Mjumbe wa CCM ajiunga UKAWA

Mjumbe wa CCM ajiunga UKAWA

Abarikiwe sana Ally Kessy huyu Deo Filikunjombe na mwenzake Kange Lugola ni wanafiki tu wanajifanya wanaipenda Tanzania mbona kwenye hili la katiba mpya wame fyata mikia na kua mbwa koko?

" ukiitwa mpumbavu kwa ajili ya haki na kweli , upumbavu huo una maana kubwa kuliko kusifiwa na watu wanaopenda dhuluma na hila hata kama ni wengi"
GOD BLESS LEMA.
 
Kessy, Bulaya na Lembeli ni kama mke aliyeolewa na mume mlevi na asiyejali familia lakini ana pesa na jina la kigogo ofisi ya serikali kwavile mke anapenda aendelee kuitwa ''mama kigogo'' basi anavumilia yote japo anaona siyo sahihi. Ushauri: Kujikomboa ni kuondoka ili kupata uhuru kwingineko
 
Ajabu kuna mijitu haipo hata Dodoma sembuse kuwa mjumbe wa kamati itakuja hapa na kusema. Majadiliano kwenye kamati yanakwenda vizuri sana. Hebu ona baba mzima ananyamazishwa na mwanae Ummy!
 
Mjumbe wa bunge maalum la katiba Ally Kessy amesema kuwa anaungana na UKAWA katika maamuzi yao huku akiunga mkono serikali tatu mbele ya waandishi wa habari na mwenyekiti wa kamati yake ndugu Samia Suluhu.
 
Huyu mzee japounaweza kusema ayupo makini. Ila kwakweli ni mzalendo na anafanya anachokiona ni haki na sio kukubali kuburuzwa
 
Serikali tatu hata mwenyekiti wao anazitaka sema woga tu ndo umemyumbisha ndo maana mwazo aliwaambia wajiandae kisaikolojia kwa serikali tatu lakini baadaye akachange ati serikali tatu zisubiri aondoke madarakani
 
Taarifa ya hofu hii, haina details za kutosha, ni uzushi mtupu

Hakika kuna watu mko vizuri sana katika kupinga kila kitu ambacho kinakwenda kinyume na matarajio ya CCM.

Ni kweli kabisa Mbunge Ally Kessy amesema kuwa ni LAZIMA kuwe na mabunge matatu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na aliongea msimamo wake mbele ya M/kiti wa Kamati ya BMK Na. 1, Ummy Mwalimu, na Makamu Mwenza, Prof. Mbarawa.

Wapenzi katika Bwana, kuweni na mioyo ya huruma, yenye kusikia sauti za wanyonge na kuweni na upole ili mmpate thawabu yenu kutoka kwa Mungu.

Kwanini kujisumbua kukosoa kila jambo wakati mambo ni dhahiri kuwa maoni ya wana wa nchi ni serikali tatu?

Enyi kizazi cha Nyoka, kinachotawala sasa na baadaye, ni lini mtafanya yenye kumpendeza Mungu, au hamjui kuwa umma wa wana wa nchi ndio waliotoa maoni ya kwamba ni heri kuwa na serikali tatu badala ya mbili ya sasa yenye manung'uniko?

Mbalikiwe.
 
Acha hizo propaganda. Amekuambia kwamba aliomba ruhusa ccm akaruhusiwa? Wewe vipi? Mngekuwa na democrasia ccm mngewaua kina Kolimba, Kombe, Sokoine, Mgimwa, Kibona, na kina mwangosi? Mtaona soon kinachokwenda kutokea kwenye chama chenu hicho cha kigaidi. Chama kilichokataliwa na Watanzania kinachoishi kwa msaada wa nguvu ya polisi!.

Ninaenda nitarudi tena nikupe habari usizopenda kuzisikia japo unazifahamu!.

[/QUOTE]Unalinganisha vipi uwepo wa demokrasia ndani ya CCM na CHADEMA. Imagine huyo mbunge angekuwa wa CDM angeitwa majina yote mabaya na kudaiwa kuwa amehongwa na adhabu yake ni kuvuliwa uanachama. Nadhani CCM imeonesha ukomavu na ustahimilivu wa kisiasa kwa kuruhusu wabunge wake kuwa na misimamo yao tofauiti na CDM ambako ni lazima ufuate msimamo wa chama hata kama unauona siyo sahihi!!!!!!!!!!!!!!!!!!![/QUOTE]
 
Mzimu wa Tanganyika unazunguka vichwani mwao. Ipo siku Ummy ataitetea Tanganyika. Wait you will see.
 
Mjumbe wa CCM ndani ya BMK Mh.Ally Kessy amejiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA katika swala muundo wa serikali tatu na kukataa yanaondelea Bungeni.

Source Mwananchi.

Asante sana kamanda Ally Keissy kwa kukataa kutumikishwa na magamba. Wewe ni mtetezi shupavu wa maoni ya wananchi. Kitaeleweka tu. Magamba watabana na hatimaye wataachia. Maoni ya wananchi wanayoyadharau yatafanyiwa kazi pindi UKAWA wakiingia magogoni mwaka 2015. Ndani ya siku 100 tu UKAWA watawapa wananchi katiba inayotokana na maoni yao bila kuchakachuliwa kama magamba wa CCM wanavyofanya sasa hivi.
 
Ni kweli ameonekana akipendekeza kuwe na Bunge la Tanganyika na Zanzibar(Wawakilishi) halafu Bunge la Muungano liwe na wawakilishi wachache kutoka miongoni mwa Wabunge wa Tanganyika na Wawakilishi wa Zanzibar

Waliambiwa muundo wa serikali ndio moyo wa katiba Wasira akakejeli wakati wa mdahalo. Sasa yako wapi? Wameanza kurudi kulekule ila kwa kupitia mlango wa uani. Hongereni UKAWA kwa kuona mbali.
 
Bwana Kessy ni mzalendo tatizo ni maccm wenzake, ila hawana chakumfanya zaid zaid wakijichanganya anawafyatua na wao.
 
"Kesi twende bwana.....maana nikikuacha utaongea mambo mengi sana"- Mbarawa
 
Huyu bwana ni kiboko aliyatamka hayo mbele ya Mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa kamati yake, walimpeleka kwa waandishi wa habari ili akanushe yeye akashindilia msumari wa moto na kuwaacha hawana la kufanya ,na picha yao ipo kwenye gazeti.
 
Back
Top Bottom