ndoa utasikia mmoja anatafuta kwa kwenda kujipozea, kuna wanaoenda kwenye pombe kama huyo mama aliyeua watoto Moshi, kuna wanaoenda kwa wazazi wao, kuna wengine kwa mashoga, mwingine kazini na visafari visivyoisha mradi hayupo hapo home. Kwa hiyo usisikilize upande mmoja: nini kiliwavutia wakakaa pamoja? nadhani kimekosekana sasa na pengine huyo mume akiambiwa haoni kuwa ni tatizo maana mara nyingi wanawake ni wavumilivu sana. Bora huyo anaenda kanisani, Mungu atamsaidia. Mume kama anajali kwanini kwa upole asimuulize anakwend kuombea nini na wakaomba pamoja nyumbani? badala yake hata akiimba tu nyimbo hapo home zinamkera hapo kuna tatizo!
 
Jamani tusichanganye mambo - YESU SIO DINI WALA MADHEHEBU - DINI, MADHEHEBU ni mambo ya wanadamu - SWALA NI YESU - MWOKOZI WA ULIMWENGU - Huyu Mama amepata PERSONAL ENCOUNTER WITH JESUS - kuna tofauti kubwa sana ya kuomba nyumbani na kuomba kanisani. Huyu HUSBAND WAKE - WAKATI MKEWE ANAENDA KANISANI YEYE ANAFANYA NINI?? JAMANI TUFIKE MAHALI TUACHANE NA MFUMO-DUME - INGEKUWA MWANAUME ANASHINDA KANISANI AKIABUDU - MKE ANGELALAMIKA? huyu mwanaume ajue kabisa kuwa USALAMA WA NDOA YAKE NI YEYE KUWA KWENYE MSTARI - AZIKUBALI PAMBIO NA YEYE AIMBE PIA; AENDE KANISANI BADALA YA KWENDA BAR AU KUCHEZA BAO - TENNIS - whatever - MKEWE INTEREST YAKE NI MAMBO YA ROHONI na YEYE NI MAMBO YA MWILINI - NDIO MAANA HAWEZI KUMWELEWA MKEWE - AINGIE ROHONI NDIO WATAELEWANA
mwili hushinda na roho - mwili ni audui kwa mambo ya rohoni - MWILI unapenda - kula (no fasting) usingizi (no praying) wivu, ugomvi, hasira, uasherati, uzinzi (no holiness) - ila tunda la Roho ni AMANI, UVUMILIVU, UTU WEMA, UPOLE, KIASI etc. KAMA ILIVYOANDIKWA KWENYE - Wagalatia 5:22 - hivyo AKILI ZETU NA ZIFUNGULIWE TUWEZE KUMSAIDIA HUYU MWANAUME ANAYELALAMIKA MKEWE KUSHINDA KANISANI - TENA FOR A CERTAIN PERIOD
 
hilo ndo kosa kubwa sana la kutokuelewa Biblia, umesema WATAWAAMBIA TAZAMA KRISTO YUKO HUKU AU KULE MSIWAAMINI, wewe umeshaweka kuwa alikuwa anaongelea madhehebu. kumbuka alisema, kama vile umeme uwakavo mashariki ukaonekana magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa mwana wa Mungu, hakuwa anaongelea madhehebu hapa kuwa wale wanaohama madhehebu yasiyo ya kimungu wanakosea, alikuwa anaongelea mazingira. KUNA MTU ALISHAWAHI KUJA KWAKO KUKUAMBIA YESU AMESHASHUKA NA SASA YUKO KIMARA? AU YUKO MBAGALA, AU YESU AMESHASHUKA LEO SIKU YA MWISHO YUKO MASAKI, AU MBEZI BEACH, hii ndo ilikuwa maana yake.

ukweli unabaki palepale, kama ukiona dhehebu fulani halina njia ya kimungu, hama haraka kwasababu utakuwa unapoteza muda. madhehebu karibia yote yalivyokuwa yanaanzishwa yalikuwa na mkono wa Mungu, sasa kadiri muda unavyozidi kwenda, shetani huwa anayameng'enyua kidogokidogo baadaye anaharibu mfumo mzima wa kumwabudu Mungu, kiburi, kuabudu pesa na sanamu vinaingia, na Mungu akishaona hivyo tu ya kwamba watu sasa hawamwabudu yeye wanaabudu wafu, wanaabudu wanaowaita watakatifu, wanaabudu kupitia mwanadamu badala ya kupitia kwa Yesu, wanaombea wafu, wana kiburi cha fesha, Mungu huwa anaondoka anakwenda kwa mwanadamu mwingine ambaye atamheshimu, hivyo lile dhehebu ya kwanza linabaki kopo tu, hamna Mungu wala nini, Mungu ameshaondoka. HIVYO HAUWEZI KUWA NA AKILI TIMAMU KUSEMA KUWA UTABAKI KWENYE DHEHEBU LAKO HILIHILO MILELe, wakati pengine halina hata Mungu. utapoteza muda. ushauri ni kwamba, kama ukiona dhehebu halina Mungu, umefunguka macho ukaona hivyo, kimbia, jua hapo kuna shetani. kama hakuna Mungu basi kuna mkono wa shetani. ushauri wa bure.

hII BIBLIA NADHANI TUNAITAFSIRI TOFAUTI SANA.



NI DINI GANI INAYOFUNDISHA KUJUA MUNGU YUPO HAPA AU PALE KAMA SI YA KRISTO?? NA UTAITAMBUAJE HIYO KAMA SI IMANI YAKO AMBAYO INAONGOZWA PIA NA UTASHI WA KUJUA KUSALI SI LAZIMA UKASHINDE KANISANI UKIFOKA NA KUPWAYUKA KAMA MWENDA WAZIMU SIKU NZIMA NA BADAE UKAMULIWE KWA KUTOA MAPATO YA KAZI YA MIKONO YAKO UKAMPE MTU AMBAE ANAISHI MAISHA MAZURI KWA JASHO LA WENGINE ETI KISA YEYE NDIE ANAYEJUA KUTAFSIRI NENO LA MUNGU NA KUIONGOZA ROHO YAKO (BABA NA MAMA MCHUNGANI)??

NI DINI GANI INAYOTUFUNDISHA TUSHINDWE PENGINE KUTIMIZA WAJIBU MWINGINE WA KIDUNIA??

kWA NINI BASI NA TUSISALI MAJUMBANI MWETU INAPOFIKIA KUONA MAKANISA NA MADHEHEBU YOTE YAMEPOTOKA NA HAYANA MUNGU??

IKIWA TUNAENDA KANISANI KWA KUMTAFUTA MUNGU, JE, YUPO KIONGOZI YEYOTE WA DINI AU DHEHEBU LINALOONGOZWA KWA KUFUATA MISTARI YA BIBILIA (IWE HATA KWA KUPOTOSHA) ANAYEWEZA KUSIMAMA MBELE YA WAUMINI WAKE AKASAME KUWA YEYE NI NABIII WA UWONGO NA KWAMBA KANISA LAKE HALINA MUNGU KAMA HATAKUWA PUNGUANI ???

WOTE WAKISEMA WAO NDO KANISA LA KWELI, UKIWA NA UTASHI SAHIHI WA KIROHO HUWEZI KUONA KUWA KANISA AU DHEHEBU NDILO LITAKUONGOZA KATIKA KUMJUA MUNGU, KWANI KANISA NI KRISTO ALIYE MOYONI MWAKO NA NDIE KIONGOZI WA UKWELI KATIKA ROHO NA NI NJIA YA PEKEE YA KUEPUKA KUHANGAISHWA NA BUSARA ZA WANADAMU AMBAZO PENGINE ZIMEJAA MANENO MATAMU YA UPOTOSHAJI KULIKO ASALI !.

kUNA HAJA YEYOTE YA KUZUNGUKA HUKU NA KULE KWA HISIA LABDA HAPA AU PALE NDIPO KWENYE MUNGU??

TUNAKOSA NINI TUKISALI KIMOYO MOYO, TUKIONGOZWA NA ROHO NA KUMWOMBA MUNGU HAYA TUKIWA NA FAMILIA ZETU??
 
inawezekana kabisa mchungaji akawa anatembea na huyo mwanamke......
wachungaji hawa wa makanisa yanayoibuka kila siku kwa kupenda wanawake hao.

jaribu kutoa mchango wa maarifa kidogo, utakao weza kumsaidia mhusika,

swala la mahusiano ni personal sana katika maisha ya mwanadamu, hivyo
onesha umakini juu ya nini unachangia na si kuropoka tu...
 
hII BIBLIA NADHANI TUNAITAFSIRI TOFAUTI SANA.



NI DINI GANI INAYOFUNDISHA KUJUA MUNGU YUPO HAPA AU PALE KAMA SI YA KRISTO?? NA UTAITAMBUAJE HIYO KAMA SI IMANI YAKO AMBAYO INAONGOZWA PIA NA UTASHI WA KUJUA KUSALI SI LAZIMA UKASHINDE KANISANI UKIFOKA NA KUPWAYUKA KAMA MWENDA WAZIMU SIKU NZIMA NA BADAE UKAMULIWE KWA KUTOA MAPATO YA KAZI YA MIKONO YAKO UKAMPE MTU AMBAE ANAISHI MAISHA MAZURI KWA JASHO LA WENGINE ETI KISA YEYE NDIE ANAYEJUA KUTAFSIRI NENO LA MUNGU NA KUIONGOZA ROHO YAKO (BABA NA MAMA MCHUNGANI)??

NI DINI GANI INAYOTUFUNDISHA TUSHINDWE PENGINE KUTIMIZA WAJIBU MWINGINE WA KIDUNIA??

kWA NINI BASI NA TUSISALI MAJUMBANI MWETU INAPOFIKIA KUONA MAKANISA NA MADHEHEBU YOTE YAMEPOTOKA NA HAYANA MUNGU??

IKIWA TUNAENDA KANISANI KWA KUMTAFUTA MUNGU, JE, YUPO KIONGOZI YEYOTE WA DINI AU DHEHEBU LINALOONGOZWA KWA KUFUATA MISTARI YA BIBILIA (IWE HATA KWA KUPOTOSHA) ANAYEWEZA KUSIMAMA MBELE YA WAUMINI WAKE AKASAME KUWA YEYE NI NABIII WA UWONGO NA KWAMBA KANISA LAKE HALINA MUNGU KAMA HATAKUWA PUNGUANI ???

WOTE WAKISEMA WAO NDO KANISA LA KWELI, UKIWA NA UTASHI SAHIHI WA KIROHO HUWEZI KUONA KUWA KANISA AU DHEHEBU NDILO LITAKUONGOZA KATIKA KUMJUA MUNGU, KWANI KANISA NI KRISTO ALIYE MOYONI MWAKO NA NDIE KIONGOZI WA UKWELI KATIKA ROHO NA NI NJIA YA PEKEE YA KUEPUKA KUHANGAISHWA NA BUSARA ZA WANADAMU AMBAZO PENGINE ZIMEJAA MANENO MATAMU YA UPOTOSHAJI KULIKO ASALI !.

kUNA HAJA YEYOTE YA KUZUNGUKA HUKU NA KULE KWA HISIA LABDA HAPA AU PALE NDIPO KWENYE MUNGU??

TUNAKOSA NINI TUKISALI KIMOYO MOYO, TUKIONGOZWA NA ROHO NA KUMWOMBA MUNGU HAYA TUKIWA NA FAMILIA ZETU??

Bwana mdogo, nilikuwa nakujibu swali tu, kwasababu niliona wewe haujaelewa sehemu fulani hivi ya Bible inaposema ya kuwa, siku za mwisho watatokea makristo wa uongo, ya kwamba, mkisiikia yuko jangwani msiende, mkisikia yuko huku msiende, kama vile umeme uwakavyo mashariki ukaonekana magharibi ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa mwana wa Adam. nilikuwa nakusaidia kukuelewesha uelewe kuwa hii haikuwa inamaanisha madhehebu, ilikuwa inamaanisha mazingira physically kabisa, mashariki mangaribi,kaskazini kusini, jangwani, nyikani etc. kuna watu wachache wameshajitokeza kusema wao ni Yesu ameshuka kulichukua kanisa, lakini wanapotea tu, ni shetani. Yesu alikuwa anamaanisha kuwa, siku hiyo Yeye atakapokuja kulichukua kanisa lake, kufumba na kufumbua watu woote duniani watasikia parapanda yake, aliyeko marekani atasikia muda uleule na aliyeko ubungo na mbagala. ndio maana alisema umeme ukiwaka mashariki muda huohuo unaonekana magharibi, akimaanisha kuwa, atakapokuja kulichukua kanisa lake tu, muda huo hakuna cha kuulizauliza, watu wote duniani watakuwa wameshajua kilichotokea kwa wakati mmoja, sio kwamba wamarekani au waarabu wajue kuwa Yesu amekuja halafu wale walioko moshi na kenya wasijue, no, ndio maelezo hayo Yesu aliyokuwa anasema.

nikija kwenye swala lingine, ni wazi kwamba, madhehebu ni NGO tu ambazo watu wanaanzisha, na they are registered in the same status kama non-govermental organisations. Cha muhimu katika madhehebu ni msingi wake, msingi ukiwa umejengwa kwenye mabua na mchanga, icho kitakuwa ni kiti cha shetani. msingi ukiwa umejengwa kwenye mwamba ambao ni Yesu Kristo aliye Neno la Mungu kulingana na Yohana 1, basi Yesu mwenyewe atakuwa pamoja na hil dhehebu. kwasababu hii, Mungu huwa anaangalia wako wapi wawili watatu waliokusanyika kwa Jina langu ili mimi niwe papohapo katikati yao, akiona kuwa watu wamekusanyika kwa kufuata neno lake, atashuka na atakuwa pamoja nao, atakuwa Mungu wao na atafanya mambo makubwa katika maisha yao. akiona watu wamekusanyika katika michanganyo, kuabudu masanamu, kuabudu watu, kuombea wafu wakati Bible inakataza, hashuki hapo, haji ng'oooo.

madhehebu mengi duniani yalianzishwa yakiwa na Mungu, angalia RC lilianza vizuri sana na lilikuwa na Mungu, lakini selikali ya kirumi ilivyolichanganya na siasa, wakaweka hekima za kibinadamu badala ya uongozi wa Roho Mtakatifu, walivyoanza kukwapua pesa kwaajiili ya msamaha wa dhambi, kukwapua pesa kwaajili ya kujenga St.Peter kule vatican, walipoanza kutoza waumini pesa, na kufanya mambo mengi kwa kutumia akili za wanadamu, Mungu akaondoka. Mungu akaonekana kwa watu wengine kama kina Martin Luther ambao mwanzoni walikuwa watu wa Mungu, lakini baadaye wao pia kutokana na udhaifu wa mwanadamu, adui akaingia, ikawa dini isiyoongozwa na Roho mtakatifu, matokeo yake Mungu akaondoka kwasababu hawakuona kuwa yeye ni wa muhimu. miaka ya arobaini hadi sitini kule Marekani kwenye mtaa unaoitwa Azuza street, watu wa Mungu walipokuwa wakimwabudu, ndo kwa mara nyingine zaidi ya miaka mianne na ushee, Roho Mtakatifu aliposhuka, uamusho wa kanisa lililokuwa limejichanganya na siasa na akili/hekima za kibinadamu likaanza kuchipua kwasababu gani? kwasababu Roho Mtakatifu alihusishwa kwenye ibada zao.

walakinni yeyote yule asiyekuwa na huyo Roho si wake, ukiona hauna Roho mtakatifu wewe si mtu wa Mungu. ukiona unaabudu sehemu kavu, isiyokuwa na udhihirisho wa Roho mtakatifu hapo kimbia hamna kitu. Mungu anajidhihirisha kwetu kupitia Roho mtakatifu, ndo Roho yake hiyo. Yesu alisema siwezi kuwaacha yatima, Roho mtakatifu alikuwa ili tusiwe yatima, makanisa mengi yana majina lakini ni yatima, hayana msaidizi kabisa.

Kitu cha muhimu kukushauri ni hikii, na wote mtakaosoma. UKIONA UNAFANYA JAMBO LOLOTE LILE BILA UONGOZI WA ROHO MTAKATIFU, hili jambo mwisho wake ni uharibifu tu. hata kama Mungu ametupatia utashi na akili kama ndugu anavyosema hapa, lakini hakika yake hatuwezi peke yetu kwasababu hatujui yaliyoko mbele yetu, ndio maana ukiwa na Mungu Roho wake anatuongoza kufanya mambo mengi kwasababu anajua yaliyoko mbele yetu. usijiamini sana ukaona wewe unaweza lolote ndugu yangu, hauwezi chochote, ni neema ya Mungu tu hata kuongea hivyo. unahitaji msaada wa Mungu 100%, usifikiri kwasababu ya elimu yako, kwasababu ya chochote kile ulichonacho, ukafikiri wewe una hekima, utashi sana, au akili sana. AJISIFUYE NA AJISIFU KWAKUWA ANAMFAHAMU MUNGU. mwanadamu akiwa na hekima nyingiiiiiii, hata mwisho, bado hajafikia hata kunusa tu hekima na ujuzi wa Mungu. we are helpless, ile Mungu ametupatia msaidisi Roho Mtakatifu.

kwanini naongea yote haya, kwasababu makanisa mengi sana tz hayana uongozi wa Roho mtakatifu. mtu anakwambia tuombe halafu anaanza kusoma kitabu. ibada zimekauka haziongozwi na Roho. Yesu alisema siku zinakuja ambazo wamwabuduo halisi watamwabudu yeye katika roho na kweli kwasababu Mungu ni Roho nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika Roho na kweli. kumwabudu Mungu bila kumshirikisha Roho mtakatifu ni bure. mahubiri yasiyokuwa na uhuisho wa Roho mtakatifu ni kande na mawe magumu hayana afya, ukihubiri hubiri katika uongozi wa Roho, ukiomba omba kwa Roho, ukifanya chochote cha kimungu fanya kwa uongozi wa Roho. nitaishia hapa nisije kumaliza ukurasa. but I have so much things to tell you my brother. God bless you, haleluya to the Lamb of God!
 
bwana mdogo, nilikuwa nakujibu swali tu, kwasababu niliona wewe haujaelewa sehemu fulani hivi ya bible inaposema ya kuwa, siku za mwisho watatokea makristo wa uongo, ya kwamba, mkisiikia yuko jangwani msiende, mkisikia yuko huku msiende, kama vile umeme uwakavyo mashariki ukaonekana magharibi ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa mwana wa adam. Nilikuwa nakusaidia kukuelewesha uelewe kuwa hii haikuwa inamaanisha madhehebu, ilikuwa inamaanisha mazingira physically kabisa, mashariki mangaribi,kaskazini kusini, jangwani, nyikani etc. Kuna watu wachache wameshajitokeza kusema wao ni yesu ameshuka kulichukua kanisa, lakini wanapotea tu, ni shetani. Yesu alikuwa anamaanisha kuwa, siku hiyo yeye atakapokuja kulichukua kanisa lake, kufumba na kufumbua watu woote duniani watasikia parapanda yake, aliyeko marekani atasikia muda uleule na aliyeko ubungo na mbagala. Ndio maana alisema umeme ukiwaka mashariki muda huohuo unaonekana magharibi, akimaanisha kuwa, atakapokuja kulichukua kanisa lake tu, muda huo hakuna cha kuulizauliza, watu wote duniani watakuwa wameshajua kilichotokea kwa wakati mmoja, sio kwamba wamarekani au waarabu wajue kuwa yesu amekuja halafu wale walioko moshi na kenya wasijue, no, ndio maelezo hayo yesu aliyokuwa anasema.

Nikija kwenye swala lingine, ni wazi kwamba, madhehebu ni ngo tu ambazo watu wanaanzisha, na they are registered in the same status kama non-govermental organisations. Cha muhimu katika madhehebu ni msingi wake, msingi ukiwa umejengwa kwenye mabua na mchanga, icho kitakuwa ni kiti cha shetani. Msingi ukiwa umejengwa kwenye mwamba ambao ni yesu kristo aliye neno la mungu kulingana na yohana 1, basi yesu mwenyewe atakuwa pamoja na hil dhehebu. Kwasababu hii, mungu huwa anaangalia wako wapi wawili watatu waliokusanyika kwa jina langu ili mimi niwe papohapo katikati yao, akiona kuwa watu wamekusanyika kwa kufuata neno lake, atashuka na atakuwa pamoja nao, atakuwa mungu wao na atafanya mambo makubwa katika maisha yao. Akiona watu wamekusanyika katika michanganyo, kuabudu masanamu, kuabudu watu, kuombea watu wakati bible inakataza, hashuki hapo, haji ng'oooo.

Madhehebu mengi duniani yalianzishwa yakiwa na mungu, angalia rc lilianza vizuri sana na lilikuwa na mungu, lakini selikali ya kirumi ilivyolichanganya na siasa, wakaweka hekima za kibinadamu badala ya uongozi wa roho mtakatifu, walivyoanza kukwapua pesa kwaajiili ya msamaha wa dhambi, kukwapua pesa kwaajili ya kujenga st.peter kule vatican, walipoanza kutoza waumini pesa, na kufanya mambo mengi kwa kutumia akili za wanadamu, mungu akaondoka. Mungu akaonekana kwa watu wengine kama kina martin luther ambao mwanzoni walikuwa watu wa mungu, lakini baadaye wao pia kutokana na udhaifu wa mwanadamu, adui akaingia, ikawa dini isiyoongozwa na roho mtakatifu, matokeo yake mungu akaondoka kwasababu hawakuona kuwa yeye ni wa muhimu. Miaka ya arobaini hadi sitini kule marekani kwenye mtaa unaoitwa azuza street, watu wa mungu walipokuwa wakimwabudu, ndo kwa mara nyingine zaidi ya miaka mianne na ushee, roho mtakatifu aliposhuka, uamusho wa kanisa lililokuwa limejichanganya na siasa na akili/hekima za kibinadamu likaanza kuchipua kwasababu gani? Kwasababu roho mtakatifu alihusishwa kwenye ibada zao.

Walakinni yeyote yule asiyekuwa na huyo roho si wake, ukiona hauna roho mtakatifu wewe si mtu wa mungu. Ukiona unaabudu sehemu kavu, isiyokuwa na udhihirisho wa roho mtakatifu hapo kimbia hamna kitu. Mungu anajidhihirisha kwetu kupitia roho mtakatifu, ndo roho yake hiyo. Yesu alisema siwezi kuwaacha yatima, roho mtakatifu alikuwa ili tusiwe yatima, makanisa mengi yana majina lakini ni yatima, hayana msaidizi kabisa.

Kitu cha muhimu kukushauri ni hikii, na wote mtakaosoma. Ukiona unafanya jambo lolote lile bila uongozi wa roho mtakatifu, hili jambo mwisho wake ni uharibifu tu. Hata kama mungu ametupatia utashi na akili kama ndugu anavyosema hapa, lakini hakika yake hatuwezi peke yetu kwasababu hatujui yaliyoko mbele yetu, ndio maana ukiwa na mungu roho wake anatuongoza kufanya mambo mengi kwasababu anajua yaliyoko mbele yetu. Usijiamini sana ukaona wewe unaweza lolote ndugu yangu, hauwezi chochote, ni neema ya mungu tu hata kuongea hivyo. Unahitaji msaada wa mungu 100%, usifikiri kwasababu ya elimu yako, kwasababu ya chochote kile ulichonacho, ukafikiri wewe una hekima, utashi sana, au akili sana. Ajisifuye na ajisifu kwakuwa anamfahamu mungu. Mwanadamu akiwa na hekima nyingiiiiiii, hata mwisho, bado hajafikia hata kunusa tu hekima na ujuzi wa mungu. We are helpless, ile mungu ametupatia msaidisi roho mtakatifu.

Kwanini naongea yote haya, kwasababu makanisa mengi sana tz hayana uongozi wa roho mtakatifu. Mtu anakwambia tuombe halafu anaanza kusoma kitabu. Ibada zimekauka haziongozwi na roho. Yesu alisema siku zinakuja ambazo wamwabuduo halisi watamwabudu yeye katika roho na kweli kwasababu mungu ni roho nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika roho na kweli. Kumwabudu mungu bila kumshirikisha roho mtakatifu ni bure. Mahubiri yasiyokuwa na uhuisho wa roho mtakatifu ni kande na mawe magumu hayana afya, ukihubiri hubiri katika uongozi wa roho, ukiomba omba kwa roho, ukifanya chochote cha kimungu fanya kwa uongozi wa roho. Nitaishia hapa nisije kumaliza ukurasa. But i have so much things to tell you my brother. God bless you, haleluya to the lamb of god!

ameni mtu wa mungu nimekupata!.
 
Mtafute uyo mchungaji kwanza umuwashe mangumi kidogo,,. mafunzo gani hayo anatoa

hapana, huo sio ushauri mzuri, anaweza kumtafuta huyo mchungaji akampiga mangumi, muda kidogo tu mgongo wake ukipinda, akipigwa na gonjwa la ajabu, atamtafuta mchungaji huyohuyo ili amwombeee, hicho ndo kichekesho. ulishawai kumpiga mtumishi wa Mungu uka survive? have you ever tried to do that?, angalia kina Jezebel kwenye kitabu cha wafalme. Neno la Mungu linasema, washindanao na Bwana watapondwa kabisa, pia Mungu akiwa upande wetu hakuna aliye juu yetu, atakaye tugusa anagusa mboni ya Jicho la Mungu, ukigusa mboni ya Jicho la Mungu, kibao utakachopata ni aibu ambayo hautasahau. kwa kifupi, Usije hata siku moja ukajaribu kumpiga au kumtukana face to face mtumishi wa Mungu, utajilaumu badaye, Mungu huwa anawapigania watumishi wake sana. KUNA PASTA MMOJA HAPO DAR ANA KANISA KUBWA SANA, SIKU MOJA KUNA MWANAUME FULANI ALIMFUATA KWASABABU MKE WAKE AMEBADILI DHEHEBU, akamfuata pasta wa mke wake, akaanza kumtukana matusi ya ajabu pale pale kanisani, akijua ya kuwa mchungaji ni mtu wa Mungu hawezi kupigana wala nini. Bwana Bwana, mchungaji akashindwa kuvumilia, akamwambia ya kuwa, kama wewe unasema sisi sote hapa ni wajinga na matusi mengine, basi uhai na ukutoke. Jamaa aliondoka, kesho yake walienda kumzika laivu. ameshakufa kwa neno tu. Mtu wa Mungu anapoongea, maneno yake yana mamlaka na yanaumba, ndio maana akukuambia utabarikiwa unabarikiwa, akikuambia utalaaniwa unalaaniwa. Yesu siku moja alipita kando ya njia akaona mtini hauna hata matunda, akaulaani ukanyauka kabisa, wanafunzi wake waliptaka kumwuliza kwani imekuwaje, aliwaambia kama mtu akiwa na imani kiasi cha chembe ya haradani aweza kuuambia mlima huu ng'oka ukatupwe baharini nao utamtii, pia alisema, yeyote aniaminiye mimi mambo yote niyafanyayo naye atayafanya, kama yesu alifufua watu, sisi tunaomwamini pia twaweza kufufua wafu, kama Yesu aliponya wagonjwa, sisi pia tunaweza kuamuru ugonjwa ukamtoka mtu, kama Yesu alinyausha hata mtini tu, sisi pia twaweza kufanya hivyo, PIA KUMBUKA, ALISEMA TWAWEZA KUFANYA HAYO YOTE, NAAM, NA ZAIDI YA HAYO, that means, kuna Mambo makubwa kuliko yale ambayo Yesu aliyafanya tunaweza kufanya sisi. Yesu ametupatia kibali cha kufana mambo ya ajabu kuliko hata yale aliyoyafanya, makubwa zaidi manake. hivyo, ukienda kwa hawa wachungaji, uwe na uhakika huyo mchungaji ni mbabaishaji, kama si mbabaishaji ni mtu wa Mungu, unaweza kurudi ukijilaumu kwanini ulienda kwa yale utakayoyapata. hawawezi kukupiga ngumi kwasababu kwetu sisi ni dhambi kupigana, ila waweza kutamka neno tu likakupata. ni ushauri kabla haujavuka mto.
 
Back
Top Bottom