Miss Tanzania,Nape Nnauye,tunataka Taji letu

ZamdaIssa

JF-Expert Member
Nov 10, 2015
879
1,456
Heshima kwenu wana jamvi wenzangu..Kwanza nianze na masikitiko makubwa niliyonayo juu ya Kamati nzima ya Miss Tanzania,Waziri wa Habari na Michezo mh Nape Nnauye,kiukweli munatuumiza sana watanzania,munatufanya tuuchukie UTanzania wetu!!HAMJATOA TAMKO LOLOTE KUHUSU HILI MPAKA SASA

Miss Tanzania 2016 Diana flave amedhurumiwa ushindi wake,amepokonywa Taji lake!Tanzania pia tumeonewa na Wakenya katika Taji la Miss world-Africa...Lakini sijasikia Waziri akiliongelea,ila angekuwa amekamatwa msanii na madawa ya kulevya basi ungeona Nape anaitisha Press Conference kulalamika kwamba msanii anaharibiwa BRAND,ila hapa amekaa kimyaaa!!!Shame on You Kamati ya Miss Tanzania

Kama munakumbukumbu nzuri huko Nyuma,Diana alisema kwamba miss Kenya Evelyn Njambi sijui huko,amemuibia Documentary yake ya Beuty with purpose inayohusu FGM(ukeketaji kwa wanawake).

Wote tulishuhudia jinsi Diana alivyoonyesha documentary hiyo ya "masai dondosha wembe" katika kinyang'anyiro cha Miss Tanzania na akaweza kushinda...

Alivyofika Miss World Diana aliibiwa documentary yake na mrembo wa Kenya ambaye ndie Miss Africa,Evelyn..Mkenya huyo alienda mpaka kwenye kamati ya Miss world kabla ya mchujo na akawaambia kwamba kuna mshiriki kutoka Tanzania ameiba Documentary yangu,Kamati ilimuamini na Diana alikatwa jina mapema saana!!

Ukweli ni kwamba Diana ndiye aliyeibiwa Documentary,na ameambatanisha na ushahidi kwamba yeye alipandisha video yake huko Youtube tarehe 18 oct 2016 na ikarudiwa tena 24,lakini mrembo wa kenya aliiba..maelezo ni marefu sana,nadhani Diana mwenyewe ataeleza kwa kina...

Waziri tunaomba utusaidie,Miss Tanzania muliopita tunaomba mutusaidie,tunaomba vyombo vya habari hasa Clouds na kamati nzima ya Miss Tanzania,kwenda huko alikoshoot hii documentary Diana na kufanya research kwa kina tena kwa kuwafinyia enterview main character wote walioshiriki kutengeneza documentary hii na kisha kuipeleka Miss World tena kwa mkono!!

Inawezekana kabisa mrembo huyu wa Kenya akavuliwa taji la Miss Africa alilopewa kutokana na Documentary yetu aliyoiiba kutoka kwa Diana na taji ikarudi nyumbani Tanzania!!

kama ilivyofanyika kwa AllyKiba basi na hii tufanye hivyohivyo.
Justice for Diana,Justice for Tanzania
Screenshot_2017-03-05-13-36-40.png
Screenshot_2017-03-05-13-50-35.png
 
Ishatoka hiyo.

Dianna hakustahili hata kuwa miss mtaa so aridhike na kidogo alichokipata
 
Mashindano ya urembo hayana tija waziri ana issue muhimu za kusolve
 
Back
Top Bottom