MITSUBISHI Pajero JR

MITSUBISHI Pajero JR

mbona nasikia zinasumbua sana?

Malafyale, huo usumbufu bado sijauona, na kuna watu wengi wana hizo gari, siamini kama hakuna gari zinazosumbua zikichoka, lasivyo tusingeona mikweche ya magari hata Toyota yakitundikwa. Gari yoyote ile nimatunzo na service, ukiwa rough hata kama ingekuwa ngumu vipi, itakusumbua tuu, halafu kitu kingine cha msingi ni service tuu nkamu.
 
Tatizo kujua fundi mzuri

Fundi mzuri wa kukubadilishia oil?? Sema labda ikiharibika kitu kwenye engine labda, lakini pia ukiulizia wazoefu wanawafahamu mafundi wazuri. Lakini pia kununua gari nadhani cha msingi ni uwezo na matumizi yako. Majuzi kuna sehemu nilienda halafu mvua ilipiga sana kukawa na tope jingi mno. kuna jamaa wengi walikwama na Noah zao, dyna, lakini mimi nikajiwekea 4WD huyo nikatambaa zangu huku nikiwa naseleleka mdogomdo. Pajero mini ni gari ndogo sana lakini ina nguvu, iko juu sana na inatumia mafuta kidogo mno.
 
Mkuu,

kama unataka gari fuel economic, iliyo nyanyuka juu, four wheel na imara, fuata hiyo link hapo chini. Hiyo Pajero Jr sikushauri ununue. Ongea kwanza na mafundi kabla hujafanya maamuzi ya kununua gari.

Kama unanunua ulitumie kwa muda kisha uliuze, basi sawa. Ila kama utalitumia kwa muda mrefu likianza kukusumbua utatamani ulitupe.

Pia, kama unanunua gari ukiwa na matarajio ya kuliuza baadae usichukue Manual Transmission. Utapata shida sana kupata mteja. Watu wengi hawawezi kuendesha manual, na pia kwa foleni za dar mguu utauma kwa kukanyaga clutch pedal.

Karibu

Suzuki Escudo GF-TA02W(1998) / 4WD / US$3,790 / 45,000 km / Autorec Enterprise, Ltd - Japanese Used Car [ tradecarview ]


Mtaalamu wangu unamaanisha ni bora anunue Suzuki kuliko Pajero? vipi spare zinapatikana? je bei zake spare ni ndogo au kubwa?....mie nabaki na ushauri wako wa watu maskini but you move at cheap-Starlet or Raum
 
Mpaka sasa bado haijaanza kusumbua kwa kiasi hicho, nimewahi kubadilishia Fuel pump na battery tuu, kingine ni service ya oil ya kawaida ambayo nafanya kila zikikaribia km 3000 za kutembea. Ila pajero GDI ya bro mafundi wake wap jangwani sijajua ni garage ipi ambayo yeye kadumu nayo toka 2008 na iko poa. mimi kwenye gari huwa naamini ktk kulitunza na service tuu. kuna wengine wanadai Honda CRV ni mbovu sana, japo kuna watu wanadumu nazo miaka mingi tuu. Gari ni service na matumizi mazuri.
mimi iliwahi kunisumbua sana GDI,ilikuwa kuwaka asubihi unawasha hadi karibu mara 10 na ukiwa barabarani ghafla inazima!!! mara naambiwa pump ya juu mara sijui nini basi vurugu tupu!ila kuna jamaa wapo tabata wakairekebisha wakasema nozle zilikuwa hazipitishi mafuta vizuri hivyo wakazibadili!!since then inapiga mzigo!!
 
mkuu Prof Gamba!!!hicho kichwa chako vipi?!kuna mtoto nasikia alizaliwa bagamoyo miaka hiyo anakichwa kama chako na sasa ndo rahisi wa nchi je ndo wewe kiongozi ha ha ha ha!!
 
Last edited by a moderator:
mimi iliwahi kunisumbua sana GDI,ili kuwa kuwaka asubi unawasha hadi karibu mara 10 na ukiwa barabarani ghafla inazima!!! mara naambiwa pump ya juu mara sijui nini basi vurugu tupu!ila kuna jamaa wapo tabata wakairekebisha wakasema nozle zilikuwa hazipitishi mafuta vizuri hivyo wakazibadili!!since then inapiga mzigo!!

Ni kweli, hata mimi yangu iliwahi kuwa na tatizo la kutowaka lakini tatizo ilikuwa ni fuel pump (panzi), mimi kwa kuwa na nguvu naziaminia sana. Inabidi kuwa na mafundi wazuri wanaoziwezea.
 
mkuu Prof Gamba!!!hicho kichwa chako vipi?!kuna mtoto nasikia alizaliwa bagamoyo miaka hiyo anakichwa kama chako na sasa ndo rahisi wa nchi je ndo wewe kiongozi ha ha ha ha!!

Ha ha ha ha ha ha ha ha!!! umenikumbusha mbali. Kichwa unayemsema ndo tulikipasua ili kukifanyia uchunguzi, tuliyoyakuta ndo kama hayo unayoyaona kichwani hapo mkuu.
 
mimi iliwahi kunisumbua sana GDI,ilikuwa kuwaka asubihi unawasha hadi karibu mara 10 na ukiwa barabarani ghafla inazima!!! mara naambiwa pump ya juu mara sijui nini basi vurugu tupu!ila kuna jamaa wapo tabata wakairekebisha wakasema nozle zilikuwa hazipitishi mafuta vizuri hivyo wakazibadili!!since then inapiga mzigo!!
mkuu nipe direction ya ofisi ya hao mafundi wako au kama una namba zao za simu nipeleke gdi yangu
 
Ni kweli, hata mimi yangu iliwahi kuwa na tatizo la kutowaka lakini tatizo ilikuwa ni fuel pump (panzi), mimi kwa kuwa na nguvu naziaminia sana. Inabidi kuwa na mafundi wazuri wanaoziwezea.
Yes,ukipata fundi mzuri hutojuta kumiliki pajero jr/mini
 
Back
Top Bottom