Mkuu hakika wewe ni mmoja wapo ya wanaume wachache ambao bado wana uanaume wao asilia.
Kuna vitu huwa nasemaga humu na hata nje ya humu ila naishia kuonekana mjima na kupuuzwa lakini ni vitu vya msingi sana.
Wanawake tuliagizwa tuwapende na tuwajibike kuwatimizia mahitaji yao, wakati huo huo pia na wao wakiwajibika kututii kama waangalizi na watu wa kuwaongoza.
Sasa inapotokea unamkabidhi au kugawana majukumu yako na mwanamke tayari hapo unakuwa umehatarisha nafasi yako kama kiongozi wake ambaye anapaswaa akutii.
Kifuatacho ataanza kuona wewe ni sawa na yeye,atakosa utii,malumbano yasioisha na hatimae mwisho wa siku wewe ndio utajikuta una mtii... yaani mkibishana kitu wewe ndio unakuwa wa kwanza kukubali yaishe.
Lakini ukijiwekea mfumo wa maisha wenye element za mababu na mabibi zetu walivyoushi, haya mambo ya mwanamke kukupanda kichwani utayaskia kwa majirani tu.