Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Taarifa za Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda kutangaza nia ya kugombea Urais mwaka 2015 iliwashitua wengi sana hasa wakulima ambao hadi hivi sasa hawana mahali pa kuuza mahindi yao huku, Pinda akiwa hana majibu ya matatizo haya ya wakulima. Mizengo Pinda ambaye amekuwa waziri mkuu wa Tanzania kwa miaka ipatayo saba sasa, akiwa ameshindwa kabisa kuongoza nchi anatafuta Urais?
Waziri mkuu Pinda ambaye ndiye mtendaji mkuu wa nchi anatambua wazi kwamba chini ya utawala wake nchi imepitia misukosuko mingi ikiwamo ya migogoro ya kidini, ugaidi, kuongezeka kwa kiwango cha umasikini wa kaya, kuongezeka kwa idadi ya watoto wa mitaani, kuongezeka kwa idadi ya mambumbu, huku hali ya miundombinu ya nchi ikiwa mbaya kupindukia. Nchi hivi sasa inashuhudia ukosefu mkubwa wa maji vijijini na mijini, huku kitendawili cha umeme wa uhakika kikiwa kimekosa mteguaji. Tatizo la foleni za barabarani likionekana kama ni fahari machoni pa watawala hawa waliozoea kupitishwa barabarani kwa ving'ola.
Ni katika utawala huu wa Pinda na Kikwete nchi imejikuta ikiwa kwenye lindi kubwa la madeni ya nje na ndani. Huku deni la nje likikua kwa kasi ya kutisha, deni la ndani sasa linatishia hata mstakabali wa maisha ya watanzania. Kimefikia kiwango cha watanzania kuanza kukosa dawa mahospitalini kutokana na nchi kushindwa kulipa madeni yake. Wakandarasi wanalalamikia kutokulipwa pesa zao baada ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya serikali. wasambazaji wa vyakula mashuleni wapo mbioni kugoma huku baadhi ya vyuo vya elimu ya juu na diploma vikifungwa kutokana na kushindwa kulipa bili za maji na umeme.
Hali ya nchi kiujumla inakatisha tamaa. Huyu Pinda ambaye ameshindwa kutumia nafasi yake kutatua au hata kupunguza ugumu huu wa maisha ya watanzania, akiwawaacha wakulima wakiwa na hali mbaya kiasi cha vijana wengi kutokutamani kukaa vijijini, anaota kuwa Rais? Hii ni ajabu sana, na kwa hakika namuona Pinda kuwa ni mtu wa ajabu sana. Sikutarajia mtu aliyeshindwa kuongoza nchi katika nafasi ya uwaziri mkuu, aweze kufikiria kuongoza nchi katika nafasi ya u-Rais. Ni vizuri Pinda akajiengua katika kinyang'anyilo hiki kuliko kujidhalilisha kutafuta madaraka asiyokuwa na uwezo nayo.
Waziri mkuu Pinda ambaye ndiye mtendaji mkuu wa nchi anatambua wazi kwamba chini ya utawala wake nchi imepitia misukosuko mingi ikiwamo ya migogoro ya kidini, ugaidi, kuongezeka kwa kiwango cha umasikini wa kaya, kuongezeka kwa idadi ya watoto wa mitaani, kuongezeka kwa idadi ya mambumbu, huku hali ya miundombinu ya nchi ikiwa mbaya kupindukia. Nchi hivi sasa inashuhudia ukosefu mkubwa wa maji vijijini na mijini, huku kitendawili cha umeme wa uhakika kikiwa kimekosa mteguaji. Tatizo la foleni za barabarani likionekana kama ni fahari machoni pa watawala hawa waliozoea kupitishwa barabarani kwa ving'ola.
Ni katika utawala huu wa Pinda na Kikwete nchi imejikuta ikiwa kwenye lindi kubwa la madeni ya nje na ndani. Huku deni la nje likikua kwa kasi ya kutisha, deni la ndani sasa linatishia hata mstakabali wa maisha ya watanzania. Kimefikia kiwango cha watanzania kuanza kukosa dawa mahospitalini kutokana na nchi kushindwa kulipa madeni yake. Wakandarasi wanalalamikia kutokulipwa pesa zao baada ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya serikali. wasambazaji wa vyakula mashuleni wapo mbioni kugoma huku baadhi ya vyuo vya elimu ya juu na diploma vikifungwa kutokana na kushindwa kulipa bili za maji na umeme.
Hali ya nchi kiujumla inakatisha tamaa. Huyu Pinda ambaye ameshindwa kutumia nafasi yake kutatua au hata kupunguza ugumu huu wa maisha ya watanzania, akiwawaacha wakulima wakiwa na hali mbaya kiasi cha vijana wengi kutokutamani kukaa vijijini, anaota kuwa Rais? Hii ni ajabu sana, na kwa hakika namuona Pinda kuwa ni mtu wa ajabu sana. Sikutarajia mtu aliyeshindwa kuongoza nchi katika nafasi ya uwaziri mkuu, aweze kufikiria kuongoza nchi katika nafasi ya u-Rais. Ni vizuri Pinda akajiengua katika kinyang'anyilo hiki kuliko kujidhalilisha kutafuta madaraka asiyokuwa na uwezo nayo.