Mkaa VS Gesi

Mkaa VS Gesi

Watanzania wengi bado wanaishi maisha ya kupanga tena nyumba zile za chumba kimoja kimoja bila kuwa na private kitchen, sasa akinunua gesi ataliweka wapi, uani anakopikia au chumbani? Naamini wengi wanatamani gesi lkn mazingira hayaruhusu, majiko ya kushea wanaibiana mkaa, mafuta mpaka vifuu vya nazi, leo ununue jiko la gesi uliweke uani kwenye public kitchen utaishia tu kugombana na watu. Halafu mwingine kupata elf. 2000 ya mkaa ni rahisi sana kuliko kumwambia atoe 48,000 ya mkupuo kununua gesi
 
Gesi ni nishati ya bei rahisi sana ukilinganisha na Mkaa.

Nitolee mfano wa familia yangu::
Kukiwa hakuna gesi, hutumia mkaa wa sh 2000/= kwa siku, ambao ni wastani wa sh 60000/= kwa mwezi.

Lakini ninunuapo gesi ya Oryx kilo 15 kwa takribani shilingi 48000/=, hukaa kwa muda wa miezi miwili mpaka mitatu. Ambayo kwa wastani ningetumia mkaa ingekua ni kati ya 120,000/= - 180,000/=.

Japo ugumu wa gesi ni kuchemshia vitu vigumi mfano maharag n.k ambavyo kwangu mimi hununua mkaa hata wa 2000/= na vitu husika vikaCheshwa vingi na kuhifadhi kwa friji.

Kiujumla gesi + friji ni gharama nafuu sana.
Hoja ya msingi hii...ulinganifuu huu basi mzani umekaa mahali pake
 
Ni kweli lakini inategemea na mazingira.

Kwa hali halisi ya sasa mkaa wa sh 1000/= haumalizi siku? Huo mtu akijibana sana kabisa ni mkaa wa 1000/= (sijajua maeneo ulipo bei za mkaa zipoje)
Gesi ni bora na rahisi kwa watu wenye kipato cha kati lakini gesi ni bora ila siyo rahisi kwa watu wenye kipato cha chini, kwa mfano; kuna familia unakuta kwa siku wana uwezo wa kununua mkaa wa mia tano tu ambao hupika siku nzima kwa kujibana sana, hatahivyo hakuna gesi ya 500. Utambue kuwa watanzania wengi wana kipato cha chini na hawawezi kukusanya elfu 21 au 22 ya kununulia gesi ya mitungi midogo kila inapoisha ila wanauwezo wa kubahatisha 500 ya kununulia mkaa.
 
Ni kweli kabisa mkuu. Suala la utamu wa chakula ni utaalamu wa mpishi tu.

Mfano: kipindi tunaanza maisha na wife tulikua tunatumia mkaa na ndio alikua mpingaji mkuu wa wali wa gesi. Ila kwa sasa kashazoea gesi anatoa vitu vya maana mzee
Wali wa rice cooker ndo wakidwanzi.
Wali wa kupikiwa na gas unahitaji utaalamu sana kupikwa na unakiwa mtamu kama kawaida, ila ukikosea ndo unatoa boko.
 
Wewe umekuja na hoja nyingine sasa...hoja ya ladha....umetoka kwenye hoja ya unafuu kiuchumi ukahamia kwenye ladha nzuri nishati ipi inatoa ladha nzuri ya chakula,rudi kwenye hoja
Kwa unafuu wa uchumi mkaa unatosha ukitumia jiko bunifu gunia la elfu 80 utadumu nalo miezi 6 kama una familia kama hauna ni mwaka 1 na unapika haina yoyote ya chakula bila kujari ugumu wa chakula hicho kuiva
 
Watanzania wengi bado wanaishi maisha ya kupanga tena nyumba zile za chumba kimoja kimoja bila kuwa na private kitchen, sasa akinunua gesi ataliweka wapi, uani anakopikia au chumbani? Naamini wengi wanatamani gesi lkn mazingira hayaruhusu, majiko ya kushea wanaibiana mkaa, mafuta mpaka vifuu vya nazi, leo ununue jiko la gesi uliweke uani kwenye public kitchen utaishia tu kugombana na watu. Halafu mwingine kupata elf. 2000 ya mkaa ni rahisi sana kuliko kumwambia atoe 48,000 ya mkupuo kununua gesi
Nimekuelewa hapo kwenye kulipia gas 48elfu kwa mkupuo ni tofauti kweli na ili ya kununua 2000 hapo ni kweli,familia nyingi kuna ugumu kumudu nishati ya gas hasa kwa hii factor...

Nini kifanyike sasa ,cha kufanya:intakiwa wasambazaji wa gas waweze kuwa na mitungi ya size ili kila mwananchi aweze kumudu gharama,ipatikane hata kamtungi ka elf5 to satisfy kila class,kama kweli tunataka kuachana na mambo ya mkaa kabisa
 
Back
Top Bottom