Gamba la Chuma
JF-Expert Member
- Feb 11, 2012
- 1,243
- 340
MASWALI YALIYOULIZWA NA WADAU KUHUSU TATIZO HILI
Nimesafiri nayo kutoka Dar kuja Iringa na ninatarajia kuitumia kurudi Dar.
Imetokea ghafla steering imekuwa nzito (stiff) ie unatumia nguvu kidogo kukata kona.
Hakuna kelele za belt kwisha, hakuna leakage kwenye steering fluid, na hydraulic ipo level.
Wataalamu wa magari naombeni msaada wa kujua tatizo na kama naweza kuitumia kurudi Dar.
Natanguliza shukrani !
---
---Nna gari aina ya Suzuki Samurai, ambayo ki ukweli iko kiuchumi kwenye ulaji wa mafuta na hata bei ya spea zake. Tatzo imeanza kusumbua, naiwasha vzr naondoka, baadae inaanza kumiss, then inapoteza nguvu na kuzima.
Nikiiwasha tena kwa muda uleule haikubali mpaka engine ipoe kdg, ndo inawaka tena. Nmezunguka sana, kwa mafundi wa mtaani, ambao mpaka wamenishauri nibadilishe spea kama starter, ignition coil na fuel pump, na kugundua kumbe vilikua vizima, mana tatzo limebaki palepale.
Naomba ushauri juu ya ufumbuzi wa tatizo hili kwamba linatatuliwaje hili mana mafundi wa uswazi wamenichosha.
Wandugu habari za mchana. Naomba msaada wa kiuzoefu na ufundi. Nna gari yangu Nisan Serena, from no where ilianza kukosa nguvu na hatimaye ikawa haichanganyi kwa maana ya kutomaliza resi.
Nmewaleta mafundi wengi na kukaribia kumaliza tatizo ila kilichonifanya niombe msaada hapa ni kwamba gari ikiwa haijafunikwa bonet inamaliza resi vizuri, ukifunika tu tatizo linarudi palepale. Mafundi wote niliowaleta, wamepima kwa mashine lakini tatizo liko palepale.
Ebu nisaidieni, nn cha weza kuwa tatizo na wapi au nani anaweza saidia.
Natanguliza shukrani
BAADHI YA MAJIBU YALIYOTOLEWA NA WADAU
---Sababu nyingine inawezekuwa 'catalytic converter' imeziba.
kutokana na maelezo yako inaonesha engine inakosa nguvu baada ya kuendesha umbali fulani. kama mafuta hayachomwi yote kwa muda unaotakiwa kwenye chemba basi mafuta hayo yataendelea kuungua baada ya kutoka kwenye engine (yaani kuungua ndani ya bomba la moshi). Moto huo mkali huyeyusha 'materials' zilizoko kwenye 'catalytic converter' ambazo huziba moshi usitoke nje (muffler).
View attachment 572410
Sasa unapowasha gari kwa mara ya kwanza (asubuhi), 'pressure' katika bomba la moshi huanza kuongezeka kwasababu haina pa kutokea na kadiri unapoendesha ndiyo 'pressure' inazidi. Mwishowe inafika karibu na 'engine' (exhaust manifold) ambapo hukinzana na 'gases' nyingine mpya zinazotoka kwenye engine. Ni kama vile kujaza hewa kwenye tube ya baiskeli, mwanzoni ni rahisi lakini baadae inakuwa ngumu kujaza. Sasa 'pressure' hii huzuia engine kutoa 'exhaust gases' ambapo hupunguza nguvu ya 'engine'.
Sasa kujua kama hili ndo tatizo unatakiwa kupima 'temperature' kabla na baada ya 'catalytic converter' kwa kutumia 'non contact thermometer'. Kama baada ya 'catalytic converter' (kushoto kwenye picha) ni baridi kuliko kabla ya converter wakati 'engine' imepata joto basi lazima kuna mahali pameziba. Kwa kawaida joto baada ya converter linatakiwa liwe juu (150 degrees Celsius)
Baada ya kugundua hilo tatizo inabidi ubadilishe 'catalytic converter' au uweke 'straight pipe' (you didn't hear this from me) lakini inabidi pia utatue tatizo la emission (Kwanini mafuta hayachomwi yote?).
---Kupata taarifa unayohitaji kwenye search engine huwa pia inahitaji ujue key words za kutumia. Kama mleta thread hujafanikiwa ku-identify kwa usahihi tatizo la gari yako sio rahisi Google ikupe solution. Tena basi information nyingi kwenye mtandao zinahitaji maneno sahihi ya kiingereza,
Vitu kama mfano "rejeta" havijulikani! Nashauri uachane na gereji bubu za mtaani zinazotengeneza magari kwa trial and error na badala yake ukubali gharama uende gereji nzuri zipo nyingi,tena ukiweza utafute kabisa Dealer wa SUZUKI maana hii ni model ya zamani kidogo, hakika matatizo yake mengi si mageni kwa wazoefu.
Kila raheli.
---Kwa suala la kuishiwa ngivu na kuzimila halafu haiwaki mpaka ikae muda, hiyo gari itakua ina overheat na chanzo kinaweza kuwa ubovu wa cooling system, yaani radiator na fan au inaweza kuwa cylinder head.
I had the same issue kwenye gari yangu baadae nikaja kugundua tatizo ilikua cylinder head (expensive to buy)
Kukurahisishia kujua kama ni cylinder head rejea historia ya hiyo gari, kama imewahi kuwa na tatizo la kukausha maji (radiator kuvuja or something) na ukaendelea kuitumia kwa mtindo wa kuongeza ongeza maji basi hiyo ni rahisi sana kuharibu cylinder head
Nipe mrejesho and will try my best to help you discovering the acrtual problem
---Kwa kiasi kikubwa inawezekana fuel pump yako imechoka hasa kama gari haiwezi kuaccelerate. Vinginevyo, inawezekana air filter yako imeshaziba, inabidi uibadilishe. Kwa jumla matatizo ya gari kuishiwa nguvu ni ama hakuna mafuta au hewa ya kutosha kwenye combustion chamber. Utaiona wakati mweingine inatoa moshi mweupe.
---Hiyo gari inatumia mfumo wa coil au distributer? kwa uelewa wangu mdogo ili gari ipige res vizuri lazima plug ziwe madhubuti,kama inatumia distributer waya zinazokwenda kwenye plug zikiwa na mchubiko tu inapoteza moto na kusababisha miss.
Hivyo uwezi kuexcelerate ipasavyo, na kama inatumia coil unapaswa kupima coil zote,coz moja ikiwa aifanyi kazi usababisha gari kukosa nguvu na ulaji wa mafuta pia unaongezeka kwakuwa yatakuwa ayachomwi vema kwenye chumba cha coil/plug ambayo aipekeki spark vizuri,
Okay kwa haya maelezo yako kuna uwezekano mkubwa Throttle position sensor ikawa ina shida, kwa sababu hii ndio sensor inayopeleka taarifa kwenye ECU kuwa throttle imeopen kwa nafasi kubwa kiasi gani wakati unaendesha gari.
Kwa hiyo unapokuwa unakanyaga ukifika hapo kwenye 3 badala ya kuendelea kupeleka taarifa kwamba throttle inazidi kuopen yenyewe itakuwa inapeleka taarifa kwamba throttle imeopen kidogo na hivyo kupelekea hewa nyingi kuendelea kuingia kwenye engine wakati ECU inallow mafuta kidogo yaende, na hapo ndio linayokea hilo tatizo la kukosa nguvu.
Kama gari yako ina Accelerator pedal sensor nayo ingeweza kupelekea hilo tatizo.
Anyway kama ungekuwa Morogoro ningekupimia hiyo sensor before ubadili nyingine ili kama tatizo siyo hiyo sensor usingeingia gharama ya kununua sensor nyingine Ila lingetafutwa tatizo exact lipo sehemu gani.
Kama gari yako ina OBD2 port unaweza kupita kwa mtu mwenye OBD2 scanner akakufanyia scanning. Inaweza kukupa picha shida ipo wapi.
Kila la heri mkuu.