Mjumbe wa CCM ajiunga UKAWA

Mjumbe wa CCM ajiunga UKAWA

Angekuwa CHADEMA angeitwa msaliti kwa kweda kinyume na msimamo wa chama, angeandaliwa waraka ukionesha alivyolipwa hela ili kisliti cham na kushughurikiwa ikiwemo kufukuzwa uanachama, nadhani bunge hili limesaidia kuonesha ukomavu wa demokrasia kati ya CDM na CCM

Unajishaua tu kuchomekea cdm ili upotezee hiyo picha iliyotokea mbele ya waandishi wa habari. Kama wanaukomavu wa kisiasa mbona walikuwa hawataki aongee mambo mengine. Huyo sijiu Ummi Mwalimu mbona alikuwa anamlazimisha ajibu anavyotaka yeye? Na kwanini walimlazimisha kuondoka asiendelee kuongea na waandishi wa habari? Hiyo aibu inayoendelea huko ndani kuna wenye akili timamu wameshawajua kwamba hamna nia njema. Mnaibadilisha rasimu mpaka mambo ya uwajibikaji mnatoa huku mkijifanya mnajali demokrasia. Ona aibu kidogo.
 
Kwann serikali tatu na kwann serikali mbili ?!

#TUACHE SIASA emu fanya kunielewesha apo

Unapounganisha vitu viwili kinatokea kitu kimoja! Huu ndo MUUNGANO lakini unapounganisha vitu viwili na vikaendelea kuwa viwili basi kuna kasoro! Maana yake ni kuwa kuna kiunganishi ambacho ama kimeua asili yake na kuvaa asili mpya ama kumekumbatia asili mbili! Kwa maana nyingine lazima muungano huo utasababisa kimoja kupooza na kingine kuwa na nguvu. Ili kuondoa dhoofu hiyo tunashauri kuwa kila kiunganishi kiwe na uhalisi wake baada ya hapo kuwepo na ushirikiano tu. Ushirikiano huu tutakaoubatiza Muungano utakuwa wa kushirikiana baadhi ya mambo fulanifulani na sii yote. Sioni hofu inatoka wapi! Kimsingi ukiangalia Waziri mkuu hafanyi mambo ya muungano wa Tanzania. Ukichunguza kwa makini utajua tu kuwa kuna nchi iliyofichika ambayo tunawafumba watu macho kwa lazima ili waamini hivyo! Huu sio ukweli!
Hivi kiukweli neno Tanganyika lilikwenda wapi? Kumbuka mkataa kwao Mtumwa! Kwa nini Tanganyika ife?
Asante Mh Ali Mohamed Kessy kwa kuliona hili.
 
Ukikubali kuwa CCM lazima ukubali kukabidhi akili yako kwa Kinana, huwezi kutumia akili yako. Kila mwenye akili anajua kabisa serikali mbili ni uhayawani lakini ukiwa CCM unalazimishwa uhayawani uuone ndiyo werevu.

UKAWA ndo nini
 
Kama mnara wa baberi vile. Miccm imeshaanza kuvurugana yenyewe kwa yenyewe.
 
Mtu mwenyewe chizi nilijua mtu wa maana.
 
Nimecheka sana kweli Kessy mwanaume wa shoka.
Hata mimi kessy namkubali sana kwani anaongea kama masihara ila kuna ukweli ndani yake
Big up mbunge kessy
 

Attachments

  • Ally-Kessy(2).jpg
    Ally-Kessy(2).jpg
    16.1 KB · Views: 131
"Kesi twende bwana.....maana nikikuacha utaongea mambo mengi sana"- Mbarawa

Hata mimi hiyo kauli hiyo imenikuna maana inaonesha dhahiri kuwa ccm wanakiri kuwa hata wao wenyewe wanajua kuwa wanachofanya ni uhuni mtupu!
 
Namuheshimu Zaidi Kessy ndiyo uanaume huo.... Ana mawazo tofauti lakini anasemea Bungeni. Ukawa walitakiwa kubaki Bungeni wapinge mlemle.
 
unapounganisha vitu viwili kinatokea kitu kimoja! Huu ndo muungano lakini unapounganisha vitu viwili na vikaendelea kuwa viwili basi kuna kasoro! Maana yake ni kuwa kuna kiunganishi ambacho ama kimeua asili yake na kuvaa asili mpya ama kumekumbatia asili mbili! Kwa maana nyingine lazima muungano huo utasababisa kimoja kupooza na kingine kuwa na nguvu. Ili kuondoa dhoofu hiyo tunashauri kuwa kila kiunganishi kiwe na uhalisi wake baada ya hapo kuwepo na ushirikiano tu. Ushirikiano huu tutakaoubatiza muungano utakuwa wa kushirikiana baadhi ya mambo fulanifulani na sii yote. Sioni hofu inatoka wapi! Kimsingi ukiangalia waziri mkuu hafanyi mambo ya muungano wa tanzania. Ukichunguza kwa makini utajua tu kuwa kuna nchi iliyofichika ambayo tunawafumba watu macho kwa lazima ili waamini hivyo! Huu sio ukweli!
Hivi kiukweli neno tanganyika lilikwenda wapi? Kumbuka mkataa kwao mtumwa! Kwa nini tanganyika ife?
Asante mh ali mohamed kessy kwa kuliona hili.

niliambiwa kuna bendera ya tanganyika ila watanzania hatuijui ??!

Kwanini serikali tatu na kwanini serikali mbili apo ndo nataka kuelewa ??!
 
Huu ndio ukweli baadhi ya wajumbe wanabututwa na siku zote ccm hawataki kupewa ukweli nashkuru sana MR KESSI natambua mpo wachache simamia ukweli usiyumbishwe sisi wananchi wako wa nkasi tupo pamoja na wewe tetea maoni yetu wala usiwe na shaka 2015 maana wengi wanaogopa hawatapewa nafasi sisi tupo na wewe hata wakikukataa sisi ndo tunaofanya maamuzi bg up Mbunge wangu Kessy
 
mkuu huwa una kimuhemuhe...

post moja haikutoshi?


Mwenzio yupo kazini hapo kila post buku saba lazima akatishe katishe sentensi ili apate 7,000X nyingi watoto waende choo.

Ni moja ya ajira milioni moja na nusu za CCM
 
ni haki yake ya kidemokrasia ,,hamna shida yoyote, hongera kessy kwa kutoa maoni yako
 
Back
Top Bottom