Mkaa VS Gesi

Mkaa VS Gesi

Watanzania walio wengi vipato vyao vidogo sana ivyo upelekea kumudu kununua mkaa wa 500 mpaka wa 1000 ambao utumika mpaka jioni, sasa uku kwenye gesi shida pale inapoisha ndio ugumu unapoanzia pesa ndani huna lazima utanunua tu mkaa hili maisha yaendelee. Ila sasa kwenye hizi gesi kuna mitungi midogo na mikubwa shida kwenye hii mikubwa sasa ikitokea gesi imeisha na ndani huna hata mia itabidi uuweke pembeni sijui mpk baada ya mwezi mmoja au miwili hata mitano ushuuda ninao wapo wengi sana mitungi mikubwa imewashinda ushaur kama unaona kipato chako cha shida nunua kamtungi kadogo tu maisha yaendelee
 
Habarini,
Jamani leo naomba tujadili hili jambo binafsi, naona gesi ni bora na bei rahisi kuliko mkaa lakini naona hadi leo kuna watu wanapendelea kutumia mkaa wakisema ni bei rahisi kuliko gesi sasa nashindwa kuelewa ni bei ndogo kweli au ni mazoea, naomba tujadiliane kati ya gesi na mkaa kipi bora na bei rahisi?
Hii maada haijabeba uhalisia wa maeneo tofauti tofauti ya Tanzania.. inawezekana mtoa maada amefikiria miji mikuu pekee.. Mfano: Kwa mji wanakoishi wazazi wangu ambao ni makao makuu ya mkoa fulani, tunapata gunia la mkaa kwa sh 17,000/=. Burnout ya mkaa ni tofauti na gesi, Wakemia wanajua vema.. kupika majimbi, maharage, kande, kuchemsha maji ya kuoga familia etc.. kwa ile location mkaa >>>>>>>>gesi
 
Gesi ni bora na rahisi kwa watu wenye kipato cha kati lakini gesi ni bora ila siyo rahisi kwa watu wenye kipato cha chini, kwa mfano; kuna familia unakuta kwa siku wana uwezo wa kununua mkaa wa mia tano tu ambao hupika siku nzima kwa kujibana sana, hatahivyo hakuna gesi ya 500. Utambue kuwa watanzania wengi wana kipato cha chini na hawawezi kukusanya elfu 21 au 22 ya kununulia gesi ya mitungi midogo kila inapoisha ila wanauwezo wa kubahatisha 500 ya kununulia mkaa.
Umesema kweli kabisa
 
Kama rahisi kwann isipike maharage?
Hii dhana ya gesi kutokupika maharage sijui inatokea wapi!!!??? Mi naona ni woga wa watu kuhisi maharage yanachukua muda mrefu kuiva kwahiyo yatamaliza gesi na si kwamba gesi haiivishi maharage.
Mimi natumia jiko la gesi kupikia kila kitu na mambo yanaenda poa tu, hofu yangu kwenye gesi ni usalama maana inahitaji umakini mkubwa sana kuihifadhi ili kuepuka mlipuko.
 
Gesi ni nishati ya bei rahisi sana ukilinganisha na Mkaa.

Nitolee mfano wa familia yangu::
Kukiwa hakuna gesi, hutumia mkaa wa sh 2000/= kwa siku, ambao ni wastani wa sh 60000/= kwa mwezi.

Lakini ninunuapo gesi ya Oryx kilo 15 kwa takribani shilingi 48000/=, hukaa kwa muda wa miezi miwili mpaka mitatu. Ambayo kwa wastani ningetumia mkaa ingekua ni kati ya 120,000/= - 180,000/=.

Japo ugumu wa gesi ni kuchemshia vitu vigumi mfano maharag n.k ambavyo kwangu mimi hununua mkaa hata wa 2000/= na vitu husika vikaCheshwa vingi na kuhifadhi kwa friji.

Kiujumla gesi + friji ni gharama nafuu sana.
Pole mkuu mkaa wa 2,000 ni debe 1 kwetu
 
Hivi ile gesi ya mtwara tuliyoambiwa tutauziwa bei rahisi bado?
 
Naomba utupie picha ya hilo jiko bunifu na sehemu ambayo mtu anaweza kulipata
 
Back
Top Bottom