Mkakati wa Freeman Mbowe kugombea urais utaangamiza CHADEMA kama utaendelea anavojipanga

Nani asiyejua kwamba Urais ni mtamu? Nani asiyeutaka? Watu wanajipanga wanapanga mitandao yao ndani ya vyama ndio maana hakuna chama ambacho tayari kimeishamtaja mgombea Urais wake. Ndani ya CDM kuna mitandao ya Urais halikadhalika CCM kuna mitandao ya Urais. Watu wanajipanga kimya kimya wakiviziana. Mbowe ana karata ya kuwa KUB na pia Mwenyekiti wa Chama kwa sasa na Dr. Slaa ana karata ya kuwa Katibu Mkuu wa Chama nasi kila mmoja anajipanga kivyake.

Ndoto za mchana ni mbaya sana....
 
Hizi ni propaganda tu za kutaka kufifisha chadema.
Kila mwanachama wa chadema ana haki ya kugombea na demokrasia itaamua.
 
Freeman Alkaeli Mbowe anaamini kuwa fursa ya CHADEMA kuchukua nchi ni 2015,hivyo ni fursa muhimu kwake kugombea urais kupitia CHARDEMA,ili afanikiwe ameamua kugombea tena uenyekiti wa CHADEMA mwakani ili ajiweke katika nafasi nzuri kinyume na kauli yake kuwa hatagombea uenyekiti tena.

Ili kufanikiwa kwa sasa mkakati unaoratibiwa na wafanyakazi wa CHADEMA ndani ya chama ni kuandaa na kuratibu mapambano dhidi ya Dr.Slaa anaeonekana kuwa kikwazo kikuu na kisiki cha mpingo kwake,hofu juu ya zitto inazidi kupungua kutokana na umri,kasha zinazozidi kumuandama Kabwe.

Wapenda haki na mabadiliko ndani ya nchi hii,mwambieni Freeman Mbowe kuwa kwa sasa Dr.Slaa anafaa kwa vigezo vyote japo anamadhaifu mengi kama wanadamu wengine lakini ukimlinganisha na Mbowe utajua umuhimu wa Dr. Slaa.

Naomba kusema haya kwa kuwa napenda mabadiliko yatakayohakisi maisha ya watanzania na si vinginevyo

Akili za akina Mazomba hizi .
CCM knows kwamba Mbowe amekuwa kisiki na Slaa .Sasa wanaanza majungu .Akili ndogo hizi haziwezi kuongoza kubwa .Mkakati umeshindwa kabla haujaanza .Mbowe is very smart na hana shida na Urais na yeye kugombea uenyekiti tena nakubali maana ameongoza vyema Chadema akiwemo Zitto na wote wana Chadema .Mbona hamsemi Lipumba na KAFU maana mnajua kisiki ni Chadema na viongozi wake
 
Mkuu kwenye thread za Tuntemeke hukosekani......Zitto ana kundi la vijana gani? Wa CCM? Unaonaje kura ya maoni hapa JF? Siyo vijana wanapiga hizi kura? Achana na cheap politics mkuu....

Mku OPORO ndiye TUNTEMEKE? Mkuu Molemo mbona nimemtaja Dr. Slaa, Mbowe na Zitto lakini wewe umesingle out Zitto tu? Naona wewe na Zitto ni paka na panya. Mkuu kura ya maoni ndani ya JF hali reflect mawazo ya wana CDM wote.
 
Last edited by a moderator:
Kwenye katiba mpya bei ya vinywaji iendane na mnywaji mwenyewe!
 
Mimi napendekeza Halima James Mdee agombee kwani anakubalika sana kwa vijana wengi wa kawe na anaweza kujenga hoja. Halima Mdee is Presidential Material
 
Freeman Alkaeli Mbowe anaamini kuwa fursa ya CHADEMA kuchukua nchi ni 2015,hivyo ni fursa muhimu kwake kugombea urais kupitia CHARDEMA,ili afanikiwe ameamua kugombea tena uenyekiti wa CHADEMA mwakani ili ajiweke katika nafasi nzuri kinyume na kauli yake kuwa hatagombea uenyekiti tena.

Ili kufanikiwa kwa sasa mkakati unaoratibiwa na wafanyakazi wa CHADEMA ndani ya chama ni kuandaa na kuratibu mapambano dhidi ya Dr.Slaa anaeonekana kuwa kikwazo kikuu na kisiki cha mpingo kwake,hofu juu ya zitto inazidi kupungua kutokana na umri,kasha zinazozidi kumuandama Kabwe.

Wapenda haki na mabadiliko ndani ya nchi hii,mwambieni Freeman Mbowe kuwa kwa sasa Dr.Slaa anafaa kwa vigezo vyote japo anamadhaifu mengi kama wanadamu wengine lakini ukimlinganisha na Mbowe utajua umuhimu wa Dr. Slaa.

Naomba kusema haya kwa kuwa napenda mabadiliko yatakayohakisi maisha ya watanzania na si vinginevyo

Oporo

Acha kujificha mgongoni mkuu...acha kuweka hoja za kutunga hapa kisha watu wapoteze muda wao kujadili. Labda humjui Freeman Aikaeli Mbowe. Kwake yeye muda huu suala la muhimu zaidi ni kujenga chama, kueneza chama na kuimarisha structure ya chama kuanzia ngazi ya chini mpaka ya juu. Hii inawaumiza kweli ambao mgependa kuona CHADEMA ikipiga mark time, ifanane na vile vyama vingine mnavyovitumia wakati wa uchaguzi na kwenye maslahi yenu ya kuendeleza 'status quo' kadri mnavyotaka

Inajulikana wazi kuwa kuna watu, wakiwemo wanachama, mashabiki, wapenzi wa CHADEMA na hata maadui wa chama hicho mbadala pekee wa CCM Tanzania, wangependa kweli kujua mgombea wa CHADEMA kwenye urais 2015. Bahati mbaya sana wanasahau kila mara kuwa imesisitizwa hilo si moja ya masuala yanayopewa kipaumbele kwa sasa na chama hicho. Muda ukifika kila kitu kitakuwa wazi, mgombea atapatikana.

Wengine wapo wanatamani kweli kweli kuwe na mtifuano juu ya masuala yasiyokuwa na msingi kwa sasa kati ya viongozi wakuu wa CHADEMA, hilo nalo limeshindikana kwa sababu mambo ya CHADEMA yanaongozwa kwa kufuata katiba, kanuni, miongozo na taratibu! Yote haya yatazingatiwa.

Nani anakumbuka mgombea wa CHADEMA 2005 NA 2010 alipatikana namna gani? Msisahau pia mwaka 2000 na 1995 suala la kugombea urais kwa chama hiki lilikuwaje au lilikuwa treated namna gani.

Kama kweli Aporo unapenda mabadiliko, tena kupitia chama cha watu CHADEMA kama unavyotaka kuonesha hapa, achana na hoja za kupikwa na CCM ili kubadilisha watu mawazo badala ya kuzungumzia Operesheni M4C, awamu ya kwanza, inayoendelea mkoani Morogoro sasa, kisha Iringa, Dodoma, Manyara na hatimaye Singida, tujadili masuala ya CCM. Jiunge na wengi katika kuwa focused. Usiwe na wachache wanaokubali kuyumbishwa na kujadili hoja za CCM katika namna ya kuendesha CHADEMA!

Watieni nguvu makamanda walioko mstari wa mbele kwa sasa katika Operesheni M4C ambayo itakuwa ni non stop mpaka Mei mwakani.
 
Lakini pia wanaotaka CHADEMA kwa sasa wapoteze muda kujadili urais badala ya kujenga na kuimarisha mapambano na kuwaandaa Watanzania kwa ajili ya mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala, wakumbuke hii taaarifa muhimu, iliyotolewa siku nyingi hivi;

TAARIFA KWA UMMA

CHADEMA; URAIS UTAAMRIWA KWA MAHITAJI YA UMMA NA SIFA ZA KIONGOZI, SI UTASHI WA WATU/MTU BINAFSI

KUMEKUWEPO taarifa zinazosambazwa kwa umma kupitia njia mbalimbali za upashanaji habari, zikiwa na nia ya kuonesha kuwa kuna mbio za kuwania urais ndani ya chama na kuwa kuna baadhi ya watu wanapewa nafasi kubwa kugombea nafasi hiyo, kiasi kwamba sasa ndani ya CHADEMA "hapatoshi" kwa ajili ya kuwania urais.


Chama kinapenda kutoa taarifa sahihi kwa wanachama, wapenzi, washabiki wake na Watanzania wote kwa ujumla, juu ya suala hili ambalo linaweza kuiweka CHADEMA katika mizania moja vyama vingine au kuwafananisha viongozi wa chama hiki na viongozi wa vyama vingine ambao wamekuwa wakilifanya suala la kugombea nafasi ya urais kuwa linaongozwa na kuamriwa kwa utashi binafsi wa mtu, ukiongozwa na uchu na tamaa ya nafasi ya vyeo.



Kwa sasa ndani ya CHADEMA kitu hicho cha ‘kupamba moto' kwa ajili ya kuwania urais hakipo na wala hakiwezi kuwepo. Hasa kwa sasa ambapo chama kimejikita kuzidi kujijenga kwa kutimiza wajibu wake, kama serikali mbadala inayosubiri kupata ridhaa ya wananchi kuongoza nchi.



Kwa muda huu, kwa CHADEMA suala muhimu ni namna ya kutafuta mizizi au vyanzo vya matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii pana ya Watanzania na kisha kutafuta majawabu au masuluhisho ya kudumu, kwa kushirikiana na Watanzania wote wenye nia njema na nchi yao, kwa ajili ya maendeleo ya watu. Hii ndiyo ajenda muhimu, chama kinasimamia na hakiwezi kutolewa kwenye mstari kwa watu kukimbilia urais.


Kwa CHADEMA, siku zote suala la urais linategemea na kufuata mahitaji mapana ya Watanzania, kamwe haliwezi kuamriwa kwa kufuata matakwa, utashi au uchu wa watu/mtu binafsi. Na katika kufikia hatma ya mahitaji/ maslahi mapana ya wananchi, chama hiki siku zote huamua kwa kufuata na kuzingatia katiba, kanuni na taratibu zake, si vinginevyo.


Ni uwezo na umakini wa kuzingatia mahitaji ya chama na maslahi mapana ya umma katika kuamua masuala mazito kwa mstakabali wa taifa, huku kikifuata katiba yake, kanuni na taratibu, ndiyo umekipambanua CHADEMA kuendelea kuwa chama makini, kinachoaminiwa kwa dhati na Watanzania, na kiupekee kuwa kinastahili kupewa ridhaa ya kuongoza nchi hii.


Mahitaji ya chama na ya Watanzania ndiyo yaliyotumika kupata wagombea urais wa CHADEMA katika chaguzi kuu mbili, mwaka 2005 na 2010. kwa kuzingatia mtazamo huo, mara zote hizo mbili, wagombea waliombwa, wala hawakuongozwa na uchu au tamaa ya madaraka.


Hali itakuwa hivyo hivyo wakati ukiwadia wa kumpata mgombea urais wa mwaka 2015, kamwe utashi, uchu au maslahi binafsi ya mtu hayawezi kupata/kupewa nafasi ndani ya CHADEMA.


Kwa CHADEMA, urais si cheo, ni dhamana ya utumishi kwa umma, suala ambalo linazingatia masuala muhimu, ambayo ni mahitaji ya wananchi (nchi) na kisha sifa za mtu husika kuwa kiongozi wa nafasi hiyo.


Kwa sasa CHADEMA na viongozi wake makini hawawezi kuanza mbio za kusaka urais, badala yake, muda wa sasa unatumika kujikita katika kushughulikia na kutafuta ufumbuzi wa vyanzo vya matatizo ya jamii yanayozidi kuongezeka, huku serikali ikiishia kushughulika na dalili/matokeo, hivyo kukosa majawabu ya kudumu na kuishia kutoa lawama kwa wakosoaji wake.



Hivyo kinachopewa umuhimu ni utumishi kwa umma, kwa ajili ya maendeleo ya watu na si mbio za kusaka vyeo. Ni vyema hii dhana ya mtu kufuatwa na kuombwa, mara anapoonekana kuwa anafaa kuongoza, kulingana na mahitaji ya watu na sifa za nafasi hiyo, kama ambavyo imekuwa ikifanyika ndani ya CHADEMA, ikaenziwa na kufanywa kuwa ni namna bora ya kupata viongozi.


Daima, CHADEMA na viongozi wake makini, kitaendelea kuweka mbele kwanza kabla ya kitu kingine chochote, mapambano dhidi ya vyanzo vya matatizo kama vile umaskini (ugumu wa maisha), rushwa na ufisadi mwingine lukuki unaozidi kutafuna na kuangamiza taifa na watu wake, hali inayowafanya Watanzania kuwa katika mtanziko na mkwamo mkubwa kimaendeleo, miaka 50 baada ya uhuru, huku wakiwa ndani ya taifa lenye baraka tele za utajiri wa rasilimali na kila aina ya nyenzo muhimu inayohitajika kwa maendeleo ya watu. Hii ndiyo ajenda ya muhimu kwa sasa.


Imetolewa leo, Januari 8, 2012, Dar es Salaam
Kurugenzi ya Habari na Uenezi, Makao Makuu ya CHADEMA Taifa


 
Huyu mleta thread,anataka kucheza na akili za watu,swala la urais ndani ya CHADEMA limetolewa ufafanuzi mara kwa mara,kuwa sio KIPAUMBELE cha chama,
 
Mie naona kwanza wangejaribu kupata japo nusu kitu (uwakilishi) huko Zanzibar.

Sisi kama vuguvugu la madiliko hatuwatambui watu wa visiwani ( Zan & Pemb).
Zanzibar wana wa2 1.5 million ambao wanaingia mara mbili kwa mji mzima wa Mwanza na wanaingia mara 9 kwa kanda ya ziwa.
Chadema wanaitaji kushinda kwa kishindo KANDA YA ZIWA, KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI, na KANDA YA KASKAZINI. Maeneo mengine ya nchi CDM watagawana kura na vyama vingine.
Zanzibar haina umuhimu.
 
Sisi kama vuguvugu la madiliko hatuwatambui watu wa visiwani ( Zan & Pemb).
Zanzibar wana wa2 1.5 million ambao wanaingia mara mbili kwa mji mzima wa Mwanza na wanaingia mara 9 kwa kanda ya ziwa.
Chadema wanaitaji kushinda kwa kishindo KANDA YA ZIWA, KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI, na KANDA YA KASKAZINI. Maeneo mengine ya nchi CDM watagawana kura na vyama vingine.
Zanzibar haina umuhimu.

Wahesabu na ndugu zao wapenzi walioko bara nao nadhani unawajuwa na hata huko Mwanza wako. Kisha hesabu kura zako. Ukishinda uchaguzi wa Urais ntatembea uchi siku hiyo. Nakuahidi.
 
Mkuu hujasikia kuna mama anapitapita huku na huku kusafisha njia? Zitto ana kundi la vijana, Dr. Slaa ana kundi la wakereketwa na Freeman Aikael Mbowe ana kundi la wahafidhima ndani ya chama! Unataka udadavuzi zaidi? Mkuu siasa ni kujipanga na siasa ni makundi hakuna siri yoyote na asikudanganye mtu kwamba kuna mwanasiasa ambaye anataka uongozi lakini hana kundi hasa akiwa anataka uongozi huo kupitia jumuiya fulani kama chama cha siasa.

Kwa sasa CDM hakuna mgombea Urais kwa hiyo nafasi ipo kwa yeyote atakayemzidi mwenzake kwenye uamuzi ndani ya chama. Hivyo basi watu wanajenga ngome zao. Ingekuwa hakuna shida basi ingekuwa wazi kwamba Dr. anapewa nafasi nyingine ya kujaribu lakini kwa kuwa si hivyo basi uamuzi wa wanachama au wazee (kumbuka uenyekiti na Zitto) utachukua nafsi.

Mkuu Kimbunga,
Mbona umefanya makusudi umemsahu Lema na kundi lake.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom