Nashengena
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 2,022
- 3,700
Haya maisha ni hayatabiriki. Kuna jamaa mmoja alikuwa anafanya kazi na mkewe ni mama wa nyumbani. Juzi juzi kafukuzwa kazi . Mbaya zaidi akapelekwa polisi. Hela alizokuwa nazo inabidi azitumie ili aweze kuachiwa. Sasa hivi hana hata mia, yaani ni shida tupu nyumbani. Hata kama mume ana hela jitahidi sana na wewe kujua namna ya kuzitafuta pamoja na mumeo. Huwezi jua kitatokea nini kwenye haya maisha.Kwahio mkuu tuchukulie mumeo alikuwa na fedha Ila baadae akafilisika au kufariki alafu wewe ndo hivyo majukumu yake huyawezi, yaani ulikuwa golikipa na Sasa umeachiwa watoto... Unafanyaje kuendesha gurudumu au ndo utaanza kudanga? Maana majukumu yote yatakuangalia wewe tu mwanamke?