Missed call ya shemeji

Missed call ya shemeji

MH! MISSED CALL YA SHEMEJI!-8

ILIPOISHIA
Nawewe unayaweza mama najuta kumfahamu mdogo wako kabla yako, wewe ndiye ulipaswa uwe mke wangu, unipikie, unifulie, uniogeshe na unifanyie mambo mazuri kama haya kila ninapohitaji. Beka alimwambia shemejiye, wakachela
"Mimi naona hujaamua tu kufanya hivyo…hata leo ukitaka kumuacha yule chakubimbi wako unaweza…tena ukimuacha nitafurahi sana," shemeji yake alimwambia Beka.
SASA JIONGEZE MWENYEWE…


"Mimi naweza kumfanyia mizengwe mpaka akimbie halafu uchukue nafasi yake tule nanasi kwa nafasi na si kwa kujibanabana!" Beka alimwambia shemeji.

Baada ya kutoa kauli hiyo, shemejiye alikenua meno yote thelathini na mbili nje, akamkumbatia Beka, akambusu midomoni, mume huyo wa mdogo wake akachaji tena, akampa mambo.

Walipomaliza kufurahishana, waliingia bafuni wakaogeshana, wakavaa nguo ndipo Beka akamshauri shemejiye huyo abaki pale kwa muda ili yeye atangulie nyumbani.

Kufuatia shemejiye huyo kufurahishwa na penzi tamu la mume wa mdogo wake, hakuwa na neno alimruhusu kiroho safi, walibusiana na Beka akashika njia kuelekea kwake.

Alipofika alijifanya kushtuka kumkuta mkewe akiwa amejikunyata nje, akamuuliza kulikoni?
"Kila nikikuambia dada yangu hajatulia ndiyo maana kaachwa na mumewe unakuwa upande wake, sasa kaondoka hapa nyumbani bila kuaga mbaya zaidi kaenda kwenye michepuko yake na funguo," mke wa Beka alimwambia mumewe.

"Inamaana umetafuta kila mahali hujaziona?" Beka alimuuliza mkewe.
"Ndiyo maana yake, wewe unafikiri mimi napenda kukaa hapa nje?" mkewe alimuuliza.
Baada ya Beka kuambiwa hivyo, alijongea kwenye zulia la mlangoni akalifunua na kutoa funguo, mkewe akapigwa na butwaa.

"Si huu hapa," alisema Beka akimwonesha mkewe.
"Khaa! Au we ulijua funguo iko hapa nini? Mliwasiliana au mlikuwa wote?" aliuliza Aisha huku akimwangalia mumewe kwa macho yaliyojaa maswali kibao na mshangao juu…
"Hapana, huwa najua wengi wanapoondoka majumbani kama kuna wengine watakuja funguo wanaweka chini ya kapeti, we hulijui hilo?"

"Mimi silijui hilo, nina wasiwasi kwamba huenda alikwambia au mlikuwa pamoja."
"Hapana mke wangu. Mimi nilijaribu tu. Labda kesi ya msingi kwake iwe ya kumpigia simu halafu hapokei na kama atakuja itabidi nimpe masharti ya jinsi ya kuishi hapa nyumbani kwangu, anatakiwa kufuata sheria za hapa na si vinginevyo anavyotaka yeye."

Kwa maneno hayo ya mume wake, kidogo Aisha alionekana kuelewaelewa, lakini kabla hajafumbua kinywa, dada yake aliingia…

"Dada ulikuwa wapi na kwa nini nakupigia simu hupokei wakati unajua funguo umezificha mahali?" Aisha alikuja juu…

"Sasa kama funguo ningekuwa nimezificha kweli ningewakuta ndani?"
"Hayo ndiyo majibu yako dada angu?"
"Umeyataka mwenyewe Aisha, kuniuliza ."

Beka alipopata nafasi ya kukaa peke yake alianza kumwona shemeji yake ni tatizo kwani hata kama kweli wanaiba lakini ni kwa nini dada mtu amseme vibaya mdogo wake?
"Kwanza ilitakiwa awe mtulivu sana na mpole maana yeye ni dada mtu, angekuwa mdogo mtu ndiyo anafanya hivyo sawa," aliwaza sana Beka.
***
Mwezi mmoja na nusu mbele, siku hiyo shemeji mtu huyo alimtumia meseji shemejiye Beka akimuuliza kama wanaweza kuonana…

"Kuna nini kwani dear?" aliuliza Beka…
"Kuna kitu kizuri sana nataka kukwambia mpenzi wangu jamani."
"Kama nini?"

"He! Kwani hutaki kukutana na mimi siyo?"
"Niko tayari, ila wewe tu. Ninyetishie basi."
"Nikunyetishie nini bwana, we tulia. Niambie tuonane wapi?"
"Basi jioni ya saa kumi, palepale pa juzi."

"Sawa, pale ni mwao najua na mambo mengine nitapata."
"Acha mambo yako wewe! Mambo kama yapi?"

"Si yale baby bwana na wewe, unajifanya hujui siyo? Unajua kila nikikumbuka tulichoofanya kwenye sita kwa sita kule gesti damu zinanikimbia kwa sana mwilini, natamani tena iwe sasa hivi."
"Teh! Teh! Teh!" Beka aliishia kucheka kwenye meseji kisha akamwambia shemeji yake…

"Lakini mke wangu unazifuta hizi meseji au unaziacha ili uziangalie kama shoo ya muziki?"
"Aaa mume wangu bwana! Ina maana mimi ni mtoto mdogo kama mkeo?"
***
Muda wa ahadi ulifika, dada wa Aisha alijiandaa akaondoka akiwa ameweka funguo chini ya kapeti kama alivyofanya siku ya kwanza.

"Na leo kama atarudi na kutoziona funguo itakuwa shauri yake...ngoja nikampe raha mumewe, mjini hapa ukilala wenzako hatulazi damu," dada wa Aisha alijisemea moyoni wakati akielekea katika gesti waliyokuwa wakikutania na Beka.

Akiwa anaelekea huko gesti, alimtumia meseji Beka naye akamwambia achukue chumba akifika atalipa. Baadaye Beka naye alifika, akalipia chumba.

Ndani ya chumba, Beka alipokelewa na mabusu kibao huku shemeji yake huyo akimchagiza na maneno ya nakupenda sana baby, sitaki kukupoteza na mengineyo mengi yenye kujazwa na mahaba.
"Mimi pia baby…mimi pia baby," ndiyo yalikuwa majibu ya Beka kwa shemeji yake huyo.

"Enhe, katika yote tutakayoyafanya leo au muda huu kwanza nataka uniambie hicho ulichoniitia."
Shemeji mtu huyo alicheka kwanza kisha akawa siriasi, akafunguka …
"Baby nimenasa."

Beka kwanza hakuelewa, akahisi kama alichokisikia amekitafsiri vingine, akamuuliza…
"Unasema?"

"Nasema mwenzio nimenasa ujauzito, maana nimepitiliza."
"Una maana gani?"
"Nina ujauzito wako bwana, acha mambo yako wewe."
 
MH! MISSED CALL YA SHEMEJI!-9

ILIPOISHIA
"Nasema mwenzio nimenasa ujauzito, maana nimepitiliza." "Una maana gani?"
"Nina ujauzito wako bwana, acha mambo yako wewe." SONGA NAYO…

He! Shemeji! Una nini wangu?"
"Ujauzito."

"He! Kwa hiyo?"
"Kwa hiyo nini shemeji, wewe si ndiye mhusika!"
"Ina maana upo tayari kuzaa?"
"Tatizo liko wapi?"
"Kuzaa na mimi?"
"Mimi sioni shida."

"Ukitoa mtoto yupo kama mimi mtupu?"
"Haiwezekani hata siku moja."
"Mh! Hapana, tutoe shemeji."

"
Kutoa! Sisi tuliapishwa na baba, mtu akipata mimba akitoa anakufa, hajakwambia mkeo?" alisema dada wa Aisha huku akijing'atang'ata midomo.
Beka hakuwa tayari kuzaa na shemeji yake huyo hata kama walikubaliana kula uroda. Kwake kuzaa na shemeji yake ilikuwa ni kupitiliza kwa kufuru jambo ambalo aliamini linaweza kumpa wakati mgumu katika maisha ya kifamilia…

"Yaani shemeji itakuwa ngumu sana wewe kuzaa na mimi halafu…"
"Hata mimi itakuwa ngumu sana kutoa hii mimba. Hivi kama ulikuwa hutaki kuzaa na mimi kwa nini hukuniambia mapema?"
"Shemeji kwani hukujua?"
"Kwamba?"

"Mimi na wewe hatuwezi kuzaa!"
"Tunaweza, sii hutaki! Au hatuwezi kivipi wakati mimi tayari nina mimba yako."
Beka aliangalia pembeni, shemeji yake akamfuata na kumshikashika sehemu mbalimbali za mwili na kumfanya Beka kusisimka…

"Una…jua she…m tati…zo wewe hu…jui tu, mdo..go wako…ana…" alisema Beka huku akisisimka mwili kutokana na kushikwashikwa na shemejiye mwilini. Alihisi kuchanganyikiwa.

Shemeji mtu huyo naye alijua Beka ameshaingiliwa akili hivyo akazidisha kujituma ili kuingia kwenye hatua nyingine na kuisahau ile ya kwanza ya madai ya mimba…
"Shemeji…"
"Mmh!" Beka aliitika kwa sauti ya chini sana huku macho yakiwa hayaoni sawasawa.
"Unataka nini?"

"Unataka unipe nini wewe?"
"Chochote unachokitaka wewe."
"Sawa na wewe nipe chochote unachotaka kunipa."
Mazungumzo yote hayo yaliendelea huku kila mmoja akiwa tayari amewaka moto, hakuna kitu mbele yao zaidi ya mahaba.

Shemeji alimvua nguo Beka huku wakiendelea kusemeshana maneno mbalimbali yenye kuhamasishana zaidi kimahaba mpaka wakajikuta wote hawana nguo kitandani wakaingia mechini..!

***
Ilikuwa siku ya Jumapili, Aisha alikuwa nyumbani, mumewe pia. Aisha alikuwa akizungumza na mumewe kuhusu mambo mbalimbali ya maisha, ghafla dada wa Aisha alikatiza mbele yao akitokea chumbani kwake kwenda bafuni huku akikimbia akiwa amejishika tumbo na kujipigapiga kifuani kama vile anasikia maumivu…

"Dada nini tena?" Aisha aliuliza akimfuatilia kwa macho.
Beka moyo ulimlipuka, alijua tayari kinakaribia kunuka kwani dalili zile za shemeji yake ni za ujauzito wa wazi kabisa…

"Ngoja niende nikamcheki dada," alisema Aisha.
"Ukamcheki nini sasa wakati mtu mwenyewe anaonesha hataki kusema?"

"
Atasema tu, si ajabu anaumwa sana."
Aisha alikwenda bafuni akakutana na matapishi kibao huku dada yake amechuchumaa…
"Dada, ni nini?"
"Naumwa."
"Nini zaidi?"
"Nahisi malaria."

"Malaria au mimba dada?"
"Malaria, mimba niitoe wapi mimi?"
"Dada angalia sana na safarisafari zako hizo, kapime dada."
"Aisha, mbona unanikosea adabu dada yako. Maswali gani hayo kwangu?"
"Sahamani sana dada," alisema Aisha huku akiondoka kurudi sebuleni.

***
Usiku wa manane, Beka aliamka na kukosa usingizi kabisa. Akaanza kukumbuka picha ya shemeji yake kupita mbio mbele yake na kukimbilia bafuni. Akakumbuka maneno ya mke wake baada ya kurudi bafuni…
"Ana nini?"

"Mh! Mi nahisi ni mjamzito huyu!"
"Yeye kasema mwenyewe?"
"Hajasema, anasingizia homa."
"Labda ni homa kweli."
"Homa si angetapika nyongo, huyu kanasa. Na hii yote ni matokeo ya safari zake za kutoeleweka, yamemkuta sasa."

"Da! Shemeji naye kumbe yupo?"
Beka alijikuta mapigo ya moyo yakimwenda kwa kasi ya ajabu…

"
Ile mimba lazima itoke. Nikisema iendelee kubaki nitaumbuka," Beka alijikuta akisema kwa sauti…
"Unasemaje Beka?" mkewe alimuuliza kwa sauti iliyotoka kuamka ghafla.
"Aaa! Nilikuwa naota tu."
"Sasa kama kuota ndiyo unaota mimbamimba?"
"Sijaota mimba, nimeota miiba. Nimeota kuna rafiki yangu amechomwa na miba, sasa anataka kutolewa."

"Tuambiane mwenzetu maana tayari humu ndani tuna mjamzito, isijekuwa unamuotea yeye."
"Aaah! Wapi! Yaani mimi niote ndoto ya mtu mwingine?"
"Kwani haiwezekani?"

Mara simu ya Beka ilitoa mlio wa meseji kuingia, Aisha akashtuka na kuuliza…
"Nani huyo saa hizi?"
Beka pia alishtuka. Alijua kwa swali la mkewe ina maana akishaisoma meseji hiyo lazima aseme ni nani kaituma. Sasa je, kama itakuwa imetumwa na shemeji mtu?
"Sijui nani?" alisema Beka akitaka kupotezea kusoma…

"Hebu msome tumjue huyo anataka nini usiku huu na waume za watu?"
 
MH! MISSED CALL YA SHEMEJI!-10

Beka, licha ya kujibalaguza ilifika mahali akajua amekwisha. Akili za haraka zilimwambia kwamba katika uzoefu wa kawaida, haijawahi kutokea akatumiwa meseji usiku na mtu, kwa hiyo aliamini ni dada wa mkewe tu huyo.

"Soma basi," alirudia Aisha.
"Kaka Beka mambo? Asubuhi pitia kwa mzee Ismail uchukue ule mzigo wako. Mimi wajina."
Beka alisoma meseji ya uongo kwa kuitunga kutoka kichwani kwake, mkewe akaamini lakini akamuuliza…

"Ni mzigo gani kwani?"
"Kuna boksi la tende."
"Ooo! Halafu jana huyo wajina wako nilikutana naye pale msikitini, akasema nikupe hai."
"Okey."

Beka alipoisoma ile meseji sawasawa, iliandikwa na shemeji mtu na ilikuwa ikisema…
"Piga ua galagaza, alfajiri njoo chumbani uniamshe na joto lako tamu! Mwaaa…"

Kichwani alikasirika kidogo kwa vile aliamini shemeji yake huyo ana akili timamu kwa hiyo alijua ubaya wa kutuma meseji kama ile usiku tena akiwa kitandani na mke wake.
"Kichaa sana huyu shemeji," alisema moyoni.
***
Saa kumi na moja na nusu, Beka alitoka chumbani kwake akiwa ndani ya bukta tu hadi sebuleni. Aliangalia kulia na kushoto na kubaini hali ya utulivu na amani, akanyata kwenda kwenye mlango wa chumbani kwa shemeji yake…

"Sijui mlango uko wazi?" alijiuliza baada ya kuufikia mlango huo. Alisita kwa muda mrefu hapo mlangoni kama vile alikuwa akijua ndani kuna mwanaume mwingine sasa alikuwa akimsikilizia.

"Lakini ni kwa nini moyo unasita sana kuingia? Kuna balaa nini? Na kama kuna baya ni kutoka kwa nani sasa? Mimi nadhani nisiingie," alisemasema mwenyewe pale mlangoni lakini moyo wa kuingia ukashinda, akafungua mlango na kuzama chumbani.

Shemeji mtu alishtuka kuona mlango umefunguliwa, akainuka kutoka kitandani na kukaa kwa kunyoosha miguu."Afadhali umekuja, baridi sana," alisema shemeji mtu huyo huku akiwa hayumo ndani ya shuka wala kanga halafu eti anasema kuna baridi! Kivipi? Ilikuwa ni zaidi ya baridi.
Beka alipanda kitandani huku akisema…

"Lakini shemeji leo nimekuja huku najisikia uvivuuvivu sana, sijui kwa nini?"
"Hamna bwana, wewe unataka kuninyima joto," alisema shemeji mtu huku akimparamia mume wa mdogo wake maana alianza kuhisi anamtolea visingizio ili amwache na njaa yake.

Walilala kiubavuubavu wakiangaliana. Wakaanza kushikanashikana mwilini huku wakinong'onezana maneno ya mahaba kama vile wao ni wana ndoa tena wako wenyewe tu.
Shemeji mtu ndiye aliyetangulia kupata moto wa mahaba, akamvutia kwake kijana huyo, wakaingia uwanjani na kuianza mechi kwa kasi na standadi.

Dada wa Aisha ilikuwa kama amedhamiria kumjulisha mdogo wake nini kipo kati yao kwani aliweweseka kwa sauti hadi kufumbwa mdomo ili sauti hiyo isitoke nje.
"Sasa shemeji kama ukisikika itakuaje? Si atakuja huku na kutukuta?" Beka alisema.

"Na mimi si mimi bwana, ni munkari wa mahaba umenipanda mwenzio."
Maneno hayo pia aliyasema kwa sauti licha ya kwamba Beka alimtaka asipige kelele.
***
Aisha alishtuka kitandani na kukuta kweupe. Alishangaa!
"Huyu ameshaamka?" alijiuliza.

Alitega masikio ili kusikia kama mumewe aliingia chooni maana chumba chao kilikuwa ‘self contain'. Ukimya ulitawala hali iliyoashiria kwamba hakuwemo mle bafuni wala chooni…
"Baby…baby," alijaribu kuita kwanza ili kujiridhisha.

Akatoka kitandani na kuifuata simu yake kisha akaitupia macho…
"Mh! Saa kumi na mbili na dakika tatu. Mbona si kawaida yake saa hizi awe nje!"
***
Beka na shemeji yake walipitiwa usingizi baada ya mzunguko wa kwanza wa mechi, wakalala kabisa. Hakuna aliyekuwa na habari na dunia inakwendaje!
Baby," Aisha aliita sasa akiwa amefika sebuleni ambapo hakuona dalili yoyote kwamba mumewe alifika hapo…

"Baby," aliita kwa sauti ya juu sasa, akashtuka kutoka kwenye chumba cha shemeji yake. Kidogo aitikie ‘sema', kushtuka hivi kumbe alikuwa kwenye mchepuko.

"Mh! Shemeji tumefumwa," alisema Beka, shemeji yake naye akashtuka…
"Mungu vile tumefumwa," alisisitiza akitoka kitandani. Akavaa bukta yake na kwenda kuushika mlango. Aliposikia sauti inatokea sebuleni alirudi, akajishika kichwa na kuanza kujuta…

"Nilisema mimi, dalili zilishaonesha kwamba kuna balaa. Ndiyo hili sasa."
"Beka," Aisha aliita tena, sasa alibadili jina.

"Shemeji ingia chini ya kitanda," shemeji mtu alimwambia Beka huku akifunua godoro, akabinyua chaga za upande mmoja. Beka alizama ndani yake, ile anamalizikia tu, Aisha akagonga mlango…
"Dada," aliita kwa sauti iliyojaa utulivu.

Dada yake alirudisha chaga polepole kisha akafunika godoro vizuri na kurudishia shuka kama awali…
"Dada."
"Ee."

"Samahani, nina shida."
Dada mtu huyo alifungua mlango na kusimama katikati akijifanya hajui shida ya mdogo wake…

"Beka simwoni humu ndani dada."
"Ndani wapi?"
"Chumbani. Nimekuja sebuleni hayupo, nimekwenda bafuni, chooni kote hayupo."
"Kwa hiyo yuko kwangu siyo?"

"Sina maana hiyo dada. Kwani we huoni kuwa ni tatizo? Nimekwambia ili tusaidiane kujua alipo."
"Ohoo! Nilidhani unamaanisha yuko kwangu. Maana umesema sehemu nyingi umemwangalia hayupo. Nikasema makubwa! Kwani ametokaje?"
"Nadhani mimi nilikuwa sijaamka."

"Simaanishi hivyo, namaanisha alipotoka amevaa nini?"
"Naamini ametoka na bukta tu, maana haipo na ndiyo huwa anaivaa anapokuwa amelala. Mimi nahisi hajatoka nje ya nyumba hii."
"Unarudi palepale. Unaposema hivyo atakuwa wapi kama si kwangu sasa?"
"Dada tuyaache hayo, tumtafute."
"Simu yake?"

"Simu kaizima, ipo chumbani."

***
Kule chini ya kitanda, Beka alianza kupata maumivu kwani alijipinda sana kutokana na ufupi wa kitanda kiasi kwamba hakuweza kulala kwa kunyooka."
"Da! Ukisikia mateso ya kujitakia ndiyo haya. Sasa hapa kisa nini? Lakini kwa namna nyingine kisa ni yeye mke wangu na ugumu wake wa kunipa haki yangu."

***
Dada mtu alichukua kanga nyingine kutoka kwenye msumari nyuma ya mlango, akajifunika juu na kutoka. Lakini alipotoka tu, Aisha alinyoosha mkono akachukua funguo kwa ndani na kuufunga mlango huo kwa nje…
"Sasa tunaanzia wapi?" aliuliza dada mtu akiwa ameshafika sebuleni sasa.
"Humuhumu ndani dada."
"Uani ulikwenda?"
"Sijaenda."

"Sasa kwa nini usiende. Kule si ndiyo anaweza kuwepo maana ya Mungu mengi."
Aisha alikuwa kama hamuelewielewi dada yake kwa kauli zake. Mara aseme ‘kwa hiyo yupo humu kwangu?' mara ‘ya Mungu mengi.'
"Dada unaposema ya Mungu mengi una maana gani?"
"Nina maana labda yuko uani."

"Sasa atakwenda kwa njia gani wakati mlango umefungwa? Kama alitoka uani nani alifunga mlango kwa ndani baada ya yeye kutoka na humu ndani niko mimi, wewe na yeye tu?"
"Kwa hiyo bado una maana ni mimi nilifunga mlango baada ya yeye kutoka si ndiyo?"
"Ha! Dada bwana! Sina maana hiyo mimi."
"Sasa maana yako ni nini we Aisha?"
"Mbona una hasira dada?"
"Hata ungekuwa wewe ungepata hasira."

***
Kule chumbani, Beka alijua kwamba shemejiye na mkewe wametoka kwenda kumtafuta, akasukuma chaga kisha akatoka, akazirudisha vilevile. Alisimama chumbani humo na kuangaza huku na kule. Alijua akitoka atakutana nao. "Huyu mwanamke hajui kama niliwahi kupitia mafunzo ya kijeshi, sasa tangu lini askari anaweza kufumaniwa kirahisirahisi, mimi ndiyo Beka bwana nimezaliwa mjini na kukulia mjini!" Beka alizungumza moyoni kisha akapanda kwenye dari.

Alipozama, akarudishia mfuniko, akatambaa kwa upole akikumbuka kwamba, kuna mfuniko mwingine kwenye bafu chumbani kwake. Alifanikiwa kushukia huko bafuni ambapo alisimama kwa muda akihema kwa sana. Alivua bukta na kujimwagia maji.

Mlio wa maji bafuni ulimshtua Aisha, akaenda mbio chumbani na kumkuta mumewe anaoga…
"Beka," aliita Aisha kisha akatoka mbio kwenda chumbani kwa dada yake akijiuliza ataukuta mlango ukiwaje? Alishangaa kuukuta umefungwa kwa funguo nje lakini pia bado alijua kama mumewe angekuwa humo, asingeweza kutoka mpaka afunguliwe kwa nje na ndiyo maana yeye alifunga.

Alirudi tena hadi chumbani. Wakati huo dada yake alikuwa sebuleni akimshangaa. Alipokwenda chumbani kwake, dada mtu huyo alishangaa kukuta mlango umefungwa kwa nje na funguo ikining'inia. Akazama ndani na kuinua godoro hakumwona Beka!
"Mh! Huyu vipi? Yaani ametoka akaamua kuufunga mlango kwa nje? Mbona balaa, mkewe atajua," alisema moyoni.

Hakujua kama mlango huo ulifungwa na mdogo wake.

***
"
Ulikuwa wapi Beka?" aliuliza Aisha kwa sauti iliyopandwa na midadi…
"Chooni."
"Una uhakika?"
"Ningekuwa sina uhakika ningekwambia sijui nilikokuwa."
"Mimi nimeita sana hukuitika. Bafuni nimekuja sijakuona."
"Ulitaka niitike nikiwa chooni?"

Aisha alikosa jibu la moja kwa moja. Alitoka mpaka sebuleni na kumjulisha dada yake, alipomkosa akaenda chumbani na kumwambia kwamba, mumewe kumbe alikuwa chooni na sasa ametoka yupo bafuni anaoga.
"Kwa hiyo hakupotea kama ulivyokuwa unaamini?" aliuliza dada mtu huyo.
"Inawezekana."

***
Kulikucha, dada mtu huyo akawa na dukuduku la kutaka kujua shemeji yake alitokaje ndani ya chumba hicho mpaka mkewe akaamini? Akawa anamtafuta aongee naye kabla hajaenda kazini.
 
MH! MISSED CALL YA SHEMEJI!-11

ILIPOISHIA
Uzuri wake, dada mtu huyo alipoona simu ya Beka hakuminya batani yoyote ile ya simu yake hivyo ilionekana kweli hakuiona.
Dada huyo hakuwa na sababu ya kwenda kwenye meseji, akaiweka simu kitandani…
"Dada…"
"Abee."
SASA JIMWAGE MWENYEWE…


asa dada mtu alianza kuwa mpole fulani hivi aliitikia kwa upole. Yeye alijua dada yake ameona meseji zake kwa mumewe maana hajawahi kufuta.

"Beka na wewe mkoje? Niambie ukweli dada yangu."
"Sisi?"

"Ninyi ndiyo, si ndiyo nakuuliza wewe!"
"Hatuna ugomvi mbona!"
"Sijasema mna ugomvi dada, ila nahisi kama mienendo yenu haiko sawa."
"Kivipi mdogo wangu Aisha?"
"Kwa nini akubipu?"

"Sasa hilo ungemuuliza wewe mumeo kwa nini alinibipu wakati mimi sibipiki."
Aisha alishindwa kujizuia, akajikuta akicheka mwenyewe kwa majibu ya dada yake kule kusema ‘mimi sibipiki'.

Alisimama akaondoka kurudi chumbani kwake akiwa na mawazo sana.
Alikaa kitandani, akajiinamia akiwaza mambo mbalimbali kuhusu dada yake na maneno yake…
"Lakini iko sababu ya kuangalia vizuri ukaribu wa Beka na dada, mimi kama siuelewi. Juzi Beka ametoka chumbani asubuhi, nimemtafuta kote hayupo, eti mwisho nakuja kumwona akiwa bafuni. Inawezekana kweli?"

"Haya, leo tena ndiyo hivyo. Namtafuta kote, baadaye eti alitoka uani na dada nakutana naye anatoka chooni! Mh! Hapa naweza kuliwa bila mwenyewe kujijua," aliwaza sana Aisha kisha akapanda kitandani kulala akiwa ameamua jambo moja moyoni mwake.

***

Asubuhi kulipokucha, Aisha alitoka kwenda jikoni, akamkuta dada yake ameshaamka amebandika maji kwenye sufuria kubwa…
"Maji anaoga nani dada?" Aisha aliuliza.
"Hiyo ndiyo salamu mdogo wangu?"
"Ah! Sorry, shikamoo."

"Mumeo haogi leo?" Dada mtu huyo alidakia mambo mengine badala ya kujibu salamu hiyo.
"Alikwambia anaoga maji ya moto? Maana mi sijawahi kumwona au kumsikia akioga maji ya moto hata siku moja."

"Basi mjaribu kumtengea leo uone kama atachomoa."
Aisha hakuongeza maneno, aliendelea na mambo mengine huku akiwa hana amani ya moyo.
"Lazima kuna kitu, lazima kabisa," alisema moyoni Aisha.

Siku hiyo mumewe Beka alikuwa ameanza likizo ya siku ishirini na nane kazini, kwa hiyo alikuwa haendi kazini lakini yeye Aisha alitakiwa kwenda kwenye biashara yake.
Nyumbani alimwacha dada yake na mumewe lakini wakati anaondoka aliuliza…
"Darling leo utatoka?"

"Yeah, baadaye sana lakini."
"Utaenda wapi?"
"Misele yangu tu."
"Oke, nilitaka kujua tu," alisema Aisha na kutoka zake.

***

"Baby vipi?" Dada mtu alimsemesha Beka shemeji yake kwa sauti yenye mvuto wa kimahaba.
"Poa, niambie."
"Nimefurahi sana."
"Kwa nini?"
"Kuwepo nyumbani leo. Najua leo ndiyo ile ndoto yangu ya mimi kuwa mke, wewe mume itatimia."
"Utaitimizaje?"

"We utaona mwenyewe."
Dada mtu huyo akaondoka kwenda jikoni ambako alikaanga mayai manne, akatengeneza na kachumbari kwa pembeni kisha akampelekea Beka mezani akiwa ameambatanisha na maji ya kunawa yenye uvuguvugu…

"Mh! Hii kali leo, ndiyo kifungua kinywa au?"
"Kifungua kinywa kinakuja mume wangu wala usijali. Mimi ni mkeo na wewe ni mume wangu."
Beka alicheka tu huku akimkazia macho shemejiye wakati anaondoka kwenda jikoni. Alivaa gauni la kawaida na juu yake akatupia khanga moja.

"Da! Si mchezo," alisema moyoni Beka akijiweka vizuri. Tayari mwili ulishaanza kusisimka kwa kuona tu na kuvuta picha anavyokuwa naye kwenye uwanja wa sita kwa sita.
"Huyu dawa yake ni kufunga milango mchana kutwa, mpaka ikifika jioni mdogo wake anarudi, sisi hatuna hamu tena," aliendelea kujisemea mwenyewe moyoni mwake.
Mara, sinia ilifikishwa mezani, ndani yake mlikuwa na chai ya maziwa na soseji mbili, akatengewa na kukorogewa…

"Karibu mume wangu mpendwa," alisema dada mtu.
"Ooo! Asante my wife. Kweli wewe ni mke mwema,"
"Umeona ee? Wengine watasubiri."
"Watasubiri sana tu."
Beka aliipiga chai hiyo nzito, alipomaliza alisimama kumfuata shemeji yake chumbani ambapo alimkuta ametoka kuoga sasa anajifuta maji kwa upande wa khanga…
"Karibu baby."

"Asante, nimekumisi sana ndiyo maana nimekuja."
"Mimi je? Hivi hapa nilikuwa navaa ili nije unitendee haki."
"Kwa hiyo nikakusubiri sebuleni," alisema Beka huku akimshikashika shemeji yake sehemu mbalimbali za mwili hali iliyomfanya atoe mlio wa kama mtu anayetoneshwa.
Aliacha kuendelea kujifuta na kumgeukia Beka, wakatazamana kwa macho ya kurembua huku wote wakianza kuhema.

***

Aisha alipofika nyumba ya nne aliingia kwa rafiki yake mmoja aitwaye Diana. Akamsimulia hali ilivyo nyumbani kwake na kile anachokifikiri…

"Hivi hapa siendi kwenye shughuli zangu, baada ya nusu saa narudi, najua tu kama kuna kitu nitawakuta katika mazingira tata," Aisha alimwambia Diana.

ITAENDELEA ALFAJIRI.........
 
Dizaini kama part ya 10 kwenda ya 11 kuna kipande cha stori kimekosekana...

Ndugu msimulizi hebu tazama kwa makini...
 
Dizaini kama part ya 10 kwenda ya 11 kuna kipande cha stori kimekosekana...

Ndugu msimulizi hebu tazama kwa makini...
Asante kwa kufuatilia mkuu, kwema lakin
 
MH! MISSED CALL YA SHEMEJI!-12

ILIPOISHIA
Aisha alipofika nyumba ya nne aliingia kwa rafiki yake mmoja anaitwa Diana. Akamsimulia hali ilivyo nyumbani kwake na kile anachokifikiri…
"Hivi hapa siendi kwenye shughuli zangu, baada ya nusu saa narudi, najua tu kama kuna kitu nitawakuta katika mazingira tata," Aisha alimwambia Diana.
JIACHIE MWENYEWE…


"Mh! Makubwa shoga. Hata mimi naungana na wewe, nenda kwa siri, fika kwa siri na chunguza kwa umakini, kama kweli wana lao jambo lazima utaliona," alisema Diana.

***
Beka na shemeji yake baada ya kushikanashikana kwa muda mrefu huku wakihema kwa kasi, walipanda kitandani, chumbani kwa shemeji mtu huyo wakaendelea kula raha ya mahaba mazito kiasi kwamba, hakuna aliyekumbuka kwamba mwenye nyumba anaweza kuzuka wakati wowote kwani hawakuona hata sababu ya kufunga mlango.

Muda huo walikuwa kwenye kipindi cha kwanza cha mchezo ambapo dada wa Aisha alikuwa amejiachia kwa lolote lile na maneno mengi ya kumfanya Beka kuweka akili zake zote kwake na kuachana na mkewe.
Hata staili za mwanamke huyo zilikuwa za kumteka akili Beka kwani kuna wakati alimlaza Beka chali halafu yeye akapanda baiskeli na kuanza kuzungusba pedeli kwa spidi ya ajabu hali iliyomfanya mwanaume huyo kupiga kelele yeye badala ya shemejiye…

"Basi mume wangu, usipige kelele sana," alisema shemeji mtu akimwambia Beka kwa sauti yenye mahaba mazito huku akimwangalia kwa macho ya mlegezo na mahaba.Beka alishindwa kuvumilia kupekechewa baiskeli, akatangaza lakini shemeji mtu alipinga tangazo lako, ikabidi asitishe kupiga pedeli, akabadili mapozi, akajitegesha na ile ya mbuzi kupinga kutembea halafu Beka akamfuata kwa nyuma.

***
Aisha alikaa kwa Diana kwa muda halafu akaaga na kurudi nyumbani kwake akihakikisha anaingia ndani bila kujulikana labda kama atakuta mlango umefungwa.Ufungwe wapi! Aliukuta upo wazi, akazama ndani kwa kunyata. Alikuta sebule ipo kimya, akapita hadi jikoni ambako hakumkuta mtu, akakatiza hadi chumbani kwake, akafungua mlango, akakuta kitanda tu.

Aisha alibaini kuwa mume wake yupo ndani baada ya kuliona begi lake analopenda kulibeba begani. Akajua atakuwa ndani ya chumba cha dada yake, akasimama na kujipanga aingieje sasa!"Nikisema niingie kwa pupa naweza kusababisha makubwa, mimi nina hasira zangu. Dada ni mtu anayeweza kufanya lolote lile. Beka yeye hajui kupiga lakini pia ni mkorofi, hasa akikasirika…

"Lakini atakasirikaje wakati anayestahili kukasirika ni mimi? Hii si sawa, yaani nitendewe halafu niwe mpole! Haiwezekani."Alitembea bila kusababisha kutambulika hadi kwenye mlango wa chumba cha dada yake ambapo aliweza kusikia minong'ono na mihemo ya kimahaba kutoka pande zote mbili. Tena aliweza kumsikia dada yake akiomboleza mapenzi.

Mwisho wa yote aliamua kugonga mlango ili kuwajulisha kwamba kuna mtu amesimama hapo mlangoni…
"Ngo ngo ngooo…"

Kule ndani, wote walishtuka kusikia hodi. Beka akamsukuma shemejiye kutoka kwake, akaanza harakati za kupanda juu ya kidirisha cha kuzamia darini ili atembee hadi akatokee kwenye bafu la chumba chake kama alivyofanya siku ya nyuma.

Aisha alishika kitasa cha mlango akazama ndani na kumkuta dada yake akihangaikia kanga, mumewe amejiingiza kwenye kidirisha nusu, yaani kuanzia kiunoni kwenda juu kumeingia lakini sehemu nyingine iliyobaki ikiwa nje.

Aisha aliachana na dada yake, akapanda kitandani na kumshika mumewe ili asimalizikie kuingia…
"Nimekuona, unakwenda wapi Beka?" alisema Aisha akiwa ameing'ang'ania miguu ya mumewe.
Ilibidi Beka ajiachie na kurudi kitandani. Hakuwa na nguo hata moja kiasi kwamba hata kama angefanikiwa kuchomoka, bado nguo zake zingekuwa ushahidi mkubwa kwamba alikuwemo ndani ya chumba hicho.

Dada mtu kuona hivyo, alitimua mbio hadi nje akiwa amejifunga kanga moja tu! Alikuwa akihema kwa kasi…
"Ooo…ooph…oooh!"
Baadhi ya majirani kule nje walianza kuingiwa na shaka kwa jinsi dada wa Aisha alivyotoka na kanga moja jambo ambalo si la kawaida.

Na yeye alipobaini kwamba amesimama nje na kanga alirudi ndani mbio, akafikia sebuleni. Bado Aisha na mume wake walikuwa chumbani kwake wakizozana…"Mimi ndoa basi tena. Wewe umeona dada yangu ni bora kuliko mimi, si ndiyo? Basi ishi naye," alisema akilia Aisha. Beka alimshika mkono kwa sababu alikuwa akitaka kutoka…

"Nisamehe sana mke wangu, ni shetani tu alinipitia."
"Shetani yupi? Shetani yupi!"
"Shetani wa vishawishi. Sasa na mimi ndiyo nimetambua ubaya wa huyu shetani, lengo lake lilikuwa kuvunja ndoa yangu na wewe."

"Nimesema mimi ndoa na wewe basi tena," alisisitiza Aisha.
Alifanikiwa kuchomoka kutoka kwenye mikono ya Beka alipofika sebuleni akamkuta dada yake amesimama akitetemeka…

"Mdogo wangu nisamehe sana mimi dada yako. Ni shetani tu alinipitia, naamini haitajirudia," alisema dada mtu.Aisha hakumjibu, aliifuata simu yake aliyoiacha kwenye sofa na kubonyeza namba. Wakati huo, Beka naye alishatoka na kuwakuta sebuleni, mkewe na shemejiye. Aisha alikuwa ameipeleka simu sikioni akiashiria kutaka kuongea. Si Beka wala dada mtu aliyehisi anataka kuongea na nani.

Mara akaongea…
"Shikamoo shemeji…sijambo…si nzuri sana shemeji…shemeji nimemfumania mkeo na mume wangu…amini nakwambia…shemeji kumbe mkeo kaja kwa ajili ya…" kabla hajamaliza kusema Aisha huku akilia, Beka alimpokonya simu kwa kuikwapua…

"Ha! Dada ako amefikia huko?" uliuliza upande wa pili lakini sasa simu alikuwa nayo Beka…
"Haloo mkubwa…" alianza kusema Beka…
 
MH! MISSED CALL YA SHEMEJI!-13

ILIPOISHIA
" kabla hajamaliza kusema Aisha huku akilia, Beka alimpokonya simu kwa kuikwapua…
"Ha! Dada ako amefikia huko?" uliuliza upande wa pili lakini sasa simu alikuwa nayo Beka…
"Haloo mkubwa…" alianza kusema Beka…
SASA JIRUSHE NAYO…

Ee, ni nini kimetokea mkubwa?" alihoji mume wa dada wa Aisha huko aliko…
"Hamna kitu bwana, unajua wametofautiana hawa, sasa mke wangu akahisi labda mimi natembea na mkeo, yaani shemeji yangu, inawezekana kweli we unavyoona?" aliuliza Beka.

"Hamna shemeji, nimewakuta kabisa kitandani, wako kama walivyozaliwa, asikudanganye huyo," alisema kwa sauti ya juu Aisha iliyomfikia wa upande wa pili naye akajibu…

"Mimi sijui kitu bwana Beka, nyie ndiyo mpo huko. Kama ni kweli au si kweli mnajua wenyewe. Lakini sina cha kusema. Huyo mwanamke nilimwacha kwa mambo hayo ya kusaliti, yeye hata vijana wadogo kiumri kwake anataka kutembea nao, ndiyo tatizo lake kubwa," alisema mume wa shemeji wa Beka kisha akakata simu.

Beka alionekana kushtuka sana simu kukatwa, akajikuta ameduwaa na simu ya Aisha mkononi, naye mwenyewe akaikwapua na kuminya namba nyingine.Beka aliduwaa zaidi, dada mtu yeye machozi hadi kwenye ncha ya kidevu. Kutoka moyoni alikiri kwamba amekuwa akimtendea mdogo wake ubaya uliopitiliza. Kuna sauti ilikuwa ikimwambia…

"Sasa wewe, wanaume wote hao umewaona hawafai hadi kuamua kutembea na shemejio, mume wa mdogo wako wa kuzaliwa tumbo moja, baba mmoja mama mmoja? Kumbe we hufai!"
Hii sauti ilimuuma sana dada mtu huyo, akatamani ardhi ipasuke ili yeye azame ndani yake na kuachana na aibu ya dunia hii.

Aisha aliweka simu sikioni baada ya kumaliza kubonyeza namba akatulia kidogo kusikiliza, kisha akasema…
"Eee shikamoo mama…mama dada nimemfumania na mume wangu, hivi kweli mama dada anaweza kunifanyia…" kabla hajamaliza kusema, Aisha aliangua kilio, dada yake akaiwahi simu na kuiweka sikioni yeye kisha akaongea na mama yake….

"
Kwa nini umempokea kwanza mtu asiyekuwa na heshima?" dada mtu alimkuta mama yake anamalizia kusema hayo…
"Mama, ni mimi…"
"Umefanya nini huko wewe?"
"Mama si kweli, ni mawazo yake tu huyu…."

"Mama kweli, nimewakuta kitandani hawana nguo," alisema Aisha kwa sauti ya juu, mama yake akaisikia…
"Unasema anakusingizia, mbona anasema amekukuta kitandani kabisa?"
"Ah! Mama bwana, usimsikilize huyu…"

"Nijibu, amewakuta kitandani au hajawakuta kitandani?" aliuliza kwa hekima mama mtu…
"Mimi sikumbuki mama kama nilikuwa kitandani na mume wake."
"Hukumbuki?"
"Ndiyo."
"Unaugua kichaa siku hizi?"
"Kivipi?"

"Yaani ushindwe kukumbuka kitu kama hicho?" alisema mama mtu huyo na kukata simu kwa hasira. Alitetemeka, akajikuta anaishiwa nguvu, akakaa chini.

"Hivi kweli kabisa huyu mtoto anaweza kufanya hivi kwa mume wa mdogo wake? Si afadhali mdogo wake ndiyo angemfanyia yeye hivi, tungesema akili za kitoto?
"Halafu ni kweli kabisa wamefumaniwa, hata maelezo yake yanaonesha. Eti sikumbuki, anamdanganya nani?"

"Dada kifupi sitaki kukuona humu ndani kuanzia sasa hivi," alisema mdogo mtu huyo huku akimtumbulia macho ya hasira. Alionekana kutaka kumvaa wakati wowote ule…
"Kwa hiyo niende wapi?" aliuliza.
"Sijui, kwani umetokea wapi? Unakuja hapa unasema umeachwa kumbe umejiacha mwenyewe, kama hii tabia umekuja nayo kutoka kwako si ndiyo maana mumeo alikupiga chini."
Mara, simu ya mama yao iliingia kwenye simu ya dada mtu, akaipokea kwa uvivu na kujifikiria sana…
"Eee mama…"

"Sikia, panda gari njoo huku, baba yako anasema uje haraka sana," mama akakata simu.
Mara simu ya Aisha ikaita, akaipokea haraka sana baada ya kubaini ni ya mama yake…
"Haloo mama…"

"Baba yako anasema uje huku haraka sana. Sasa utakuja lini mwanangu?"
"Mimi nitakuja kesho mama, nitatoka huku asubuhi sana."
Mazungumzo yote hayo, Beka alikuwa akiyasikia, moyo ulimwenda kwa kasi akiwa haamini nini kimetokea. Moyoni alijuta sana, alijua anampoteza mkewe hivihivi anaona…

"Da! Shetani bwana, kweli ana nguvu. Lakini naamini Mungu ana nguvu zaidi kwani yeye kaweka sheria zake tu, ningezifuata haya yote yasingetokea," alisema moyoni Beka. Mwishowe akasema…
"Ah! Mi naliacha liserereke lenyewe tu, nitafanyaje sasa?"

***
Usiku wa siku hiyo ulikuwa mrefu sana kwa wote watatu, pengine hata na wazazi wao kule kijijini.
Kila mmoja aliwaza la kwake na hatima yake. Aisha alipata wakati mgumu zaidi kwani aliwaza afanye nini ili yaliyotokea yawe kama hayakuwahi kutokea na aendelee kuishi na mumewe, Beka?
"Yaani kama ananisaliti kwa dada yangu, basi kwa marafiki zangu ni zaidi," alisema moyoni Aisha akiwa amelala akiangalia juu, yaani alilala chali.

"Hivi, lakini mimi kosa langu nini? Kama mke mwenyewe namuomba unyumba hataki, ningefanyaje sasa?" aliwaza Beka naye akiwa amelala akiangalia juu.
Aisha alishindwa kuvumilia, akamwita mumewe…
"Beka…"
"Nini?"

Sasa Beka alianza kuwa mkorofi f'lani hivi kwa mkewe baada ya kuwaza yake…
"Yaani mi nakuita unasema nini?"
"Ulitaka niitikiaje?"
"Kwani siku zote unaitikiaje?"
"Hebu niambie unachotaka kusema…"
 
MH! MISSED CALL YA SHEMEJI!-14

ILIPOISHIA
Sasa Beka alianza kuwa mkorofi f'lani hivi kwa mkewe baada ya kuwaza yake…
"Yaani mi nakuita unasema nini?"
"Ulitaka niitikieje?"
"Kwani siku zote unaitikiaje?"
"Hebu niambie ulichoniitia…"
JIACHIE NAYO SASA…

"Oke, ni kwa nini umenisaliti kwa dada yangu?"
"Hilo swali jijibu mwenyewe."
"Kwa nini?"
"Kwa sababu unajua ni kwa nini?"
"Mimi sijui ndiyo maana nimekuuliza wewe."
"Na mimi najua wewe unajua ndiyo maana nimesema ujijibu mwenyewe," alisisitiza Beka kwa sauti isiyotaka utani.
"Mimi sijui, ila kusema ukweli nimeshtuka sana."
"Hata mimi nilikuwa nashtuka sana."
Aisha aliamua kukaa kimya huku akiwaza mengi kichwani. Hakumwambia mumewe kwamba kesho yake anakwenda kijijini ameitwa na wazazi.

***
Asubuhi na mapema, Aisha alitoka kitandani, akaenda kuoga. Aliporudi alijiandaa, akatungua mkoba wake na kuweka baadhi ya nguo. Beka alishuhudia tukio hilo lakini hakumuuliza.
Alipomaliza Aisha, alibeba begi na kuliweka begani ndipo akasema…
"Mimi nasafiri, nakwenda nyumbani wazazi wameniita."
"Oke," alijibu kwa mkato Beka. Hakuuliza kuna nini wala mbona unaniambia kwa kunishtukiza!
Aisha alipotoka alikuta mlango uko wazi, akajua dada yake naye ameshatoka kitambo. Kila hatua tano mbele alitupa macho kama atamwona dada yake, lakini haikuwa hivyo.

***
Mabasi stendi kuu ya kwenda kijijini kwao yalikuwa mengi lakini Aisha alichoomba ni asipande basi moja na dada yake hivyo kabla ya kukata tiketi alichungulia ndani kwanza. Alipata basi ambalo aliamini dada yake hajapanda.

***
Beka aliamka saa moja juu ya alama, akatoka na kuangaza huku na kule. Alibaini shemeji yake naye alitimua zake baada ya kwenda chumbani kwake na kumkosa. Hata begi lake halikuwepo!
"Liwalo na liwe. Atakaloamua Aisha ndiyo hilohilo. Yeye ni mke wangu ni kwa nini alikuwa ananikatalia kunipa tendo la ndoa, anadhani ningeishije. Naamini hilo ndiyo limechangia mimi kufanya vile," alisema moyoni Beka huku akirudi chumbani kulala kidogo.
Ni ukweli usiopingika kwamba Beka amekuwa na wakati mbaya kwa mkewe kuhusu unyumba, mara nyingi amekuwa akimkatalia hata kwa miezi mitatu bila sababu za msingi. Beka, pamoja na kufanyiwa yote hayo hakuwahi kumsaliti mkewe.
Kuwepo kwa dada yake ndani ya nyumba na tabia yake ya kushobokea ndiko kulisababisha Beka ajikute akitumbukia katika mtego wa mapenzi kwa shemeji yake huyo.

***
Aisha ndiye aliyetangulia kufika nyumbani kwao kijijini na kumkuta mama yake amelazwa kwenye zahanati ya kijiji hicho kwa matatizo ya presha.
Baada ya kupata taarifa za tukio la usaliti alilolifanya binti yake mkubwa kwa mume wa mdogo wake alipata msongo mkubwa na kusababisha presha ya kushuka.
Aisha alishangaa kukuta dada yake hajafika. Alimwambia baba yake kwamba yeye dada mtu ndiye aliyeanza kutoka nyumbani asubuhi. Wakiwa wanajadili, dada mtu aliingia…
"Shikamoo baba."
"Marahaba," aliitika mzee huyo bila hata kumuuliza za safari kama alivyofanya kwa Aisha.
Dada mtu huyo alipitiliza hadi ndani akatua begi lake. Aliwauliza wadogo zake wengine aliko mama yake…
"Mama amelazwa hospitali."
"Anaumwa nini?"
"Presha."
Dada mtu huyo alikwenda kwenye zahanati hiyo ambayo anaijua na kumkuta mama yake kidogo ana nafuu. Pia alimkuta Aisha, maana wakati yeye anafika nyumbani Aisha alikuwa anatoka.
"Shikamoo mama," alimsalimia lakini mama mtu huyo alimtumbulia macho tu kama anayemsuta kwa tabia yake chafu aliyoifanya…
"Pole mama," alisema. Lakini bado mama mtu huyo hakuitikia zaidi ya kutoa macho.
Ilimbidi dada mtu huyo ageuke kurudi nyumbani huku akiwa anamwaga machozi mwenyewe. Alianza kuhisi hali ni mbaya sana nyumbani hapo.

***
Jioni ya saa moja kulikuwa na kikao nyumbani na ni baada ya mama yao kutoka zahanati akiwa anajisikia nafuu sana.
Baba yao ndiye aliyeanza kuongoza kikao hicho huku akionekana kutetemeka midomo kwa hasira…
"Ime," alianza kusema baba mtu huyo kwa kumtaja jina dada wa Aisha. Wakati huo watoto wote walitakiwa kuingia ndani vyumbani mwao…
"Abee baba."
"Ni nini umekifanya kwa mdogo wako Dar es Salaam?"
Dada mtu huyo akikaa kwa muda wa kama dakika moja nzima kabla ya kusema chochote halafu ndipo akaamua kusema…
"Wazazi wangu, mimi nakiri kutenda kosa. Nimetembea na shemeji yake Beka. Ni kweli mdogo wangu alitufumania."
Ukimya wa sekunde kadhaa ulimfanya baba mtu huyo kuendelea…
"Ni kwa nini uliamua kufanya kosa kubwa kama hilo?"
Dada mtu huyo akatulia tena kidogo kisha akafunguka…
"Wazazi wangu, kusema ule ukweli nilijikuta nikiangukia kwenye dhambi ile baada ya shemeji mwenyewe siku moja kunishitakia. Aliniambia shemeji afadhali umekuja, mdogo wako amekuwa akinitesa sana kwenye ndoa.
"Mimi ni mume wake lakini anadiriki kunikatalia kunipa unyumba. Inaweza kupita hata miezi miwili mpaka mitatu hajanipa unyumba. Nilishtuka sana kusikia hivyo."
Baba mtu na mama mtu walionekana kushtushwa na kipengele hicho, wakamgeukia Aisha…
 
Back
Top Bottom