Mitandao ya simu kutoa siri za wateja, uhuru wa faragha upo wapi?

Leo wakati rais Magufuli anapokea ripoti ya makanikia amesema kwamba walifuatilia mawasiliano ya mtu ambaye alikuwa anawasiliana na mtu anayeitwa Mwanyika na kumuomba data, hii maanake ni kwamba serikali kwa kushirikiana na kampuni za simu zinaingilia mawasiliano ya watu.

Kwa lugha nyingine ni kwamba mitandao ya simu inatoa siri za wateja wake kwa serikali aidha kwa hiari yao au kwa kulazimishwa, je uhuru wa faragha ya mteja upo wapi? Na kwanini mitandao hii inakubali kutoa siri za wateja wao kwa watu wasio husika, kuna haja ya kuendelea kuwa wateja wa mitandao hii inayotoa siri za wateja wao?.
Alichokosea ni kusema vile mbele za watu.
 
Imedukuliwa ya Jemani kansela sembuse Lisu. Hata humu jamii mnadhani mmejificha? labda kama vidukuzi vyenu havina sirio namba. You are all NAKED when it comes to be 4 national security. Bila govt kudukua simu zenu security ipo wapi?
 
Usalama wa nchi ikiwemo maliasili zake ni muhimu zaidi kuliko huo usiri unaotaka. Kumbe mnahangaika kutaka kupatiwa data ili mpayuke vizuri? Tumewajua

Na inawezekna ika haina ukweli wowote pia.Hivi huyo aliyetajwa Lissu alipewa nafasi ya kujitetea au ni kama hivyo tu!Au ndiyo sababu jana Mlifuata Mwanyika Nyumbani na NOAH?
 
Lissu hawezi kuwa wa kiwango hicho. Atake data kwa Mwanyika ili iweje hasa?? Yeye Lissu ana nini cha kuogopa au kupoteza mpaka ahahe??

In fact, nasubiri taarifa/andiko lake kwenye Ripoti hii ya Pili.
 
Linda privacy kwa kutumia whatsapp call.
Speak Freely
WhatsApp Calling lets you talk to your friends and family, even if they're in another country. Just like your messages, WhatsApp calls are end-to-end encrypted so WhatsApp and third parties can't listen to them.
 
Wewe endelea kutumika kama kibaraka tu ila siku ukijua maana ya whistleblower hutauliza hilo swali
 
ESCROW mlipiga pesa <br />RICHMOND mlipiga pesa <br />TANGOLD mlipiga pesa <br />BUZWAGI mlipiga pesa <br />EPA mlipiga pesa<br />MEREMETA mlipiga pesa <br />RADA mlipiga pesa<br />KAGODA mlipiga pesa <br />DEEP GREEN mlipiga pesa <br />KIWIRA mlipiga pesa <br /><br />...., Leo mnatuletea habari za mchanga, sijui MAKINIKIA hapa.., wakati wapigaji ni ninyi wenyewe na hao makaburu wenzenu.., mnataka kutueleza nini.., habari za kujitekenya na kujichekesha wenyewe kaeni nazo wenyewe aisee.., msituchanganye!<br /><br /> LUGUMI wamepiga pesa.<br />TETEMEKO wamepiga pesa<br />LUCKY VICENT wamepiga pesa.<br />NIDA wamelamba pesa.<br />LUGUMI wamekamua pesa. <br />Eti wanataka watuchanganye kwa hivyo vikontena vya vumbi.?
 
If at all the government can not make total investigation on a particular citizen, like Lisu, then it is nothing rather than a mare institute!
 
Leo wakati rais Magufuli anapokea ripoti ya makanikia amesema kwamba walifuatilia mawasiliano ya mtu ambaye alikuwa anawasiliana na mtu anayeitwa Mwanyika na kumuomba data, hii maanake ni kwamba serikali kwa kushirikiana na kampuni za simu zinaingilia mawasiliano ya watu.

Kwa lugha nyingine ni kwamba mitandao ya simu inatoa siri za wateja wake kwa serikali aidha kwa hiari yao au kwa kulazimishwa, je uhuru wa faragha ya mteja upo wapi? Na kwanini mitandao hii inakubali kutoa siri za wateja wao kwa watu wasio husika, kuna haja ya kuendelea kuwa wateja wa mitandao hii inayotoa siri za wateja wao?.
Yaan wewe ulietoa post hii inabidi kwanza ufikirie mara 2 mbili...we unadhani ktk kufanikisha juu ya hili TCRA wanakaa mbali? PCCB je? Sasa unafikiri watajuaje kama kuna hujuma inataka kufanyika na ni nani anataka aifanye hiyo hujuma.....kwa upande wa pili, wewe bado ni kilaza hujajua mchango wa makampuni ya mawasiliano nchini....nikuulize swali! Kwan wew taarifa zako zilishawahi wekwa hadharani? Kama jibu ni HAPANA! Wew unadhani ni kwa nini taarifa zake zimewekwa hadharani?
 
Hajataja jina la mtu
Hajamtaja Lissu
Na inaonesha ni uongo maana kama ni kweli wangeweka hadharani mbona kina Kafumu wametajwa kabisa
Hakuna kitu hapo ni uongo tu mbona asimtaje,kila siku eti tunamuhifadhi
 
Sioni tatizo kwenye hili la ufuatiliaji wa mawasiliano ya baadhi ya watu kwenye vita hii iliyopewa jina la "vita ya kiuchumi".Mh.Rais anapaswa kuungwa mkono,lakini asijaribu kuuhadaa umma kwa kuwahusisha watu wasiohusika kwa namna yoyote ile na haya tunayoyapitia kama Taifa.

Nilimsikia akihoji kwa Uchungu kuwa " nani aliyeturoga?"Bila kupepesa macho,mchawi wetu siyo Tundu Lissu,Mruma wala Kafumu,Mchawi wetu ni ccm na serikali yake.Hawa ndiyo waliotufikisha hapa tulipo.Mikataba hii mikubwa inayolitafuna Taifa,ilisainiwa kipindi cha Mkapa na Kikwete.Hawa ndiyo waliobeba "tunguli za kuliloga Taifa letu kiuchumi"

Chini ya uongozi wa mkapa na kikwete,nchi yetu iliuzwa kwa kila aliyekuja kwa jina la uwekezaji.Wakati wanaoitwa wapinzani walipokuwa wanapigia kelele hiki kinachomliza Rais wetu leo,waliishia kubezwa na wengine walifukuzwa bungeni kwa mbwembwe na vifijo vya wabunge wa ccm wakiongozwa na spika wao.

Kama serikali ingeungana na mh.Zitto na Chadema kipindi kile walipokuwa wanaupinga mkataba wa Buzwagi/ACACIA uliosainiwa na Karamagi Hotelini London,yawezekana kilio hiki cha kuibiwa utajili wetu kisingekuwa hivi hivi leo,lakini wa upeo mdogo wa wabunge wa ccm akiwemo na mh.anayelia na kuomboleza leo,walimtimua Zitto na kubariki mkataba wa kinyonyaji uliosainiwa Hotelini.

Majuto ni mjukuu,suluhisho la haya yote ni kutengua kinga zinazowalinda watangulizi wake na awaburuze mahakamani wakashtakiwe kwa uhujumu uchumi,hao ndiyo waliotufikisha hapa,kusikitika na kulia huku ukikwepa kiini cha matatizo haya ni unafiki wa kiwango cha lami.
 
Back
Top Bottom