Mjue milionea Chivayo anayefuata nyayo za Ginimbi

political monger senior

JF-Expert Member
Nov 26, 2020
1,801
5,788
Chivh ni mji mdogo wenye mkusanyiko wa wakazi laki moja na elf 13. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2017. Mji wa Chivh upo umbali wa kilometers 141 kusini mwa jiji la Harare. Njia kuu ya kwenda Africa ya kusini.

Kwanini mji wa Chivh umekuwa sehemu ya andiko hili?!

Sababu hapa ndipo alipozaliwa mwanadamu mwenye kichaa na uwendawazimu wa kupenda magari ya kifahari. Namuongelea the big boss, bilionea himself, WICKNELL CHIVAYO.

'WICKNELL CHIVAYO NI NANI?!'
Wakati kamba za uchumi wa Zimbabwe zikionekana kuvutwa ndani ya mdomo wa kaburi. Lundo la Raia likiwa limenasa katikati ya tope la umaskini. Watu wakilia na kuomboleza dunia iwape mbinu za kuishinda vita dhidi ya ufukara.

Katikati ya mateso haya ya wazimbabwe wengi. Wenye nyuso zilizobeba mikunjo ya hasira na ghadhabu za maisha. Yupo binadamu anayeitwa "WICKNELL CHIVAYO."

Yeye ameigeuza Harare kuwa Las Vegas. Anaishi maisha ya anasa na kufuru, akimwaga radhi kama madon waliolala pembeni ya vitanda vya swimming pool. Kwenye casino za dhambi pale Brunley.

WICKNELL CHIVAYO ni kijana wa miaka 40. Alizaliwa November 22, 1982.

Kwenye mitandao ya kijamii hasa Instagram anatumia jina la @sir_wicknell. Huko ndiko anakofanya kufuru ya kupost ndinga za kileo. Ndinga zinazomgharimu mamilion ya dollars kuziingiza ardhi ya Zimbabwe.

Huyu ni chizi magari. May 8 mwaka huu alilipa zaidi ya billion mbili za kibongo. Kama gharama ya kununua Rolls Royce mpya tolea la 2023.

Baada ya gari kuwasili akapost maneno haya:

"Maumivu ni ya muda mfupi tu, lakini mafanikio ni ya milele. Maombi, kufanya kazi kwa bidii, uvumilivu na kujawa na dhamira, labda ndio njia bora zaidi ya kuwa tajiri. Usikate tamaa Mungu ni mkubwa."

'pain is only temporary but successful is forever. Prayer, working hard, being patient and being full of determination is perhaps the most fulfilling way of becoming rich. Never give up God is greatest.'

NINI SIRI YA UTAJIRI WAKE?!

Zimbabwe anafahamika kama mjasiliamali, mfanya biashara, na mmiliki wa kampuni ya kuuza nishati za umeme inayoitwa INTRATEK.

Hii ni kampuni ambayo inakashfa. Ya kuwahi kupewa tenda ya dola billion 1 za ki Marekani na serikali ya Zimbabwe. Kwaajili ya kuuza nishati. Wakati huo huo kampuni ikiwa haina mtaji wowote Bank.

Ingawa kuna tetesi ambazo hazina nguvu ya uthibitisho zinadai kwamba. Mke wa hayati Robert Mugabe aitwaye "Grace." Ni sehemu ya wamiliki wa kampuni hii.

Wickenell chivayo alikuwa mfadhili wa chama cha soka Zimbabwe. Baadae akajitoa na kujikita mtandaoni. Anakomaliza MB's kuonyesha picha na video mbalimbali. Akiwa sehemu tofauti duniani kuishikisha adabu pesa yake.

1692213722951.jpg
View attachment 2719316View attachment 2719315
 
MAFANIKIO ni ya muda mfupi tu, lakini MAUMIVU ni ya milele. Maombi, kufanya kazi kwa bidii, uvumilivu na kujawa na dhamira, labda ndio njia bora zaidi ya kuwa tajiri. Usikate tamaa Mungu ni mkubwa."

Fumbo umefumbiwa nimekufungulia CODE kwa uchache
Ipo wazi kabisa hasa alipotumia neno perhaps/labda.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom