SEHEMU YA KUMI NA MBILI (12)
ILIPOISHIA; Nilipoangalia saa ilikua ni saa nane usiku hakiKa niliona kama hapakuchi kabisa, kisha nikalivuta blanketi langu na kujifunika gubigubi na baada ya muda usingizi ulinipitia na nilijikuta nipo katika uwanja wa shule ya sekondari wasa lakini ajabu baba hakuwepo.
SASA ENDELEA;nilikuwepo mkutanoni na sikujua baba yuko wapi kwa wakati huo, huku hofu ikinitanda lakini nilipiga moyo konde na kuendelea kusikiliza kinachoendelea, ambapo baada ya muda alikuja mkuu ambapo wote tulipiga maguti na kusalimia kwa heshima huku tumeinamisha vichwa vyetu chini mpaka mzee huyo ambaye ndiye mkuu wa wachawi kwa ukanda wetu alipoturuhusu kuinuka.
“twambombo,vana vangu”. Aliongea mzee huyo kwa lugha ya kikabila
“twinza, baba gwetu”. (salama baba yetu) watu wote waliitikia salamu hio isipokua mimi ambaye nilikua sielewi vizuri hio lugha ya kilozi.
Baada ya salamu hio mzee huyo alikohoa kidogo kisha kuanza kuongea mambo mengi kuhusu uchawi na kuhusu chama chetu cha uchawi lakini ni kama alikua hawzi Kiswahili vizuri hivyo mambo mengi yalikua yakinipita kutokana na kuwa yakizungumzwa kwa lugha ya kikabila.
Akili yangu iliwaza hali ya baba kwa wakati huo kwani machale yalinicheza muda wote moyo wangu ulikua unaniuma sana hapo ndipo nilianza kukumbuka maneno ya baba ambayo alitoka kuniambia siku muda mfupi uliopita.
“vita ndiyo imeanza, jitahidi usitumie nguvu zako vibaya usiwanyanyase watu wala usiwe na kiburi kwani nguvu huisha taratibu na kufanya mwisho wa siku ufedheheke, na hakuna mtu yeyote atakaekua upande wako hata mimi sitakuepo kwenye fedheha yako na wewe kuwepo kwenye fedheha yangu”.
Sasa nilianza kuona kwamba maneno ya baba yakianza kutimia kwani mkuu alifunga mkutano pasipo kuzungumza jambo lolote kuhusu baba, zaidi alinipongeza kwa kafara niliyoitoa na aliniambia kwamba mizimu imefurahi sana na imeniambia nichague kitu kimoja kati ya utajiri na kuongezewa nguvu.
“sikua na yeyote wa kunishauri na mzee huyo alihitaji majibu muda huo huo, lakini kwakua nilishasikia jinsi utajiri wa kichawi ulivyo na mashariti magumu basi niliamua kuchagua nguvu”.
“kazi nzuri kijana, mizimu itakupa nguvu zaidi na utakua na uwezo wa kuona yaliyojificha kadha wa kadha”.
Aliongea mzee huyo kisha alishoosha usinga wake juu ambapo radi zilitokea kisha usinga huo akaugusisha kifuani kwangu ambapo ghafla nilianza kutetemeka, mikono na miguu vilikosa nguvu na kupelekea pia macho yangu kukosa nuru kisha nilipoteza fahamu.
Nilikuja kuzinduka nikiwa nyumbani majira ya saa kumi na moja alfajiri nikiwa nimechoka sana, moyo wangu uliniuma sana na nilijikuta nikishawishika kuingia kwenye chumba cha baba pasipo mama kujua.
Niliingia na kuukuta mwili wa baba ukiwa wa baridi sana, hakika nilishtuka sana
“ina maana baba ameshakufa?” nilijiuliza swali ambalo hapakua na mtu wa kunijibu na nisijue nini cha kufanya.
“nafsi yake imekwenda mbali sana unahitaji kufanya jitihada kabla wachawi weusi hawajaichukua, na kupelekea baba yako kupoteza maisha”.
Ghafla nilishangaa kusikia nikipewa maelekezo namna ya kufanya, sikutita kuuliza ni nani alikua akinipa maelekezo.
“nyie ni kina nani hadi mmeyajua haya yote”. Nilihoji
“sisi ni mizimu ya simangwa, tumekua tukiishi ndani ya mwili wa baba ako kwa takribani miaka ishirini sasa na tumekua tukimuongoza na kumlinda baba yako. Sasa hivi hatuna kwa kwenda kwa sababu mwili wake hauna uhai”.
Iliongea mizimu hakika nilishangaa sana
“usishangae, una muda mchache tu wa kulikamilisha jambo hili la sivyo utamkosa baba yako”.
Nilbaki nkiwa nimeduwaa tu kwani maneno waliyoniambia yalinitisha mno.
“sasa nifanyeje”. Nilihoji
“fanya tahajudi, ili uirudishe nafsi yake kupitia nafsi yako”. Iliongea mizimu lakini hata hio tahajudi nilikua siijui hivyo ilinielekeza kila kitu
“washa mishumaa kisha ondoa nguo zako na ukae chini kisha unganisha vidole vyako pamoja na miguu alafu angalia juu uwe unavuta pumzi kwa kutumia pua na kutolea mdomoni hadi utakapoona hali ya tofauti ikijitokeza, usishangae hapo ndio uta kua ukihama kwenda ulimwengu mwingine”.
Mizimu ilimaliza kunipa amaelekezo kazi ilibaki kwangu kufanya kama nilivoelekezwa, nilizivuta pumzi zangu kwa muda kama nilivoelekezwa kisha nilianza kuona hali ya ajabu ikinitokea.
Nilikua nimeganda kama barafu kisha nikaanza kujiona nikiwa eneo la makaburi ambalo tulienda na baba usiku wa kuamkia siku hiyo.
Nilifika na kuangaza huku na kule ambapo nilishangaa kumuona asia akiwa na Yule dereva bodaboda ambaye tulienda kwaajili ya kumfukua, kaburi lilikuwa wazi na jeneza lilikua juu kama tulivoliacha siku ya jana.
nilisogea taratibu huku nikinyata na kuwafanya wasiweze kuhisi chochote katika hali ya kushangaza nilimuona baba akitabasamu, nadhani alishatambua ujio wangu mahala pale.
“huyu tunamfukia na unakua ndio mwisho wake, damu yake itanisaidia kujaza kibuyu cheusi”. Yalikua ni maongezi kati ya asia ambayo niliyasikia barabara kabisa lakini sikutaka kuonesha uwepo wangu mahala pale.
“mbona kama nasikia harufu ya udi maeneo haya?”. Aliongea dereva bodaboda ambapo sikutaka kuchelewa, nilimchapa konde la kichwa na kumfany adondokee kaburini kisha kaburi likajifukia moja kwa moja.
Kisha nilimsogelea asia moja kwa moja ambaye alianza kurudi nyuma taratibu huku akitetemeka kwani hakua na nguvu yoyote ya kunizuia.
“leo nimekukamata, utakufa na utafufuka baada ya miaka elf moja au usifufuke kabisa, kwani damu yako nitaiweka kwenye kibuyu cheusi pia kwahio hizo nguvu usahau kuzipata”.
Niliongea kwa kujiamini sana kisha nilinyoosha mkono juu ambapo kilitokea kibuyu cheusi wakati huo asia akiwa ameduwaa kama zezeta ambapo niliweza kumuongoza afanye chochote nitakacho.
“haya jiue mwenyewe, kisha damu yako iweke humu alafu ujizike mwenyewe hapa hapa na kibuyu chako”.
Niliongea ambapo bila kutarajia nilishangaa kuona mvua kubwa ikinyesha kisha asia aliganda kama sanamu.
Kisha ardhi ilijichimba na mwili wa asia ulipotelea chini ya ardhi, nilihamaki kuona pia kibuyu cheusi kikiteketea kwa moto mwisho kilipotea tu kisha mvua iliyokua ikinyesha ilikoma na kukawa shwari kabisa lakini kaburi la asia lilibaki kuwa historia kwani lilikua likionekana usiku pekee na mchana halionekani.
Asia anatazamiwa kurudi baada ya miaka elf moja kwani alikosea mashariti ya uchawi mweusi.
Baada ya hapo nilimshika mkono baba kisha kupotea na ghafla baba alizinduka na kunikuta nikiwa pembeni yake kisha nilimpa pole naye alinipa hongera kwa kufanikisha zoezi la kumteketeza asia kwani alibakiza watu wachache tu ili aweze kuwa mchawi hatari sana.
Ilikua siku ya jumatatu, ambapo sikwenda shule badala yake nilitoka na kwenda mjini kwenye kanisa moja lililopo katika mji mdogo wa mlowo.
Nilifika na kuwaeleza kila kitu na baada ya kumaliza mchungaji aliniombea na niliamua kuachana na uchawi moja kwa moja kwa moyo mweupe.
Haukupita muda mrefu baba nae alitangaza kuachana na uchawi ambapo aliniomba nimpeleke kwenye kanisa nililoenda kupokea wokovu name sikusita nilimpeleka baba ambapo alisalimisha vikorombwezo vyote kisha vikachomwa moto na chungaji peter nyika wa kanisa la presibyterian mlowo.
Baada ya hapo familia yetu ilifungua ukurasa mpya toka maisha ya kichawi hadi maisha ya utakatifu na hatimaye baba na mama waliongeza familia na kufanya tuwe watu watano kwani hata tatizo la ugumba alilokua nalo mama lilipona kutokana na kufunguliwa vifungo vya kichawi.
Nimeandika simulizi hii ili utambue kwamba uchawi upo tena una nguvu sana na asitokee yeyote akakudanganya uchawi haupo lakini mungu ndiye muweza wa yote.
Karibu katika visa vijavyo, kama una mkasa wa kweli unaweza kuanitafuta kwa namba tajwa hapo juu
mwisho