Mizengwe president's delivery bureau

Mizengwe president's delivery bureau

Nndu wa Selote

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2012
Posts
733
Reaction score
521
Ndugu Wana JF,

Ni kweli Prtesident's Delivery Bureau (PDB) walitangaza nafasi nyingi na tayari wameshaanza kufanyisha watu Interview kupitia Deloitte.

Cha kushangaza pamoja na usahili kufanywa na Deloitte ambayo ni kampuni nayojitegemea, yale mambo ya Technical Know Who badala ya Technical Know How yapo palepale.


Zipo taarifa za uhakika kuwa zipo nafasi ambazo tayari baadhi ya watu walishaanza kazi kabla hata Interview hazijafanyika. Kwa mfano yupo dada mmoja ambaye tayari ameshaanza kazi kama Mkugenzi wa Mawasilano wakati hata majibu ya Interview ambayo iliyofanyika wiki iliyopita hayajatoka. Habari za uhakika zinasema kwamba huyo dada ambaye awali alikuwa akifanya kazi Airtel anafahamiana vizuri na Afisa Mendaji Mkuu wa PDB Bw.Omar ambaye alishateuliwa na Rais na alishaanza kazi. Pengne Bw. Omar ndiye aliyemwita na kumpa kibarua huyo dada bila kujali Usahili unaondelea.Mliofanya Iterview kwenye nafasi hiyo poleni kwani huenda pamoja na qualification zenu mmekwenda kumsinikiza tu huyo mdada. Hii ndio Bongo bwana !!!
 
mkuu wewe ulitegemea mpaka dakika hii CEO atakuwa pekee ofisini?kazi zimeshaanza kitambo kuna senior wangu mmoja ofisini alishapewa secondment ya kwenda huko kama director toka september,
acha kukatisha watu tamaa naamini deloitte ni taasisi makini katika executive selection
 
Huyo dada kateuliwa na watu/mtu makini kama alivyoteuliwa CEO na Deloitte wanazo taharifa zake.

Halafu kuteuliwa na kuchaguliwa zote njia sahihi kulingana na mahitaji husika.
 
kaka ni dada halafu kitengo chenyewe kinahusiana na Ikulu wala huna cha kushangaa..ni kawaida sana hiyo kitu mbona ....yaani usishindane na wanawake na maendeleo ..teh teheee
 
Jamaa hana chuki binafsi, anasema kile kinachojili ndani ya nchi yetu.. delloite nao matolori tu, watu wanapeana ajira na wakati watu kibao wenye utimamu wapo nchi hii, we kama umeshiba hujui wenye njaaa, ushapata kazi ushasahu ulikotoka, na wengine mnatunisha vifua mbele kwa kazi mlizopewa na wakwe zenu...

lazima tuwaseme, mtu unachoma nauli, unanuna mezania, unatafta fact za kukulinda mwingine anapakaa poda anaenda kujichekesha tu.
 
TUwape muda ili tuje kuyaona hayo "matokeo makubwa sasa".........
 
Back
Top Bottom