Mwande na Mndewa
JF-Expert Member
- Feb 26, 2021
- 949
- 2,865
January na Maharage kwa miaka miwili wameshindwa kuendeleza hata mradi mmoja wa megawati 10 pale TANESCO, kila siku ilikua ni kukarabati mitambo, publicity na media coverage,Wameondoka hakuna legacy yoyote walioacha pale, wameshindwa kumaliza bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere kule Rufiji lililopaswa kuzalisha Megawatt 2100 aliloanza kulijenga Hayati Rais John Pombe Magufuli.
Ebu tujiulize;
Kwanini ZESCO wanazalisha umeme Megawati 3700 ama 3.7GW huku TANESCO ikizalisha umeme uziozidi megawati 1700.
- Tujiulize tena, kwanini Zambia watushinde na tulianza nao tulipoanza kujenga bwawa la Mwalimu Nyerere kule Rufiji, 2024 Zesco watawasha/commissioning umeme wa Solar wa Megawati 2,000 mjini Lusaka, sawa na Bwawa la Mwalimu Nyerere hapa Tanzania. Tanzania tunategemea Bwawa la Mwalimu Nyerere mwaka 2024.
Wakati Wazambia wakibuni na kuendeleza vyanzo vipya vya umeme kama Maji, makaa ya mawe nk. Tanzania haina mradi wa hivi karibuni wa kuzalisha umeme kwa miaka 2 ama 3 ijayo. Kama ipo badi hata kuanza bado.
Bei ya Umeme Zambia Tsh. 5000 ya Tanzania unapata karibu unit 98 na muda mwingine wanatoa Bonus zinafika 110 unapika kwa kutumia jiko la umeme na vitu vingine vipo unafika mwezi mzima kwa matumizi wanatushangaa huku kuwa Matumizi ya Umeme kuwa juu kama tupo Hong Kong, wanasema Tanzania maisha yapo ghali sana.
Je, ni kweli Tunduma watu wanapata umeme wa Zesco hawajawahi kukatiwa umeme kwa miaka mingi, hawajuikitu kinaitwa Ratiba ya Upungufu wala ukarabati wa mitambo?
Je, ni kweli Misenyi mnatumia Umeme wa Uganda mgao mnausikia kwenye mitandao?
Je, ni kweli Congo hawana mita! Umeme ukitoka kwenye nguzo unaingia ndani moja kwa moja?
ZESCO iliwahi kuwa na mkataba kama wa Tanesco na IPTL? Tanesco na Symbion? Escrow? Imewahi kutapeliwa na Wazambia?
Je, wakati sisi tunawaza kuwaleta IPTL, DOWANS, RICHMOND na Symbion wenzetu wakiwaz kujenga mabwawa ya kuzalisha umeme?
Shukrani Hayati Magufuli kwa kuweka kipaumbele kujenga bwawa la Mwalimu Nyerere kule Rufiji, 50-60% ya kazi zote za mwanadamu wa sasa ni umeme, hivyo nchi inahitaji kuwekeza kwenye umeme!
Tupate umeme wa uhakika halafu ndipo tuwaze mengine.
Ebu tujiulize;
Kwanini ZESCO wanazalisha umeme Megawati 3700 ama 3.7GW huku TANESCO ikizalisha umeme uziozidi megawati 1700.
- Tujiulize tena, kwanini Zambia watushinde na tulianza nao tulipoanza kujenga bwawa la Mwalimu Nyerere kule Rufiji, 2024 Zesco watawasha/commissioning umeme wa Solar wa Megawati 2,000 mjini Lusaka, sawa na Bwawa la Mwalimu Nyerere hapa Tanzania. Tanzania tunategemea Bwawa la Mwalimu Nyerere mwaka 2024.
Wakati Wazambia wakibuni na kuendeleza vyanzo vipya vya umeme kama Maji, makaa ya mawe nk. Tanzania haina mradi wa hivi karibuni wa kuzalisha umeme kwa miaka 2 ama 3 ijayo. Kama ipo badi hata kuanza bado.
Bei ya Umeme Zambia Tsh. 5000 ya Tanzania unapata karibu unit 98 na muda mwingine wanatoa Bonus zinafika 110 unapika kwa kutumia jiko la umeme na vitu vingine vipo unafika mwezi mzima kwa matumizi wanatushangaa huku kuwa Matumizi ya Umeme kuwa juu kama tupo Hong Kong, wanasema Tanzania maisha yapo ghali sana.
Je, ni kweli Tunduma watu wanapata umeme wa Zesco hawajawahi kukatiwa umeme kwa miaka mingi, hawajuikitu kinaitwa Ratiba ya Upungufu wala ukarabati wa mitambo?
Je, ni kweli Misenyi mnatumia Umeme wa Uganda mgao mnausikia kwenye mitandao?
Je, ni kweli Congo hawana mita! Umeme ukitoka kwenye nguzo unaingia ndani moja kwa moja?
ZESCO iliwahi kuwa na mkataba kama wa Tanesco na IPTL? Tanesco na Symbion? Escrow? Imewahi kutapeliwa na Wazambia?
Je, wakati sisi tunawaza kuwaleta IPTL, DOWANS, RICHMOND na Symbion wenzetu wakiwaz kujenga mabwawa ya kuzalisha umeme?
Shukrani Hayati Magufuli kwa kuweka kipaumbele kujenga bwawa la Mwalimu Nyerere kule Rufiji, 50-60% ya kazi zote za mwanadamu wa sasa ni umeme, hivyo nchi inahitaji kuwekeza kwenye umeme!
Tupate umeme wa uhakika halafu ndipo tuwaze mengine.