Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda amesema isingekuwa katiba ipo “tight” kidogo, basi angetamani kuona Rais Magufuli akiongeza miaka mingine mitano baada ya muda wake kuisha.
"Ni kwakuwa tu katiba zenyewe kidogo ziko taiti lakini kama si kwa sababu hiyo, Walahi ningesema mzee piga mingine mitano tu''
Pia Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu ameongeza kuwa:
“Ni matumaini yetu kwamba katika kipindi hiki hata kama utatugomea kabisa kuongeza kidogo, lakini utahakikisha basi umetupa kiongozi mwingine mzuri kwa kusaidiana na NEC, atakayeweza kusukuma mawazo haya na maamuzi haya magumu ambayo unayafanya”
Mzee Pinda ametoa kauli hiyo leo hii wakati wa Semina ya Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) iliyofunguliwa na Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, inayofanyika Jijini Mwanza.
"Ni kwakuwa tu katiba zenyewe kidogo ziko taiti lakini kama si kwa sababu hiyo, Walahi ningesema mzee piga mingine mitano tu''
Pia Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu ameongeza kuwa:
“Ni matumaini yetu kwamba katika kipindi hiki hata kama utatugomea kabisa kuongeza kidogo, lakini utahakikisha basi umetupa kiongozi mwingine mzuri kwa kusaidiana na NEC, atakayeweza kusukuma mawazo haya na maamuzi haya magumu ambayo unayafanya”
Mzee Pinda ametoa kauli hiyo leo hii wakati wa Semina ya Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) iliyofunguliwa na Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, inayofanyika Jijini Mwanza.