Mitambo ya Dowans sasa kuwashwa - Waziri Mkuu Pinda

Kama kweli nyie wazalendo basi mjue kuna zaidi ya Dowans inanitia shaka nadhani kuna kitu kwenye hii Dowans ndio maana ikitajwa wote mnaruka uwiiiii, jamani tumevamiwa na longo longo jingiiiii hamjengi haja za msingi kwanini Dowans isiwasheshwe. Pengine hamfahamu kuwa IPTL yenye mkataba wa miaka 20 ndio ni kampuni ya kufua umeme ghali maradufu ya Dowans mbona yenyewe mmeinyamazia? au yenyewe haikuingia mkataba na tenesco kwa kutumia hila? Sisi wananchi lazima tuwe na upeo wa kujiuliza mambo tusikurupushwe na wanasiasa kisha tukawa tunaitikia viitikio vyao.

Umeme wa Dowans lazima uwashwe ili kuwapunguzia makali wananchi! utasaidia kuongeza production viwandani! sioni tatizo la kuwashwa mitambo ya Dowans ikiwa maslahi ya taifa yataangaliwa upya katika huo mkataba mpya. Sitapenda kulalama na kuropoka mpaka pale nitakapojua IPTL, AGGREKO na SONGAS WASAFI kiasi gani.......

My take.

Tuache ushabiki wa kishamba tuchambue hoja ili kujenga hoja...............

IPTL iliingia wakati kikwete ni waziri wa nishati,DOWANS akiwa rais alafu mmiliki wake ni rafiki yake wa karibu na shemeji yake..connect the dots,.kama ulikuwa unajaribu kumdefend kikwete..umeshindwa,..kwani hatuwezi kukodisha mitambo mingine zaidi ya hii yenye utata,..hivi wewe hunusi ufisadi hapa??
 
Haya mambo tulishayaona mapema mwisho wake ndiyo maana wale walioporomosha matusi niliposema serikali iache unafiki ilipe deni la watu niliwashangaa kwa jinsi walivyokosa uwezo wa kuona mbali. Huoni sasa tunayarudia matapishi kwa aibu? usimtukane mkunga wakati uzazi ungalipo/!!!!!!!!!!:loco:
 
Mitambo iwashwe wananchi tupate umeme. Ambaye hataki asitumie umeme wa dowans. Acheni chuki za kike
 
Hili ni changa la macho.........

huyo stedishooooo wa bwana sharobaro c mpendiiiiiiiiiiiiiiiiiii mnafikiiiiiiiiiiiiiiiiiiii anajidai anauchunguuuuuuuuuuuu mtoto wa peasant kumbe maf........................ tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu,navyoamini hata mgao wa ememe tz wameucreate ili kuwafanya watz waumie then wakijapewa option ya dowans wakubali coz wamechoka na mgao, nasema hatukubaliiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii atakufa mtuuuuuuuu bora tubaki gizan tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu ka uchumi ufe tu mbon wanatudanganya sana eti umekuaaa huo uliokua upo wap kwa kupandishiwa naul na sukariiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, hatutakiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
 
IPTL iliingia wakati kikwete ni waziri wa nishati,DOWANS akiwa rais alafu mmiliki wake ni rafiki yake wa karibu na shemeji yake..connect the dots,.kama ulikuwa unajaribu kumdefend kikwete..umeshindwa,..kwani hatuwezi kukodisha mitambo mingine zaidi ya hii yenye utata,..hivi wewe hunusi ufisadi hapa??

Sijamtetea Kikwete ila nakushangaeni mnavyoshupalia Dowans haya tuseme ina utata hiyo mingine haina utata? mnaweza kufikiri nje ya box kwa dakika moja ua mbili? au mmeshalishwa kasumba haitoki vichwani!

Kikwete alikuwa waziri wa nishati lakini hakuwa mwenyekiti wa baraza la mawaziri na ieleweke pia kuna sehemu njilipata kusoma kuwa kuna rushwa ya dola 200,000 ilitolewa ili kufanikisha mkataba wa IPTL "sina uhakika" nani alipewa na ilikuwaje!
 
Mitambo iwashwe wananchi tupate umeme. Ambaye hataki asitumie umeme wa dowans. Acheni chuki za kike
Teh teh teh wakiwasha tu mitambo ya Dowans nitawaita Tanesco waje wang'oe waya zao na wachukue mita yao si ndio una amanisha hivyo? ina maana na viongozi wetu watakataa umeme wa Dowans?
 
Zamani katika baadhi ya makibila ya kiafrika mtemi akifa huwa alikuwa anazikwa na vijana wawili walio hai kuipakata maiti yake, na vijana hawa walikuwa wanajitolea kama mashujaa, ni bahati mbaya sana sijasikia wala kusoma majina ya waliodhani kufanya hivyo ni ushujaa kwenye historia tunasikiatu, Mtemi Isike, Mirambo n.k.hakika ulikuwa ni ujinga si ushujaa. Sasa wewe nakuona kama mmoja wa hao vijana ambaye anaishi enzi hizi. Hivi nikuulize kwanini usione Dowans ni kama starting point ya kuelekea kuuliza hayo mengine. Maana ya dowans yako wazi hata juha anaona hapa kuna walakini.

Mkuu vere simpo Dowans wakiwasha mitambo yao ili kuonyesha uzalendo unawaita Tanesco wanang'oa waya zao na kuchukua mita yao halafu unatafuta nishati mbadala.

Nadhani hii itaonyesha ni jinsi gani wewe si juha na mzalendo wa kupigiwa mfano....

Ni ushauri tu ikiwa unayoyaamini ni ya kweli unless kuna kaunafiki kwenye nafsi yako au huishi hapa nchini na huijui adha ya mgao wa umeme....
 
Acha wawashe mitambo ya Dowans kipindi hiki cha dharura lakin mkataba usiwe zaidi ya 12 months. Lakin kwenye kesi mwendo ni ule ule. DOWANS ISILIPWE
 
Wanaofahamu kama Mh. Sitta na Mwakyembe wameridhia haya maamuzi watujuze. Au maamuzi yataishia kwenye Bodi ya Tanesco ili kuwakwepa hawa wapambanaji kwenye Baraza la Mawaziri?
Wapambanaji hao wote wawili wameshatulizwa wamezibwa midomo hutawasikia:shut-mouth:
 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda leo ametamka rasmi kuwa TANESCO itaingia mkataba mpya na Dowans wa kuzalisha umeme.

Amesema mitambo ya Dowans itawashwa muda wowote kuanzia sasa licha ya kesi iliyopo mahakamani kuhusu tozo ya ICC.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuhutubia mkutano ulioandaliwa na The Economist kwenye hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam, Pinda alisema kuwa ni vyema SONGAS au kampuni nyingine binafsi inakununua mitambo ya Dowans siku zijazo ili iendelee kuzalisha umeme nchini.

Alisema hivi sasa kuna upungufu wa 160MW kwenye gridi, hivyo 100MW ya Dowans ingesaidia kupunguza makali ya mgao.

Pinda alisema serikali kununua mitambo ya Dowans imeleta maneno mengi kuwa haiwezekani serikali ikanunua mitambo iliyotumika, hivyo ameona suluhisho ni kwa SONGAS au mfanyabiashara mwingine mkubwa anunue mitambo ya Dowans na aingie kwenye mkataba wa muda mrefu na TANESCO wa kuzalisha umeme.

Tayari Baraza la Mawaziri limetoa kibali kwa TANESCO kuingia mikataba ya kukodi umeme kama ya Richmond/Dowans ili kupata 260MW.

Sasa hivi inasubiriwa bodi ya wakurugenzi ya TANESCO itoe tamko rasmi kuwa serikali itaingia mkataba mpya na DOwans.

Hivi hawa mafisadi wa DOWANS wataendelea kupora pesa za wavuja jasho wa Tanzania mpaka lini?

i give them no credit! wolves in the lamb's skin!!!!!
 
Haya niliyasema yatatokea na yametokea hivyo mjue kabisa kwamba siku zote mambo mengi huwa yanapangwa makusudi. Kama mnakumbuka wakati wa sakata la kununua mtambo wa Dowans lililoanzishwa na Zitto tukamkemea sana, rais Kikwete mwenyewealisimama na kutuhakikishia wananchi kwamba serikali haitanunua mitambo hiyo na badala yake serikali yake ilikuwa ktk harakati za kupata generator nyingine. Leo tuna mwaka na zaidi kilichofuata ni kuturudisha kule. kule tulikotoka.. Yaani tunalishwa chicha za kisiasa kwa sababu hao viongozi wenyewe wanajua Watanzania ni mazoba . Sasa niwapeni mpya nyingine. Huu mpango wa kuzalisha umeme wa dharura ulikuwa unalipiwa na wafadhili nadhani benki ya dunia kama sikose, na walichofanya hawa mafisadi walivuta fungu la fedha toka mfuko huo baada ya shirika au manispaa ya Houston, Texas kutoa generator hiyo kama msaada bure kwetu..ndipo mafisadi wakaunda shirika Richmond kisha hiyo Dowanskwa lakini ukweli ni kwamba mtambo tumeupata bure..na hatuna mahala pa kuutupa wala kurudisha,. maana fedha tulifadhiliwa wameisha kula na hawana ushahidi wa matumizi ya fedha za msaada waliopewa na wafadhili isipokuwa kuonyesha uhalali wa Dowans na kwamba generator hiyo ipo isipokuwa mkataba ndio pingamizi..kifupi tumiwaa.. Mimi ningependa sana mwanahabari yeyote amuulize Pinda, kwa miezi sita ya mwanzo wakati wa Richmond ni nani aliyekuwa akilipwa na serikali ikiwa shirika hilo halikuwepo?hiyo cheque yao ilikuwa deposited bank gani? na kwa nini tuliwalipa hata baada ya kugundua kwamba lilikuwa shirika feki na mkataba wenyewe ulikuwa feki..
 
Naona Bwana we unaelewa mambo yanavyo endeshwa na nyumba kwa mfano hizi za msoga zinazo ota kama uyoga kwenye kichuguu watazifanyaje? Au watazihamisha maana dunia ya sasa imeendelea bwana labda kumegunduliwa technologia ya kuibeaba nyumba na kuipeleka malaysia. Maana huwezi kunishawishi kuwa hizo si mali za kuwa frozen
Mpo wengi wenye mawazo ya kufikirika.
 
Mpo wengi wenye mawazo ya kufikirika.


Hata Khadaffi na Saif ukiwauliza watakujibu hivi hivi kama wewe, haya yanayo tokea libya niya kufikirika. Uzuri ni kuwa tanzania ya leo itabomolewa kwa matendo ya viongozi wake na wenye cha kupoteza zaidi ni haohao viongozi kwani wao ndio wanao faidi keki ya taifa zaidi ya mlalahoi. Naomba kutumia nafasi hii kukupongeza shujaa MS.
 
Hata Khadaffi na Saif ukiwauliza watakujibu hivi hivi kama wewe, haya yanayo tokea libya niya kufikirika. Uzuri ni kuwa tanzania ya leo itabomolewa kwa matendo ya viongozi wake na wenye cha kupoteza zaidi ni haohao viongozi kwani wao ndio wanao faidi keki ya taifa zaidi ya mlalahoi. Naomba kutumia nafasi hii kukupongeza shujaa MS.

Naona unachanganya mada nililocomment ni technology yako ya kuhamisha nyumba kupeleka nchi nyingine! Na kuhusu yaliyotokea libya na misri hapa kwetu bado sana labda hapa JF ndio tunaweza lakini sio nje ya hapa. Nadhani umenisoma!
 
Mkuu soma between the lines nauliza kwanini Dowans???????????????? kwanini sio IPTL yenye mkataba wa miaka 20 inayotutoza capacity charges mil 300 au Songas inayotulima capacity charges mil 265! au mikataba ya hayo makampuni ni fair na iliwekwa wazi tukaikubali??????

Kama huu ndio u great thinker then nadhani mie sina uwezo wa kufikiri...............

Siku njema na wewe mitambo ya Dowans na isiwashwe tule adha ya mgao au vipi?

Mkuu usione kwamba Watanzania walio nje na hata walio ndani ya nchi wanaohoji kuhusu huu mkataba haramu ili kuhakikisha Watanzania wanaendelea kutabika na matatizo ya mgao wa umeme na uchumi wa nchi kuendelea kuanguka kwa viwanda vingi na biashara nyingine kushindwa kufikia malengo yao ya kibiashara. Watanzania umefikia wakati wa kuachana na kutafuta short cuts ambazo hazitusaidii katika kutatua matatizo yetu mbali mbali. Hiyo Songa nayo pia ni madudu gesi yetu wenyewe halafu wanatulangua tena kwa $ hakuna wa kulaumiwa ni hiyo hiyo Serikali ambayo huwa inakurupuka tu bila kutafakari kwa kina na kuangalia nchi za wenzetu zinafanya nini wanapokuwa na rasilimali kama hizi.

Hili tatizo la umeme ni mwaka wa 19 sasa bado lipo tu mwaka nenda mwaka rudi na hakuna matumaini ya kulimaliza kabisa hivi karibuni. Hakuna anayejua upya wa hiyo mitambo haramu ya Dowans inawezekana kabisa mitambo hiyo ni michakavu na kesho, kesho kutwa baada ya kuwashwa inaweza tena kushindwa kufanya kazi na tatizo la mgao kurudi pale pale. Kinachotakiwa hapa ni kutafuta ufumbuzi wa kudumu ili kusiwepo tena na huu mgao kwa miaka chungu nzima ijayo badala ya tatizo kuendelea kujirudia kila mwaka kwa kufunika tatizo hili kwa short cuts ambazo hazitusaidii hata kidogo.

Sasa hivi kinachotakiwa kufanywa ni Serikali kununua mitambo yake yenyewe na kuikabidhi kwa TANESCO. Inaelekea hakuna tatizo la pesa maana walitaka kuharakisha malipo ya $94 kwa Dowans na pia kuna malipo mengine wa RITES ya $87 hizi pesa zinatosha kabisa kupata mitambo mipya na kulimaliza kabisa tatizo la umeme kwa miaka chungu nzima ijayo au kulipunguza kwa kiwango kikubwa sana.

Hizi short cuts (za kukurupuka tu na kutafuta solutions za matatizo yetu sugu kwa muda mfupi badala ya muda mrefu) tukiziendekeza zitaifikia nchi yetu mahali pabaya sana. Hakuna kuwajibika hata kidogo watu wanaharibu kila kukicha katika utendaji wao kama viongozi lakini hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi yao, mafisadi wa ndani ya nje ya nchi wanakupua mabilioni ya pesa za walipa kodi kwa mikataba haramu n.k. lakini hakuna hatua zozote za kisheria dhidi yao. Umefika wakati wa kusema sasa basi TUMECHOKA NA USANII wa kila leo.


 
Kuna mambo mawili hapa, kwanza kwanini IPTL na SONGAS wanalipwa ili hali tunajua kuwa wanamikataba yenye mashaka na utata kama Dowans? . Mi nadhani makosa mawili hayafanyi usahihi (two wrongs don't make one right). Kama yapo makosa huko nyuma na ambayo tunayajua na kuyahoji na tunayopaswa kuendelea kuhoji, hiyo haihalalishi Dowans kupewa upenyo.
Kwanini watu wameshupalia Dowans? Ni kwasababu ya usanii usiohitaji degree ya aina yoyote. Kama mmiliki na aliyepewa power of attorney wote waliikana kampuni iweje leo tuwaone mashujaa wa kutuletea umeme kwa usanii ule ule. Tunafahamu kuwa Richmond ndiyo Dowans kwa njia za usanii, na ni kwa kutumia hujuma za hawa watu kutaka kulazimisha miradi yao wanatumia mbinu chafu ambazo kama hazitakemewea basi tutafika kubaya. Mbinu za hujuma ilikulazamisha mradi wao ukubalike, ili tupandishiwe bei na kulipa hujuma zao.Kama hujuma zao zimefanikiwa kununua viongozi, si busara kukaa kimya ili hujuma hizo zinunue akili zetu pia.

Mvua za masika zaja na sijui mkataba wa miezi 3 au 12 utatusaidia vipi pale mabwawa yatakapokuwa yamejaa. Ni kwa usanii huu tutaendelea kulipa capacity charge kwa umeme usiozalishwa. Lakini la kujiuliza hapa ni kuwa kama serikali ipo tayari kulipa zaidi ya Billion 400 ya umeme wa mkataba, ilikuaje serikali hiyo isiweze kununua mtambo wake wa bei chini zaidi kwa sasa na kwa muda mrefu.!! Suala zima halipo kwa maslahi ya taifa bali kwa maslahi ya watu binafsi, na kama huu ndio unaoitwa wivu wa kike basi mimi naukubali.
Tumekuwa na mgao kwa miezi 3 sasa na hasara kubwa imepatikana kiuchumi na kijamii, sioni kwanini wakati huu mvua zinanyesha (hapa Dongobeshi hadi Babati na Dodoma) tukimbilie kumpigia magoti Al Aadawi na matapeli wenzake sisi kama taifa. Mimi naona hii ni kuwapa ushindi kwa bahasha zao kwa watu wachache, na ni aibu kwa tiafa la watu milioni 40.
Kwa namna yoyote iwayo sitakubaliana kuwa njia zinazotumika kumaliza tatizo hili ni muafaka na kwa maslahi yetu. Ni afadhali niwe na wivu wa kijinga au wa kike kama unavyoitwa, lakini nibaki nikiwa na akili timamu kuwa huu ni usanii na uhalifu nisiouafiki.
 
Sasa maadam kuna mikataba mingine yenye utata basi inatakiwa tukubali lolote tunalopewa hata kama ni endelezo la uvunjaji wa sheria?..Matatizo ya IPTL na Songas yanajulikana na yamezumgumziwa sana pamoja na kwamba serikali ilifunga masikio yake na kutupilia mbali madai ya wananchi. Hivyo hata swala la Dowans ni ktk mlolongo wa matatizo ya uongozi uliopo leo na bado yapo mengi yanafuata. Nyie mlokwisha tupa taulo zenu na kukubali matokeo kinawawasha nini hasa tunapopinga ufisadi kama sii kushabikia matumbo yenu wenyewe. Hamuwezi kutuambia ati maadam serikali ilifanya makosa na ufisadi mkubwa huko nyuma basi yanayofuata yote yakubalike, hii akili kweli ama ndio ile akili ya mke lazima awe bikira. Haya ni mawazo mgando kabisaaa na ndio maana nasema CCM itatawala milele.
 
uuuuuuuuuuuuuuwwwwwwwwwwwwwwwwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii uwi uwi

UUUUUUUUUUUUUUUUUwwwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii uwi uwi uwi twaaaaaaaaaaaaaaaafa jamani na MAFISADI! Bwana Yesu tuokoe na hili Genge la Mafisadi linalocheza na akili yetu. Tumeeeeechoka BWANA YESU TUOKOE NA HAWA WATU MAANA WANATUTESA WATANZANIA.

Amen and Amen.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom